Rais Samia Suluhu Hassan ameanza mchezo vizuri sana

Rais Samia Suluhu Hassan ameanza mchezo vizuri sana

Anapambana na Coronavirus ??

Kafungua wafungwa wa kisiasa ?

Twitter iko hewani ??

Wamekufa watu 45 taifa katia hata pole ??

Azory Gwanda, Ben Saanane, Lissu, Kanguye, viroba: Ukweli ukoje ???

Kuna Jipya gani ???

Usiwe na matumaini sana utakuja very disappointed.

Huyo mama hana Jipya wala vision yoyote.
wewe unapambanaje na Corona, unajuwa watu wengine mnaakili za ajabu
 
Uzalendo upi unaomaanisha mkuu? Njaa haina uzalendo......na kuishi maisha magumu yenye changamoto haimaanishi ndiyo uzalendo
Simaanishi kwamba uzalendo ni maisha magumu! Namaanisha kwamba mimi ni mzalendo, na naitakia nchi yangu mema! Natamani tuwe na utawala bora kabisa, na nchi yetu ipige hatua. Natamani elimu bora itakayo jenga uzalendo wa kweli, lakini naheshimu diplomasia na uhusiano wa kimataifa, pia! Sisukumwi na njaa kuwaza na kusema haya! Naipenda sana Tanzania, na naiombea, jiunge nami, hata kama Una njaa!
 
Simaanishi kwamba uzalendo ni maisha magumu! Namaanisha kwamba mimi ni mzalendo, na naitakia nchi yangu mema! Natamani tuwe na utawala bora kabisa, na nchi yetu ipige hatua. Natamani elimu bora itakayo jenga uzalendo wa kweli, lakini naheshimu diplomasia na uhusiano wa kimataifa, pia! Sisukumwi na njaa kuwaza na kusema haya! Naipenda sana Tanzania, na naiombea, jiunge nami, hata kama Una njaa!
Mi nimetapeliwa sana na kujifanya mpenda haki naona bila rushwa ,kujuana na mtu hutoboi nchi hii trust me, kama unabisha nenda ofisi yoyote ya ardhi, na sehemu nyingine utakazohitaji huduma
 
Mi nimetapeliwa sana na kujifanya mpenda haki naona bila rushwa ,kujuana na mtu hutoboi nchi hii trust me, kama unabisha nenda ofisi yoyote ya ardhi, na sehemu nyingine utakazohitaji huduma
Kuwepo mambo hayo hakufanya, neno haki lifutike kwenye kamusi! Uongo mwingi hauwezi kufanya kusiwepo existance ya ukweli! Sijafukia kichwa changu kwenye mchanga kama mbuni, najua sana uwepo wa matatizo hayo! Nina miliki gari, nina pasipoti, nina hati miliki ya viwanja nk! Naelewa lugha unayo zungumza, lakini kuwa mzalendo ni uchaguzi wa Mtu, siyo external force yoyote!
 
Kuwepo mambo hayo hakufanya, neno haki lifutike kwenye kamusi! Uongo mwingi hauwezi kufanya kusiwepo existance ya ukweli! Sijafukia kichwa changu kwenye mchanga kama mbuni, najua sana uwepo wa matatizo hayo! Nina miliki gari, nina pasipoti, nina hati miliki ya viwanja nk! Naelewa lugha unayo zungumza, lakini kuwa mzalendo ni uchaguzi wa Mtu, siyo external force yoyote!
Nikweli ila kuna vikwazo vingi vya uzalendo vinavyokufanya kukurudisha nyuma kwenye imani ya uzalendo
 
Kuanza hua haiwi shida mkuu, Tatizo hua ni concistance ya kile ulichokianza.

Mungu amsaidie Rais wetu maana tunajua
 
Nikweli ila kuna vikwazo vingi vya uzalendo vinavyokufanya kukurudisha nyuma kwenye imani ya uzalendo
Ni kweli lakini kukubali vikwazo vituzuie kusonga mbele, ndo unyonge wenyewe! Mimi nina watoto wadogo, na taifa lina kizazi kingine ambacho, tunaweza kuwekeza ili kuwe na better future!
 
Ni kweli lakini kukubali vikwazo vituzuie kusonga mbele, ndo unyonge wenyewe! Mimi nina watoto wadogo, na taifa lina kizazi kingine ambacho, tunaweza kuwekeza ili kuwe na better future!
Uko sahihi, ila njia unayoipita wewe nchi inaelekea upande mwingine
 
Hivi Kigogo2014 ni nani? Nabii? Mtabiri wa Taifa? Whistle blower? Mshauri? Mkosoaji? Au mtukanaji? Natamani kujua hasa nini kusudi, dhamira ya taasisi hiyo kwa Taifa letu.
Ni kijana wetu wa Bumvuli
 
Hivi Kigogo2014 ni nani? Nabii? Mtabiri wa Taifa? Whistle blower? Mshauri? Mkosoaji? Au mtukanaji? Natamani kujua hasa nini kusudi, dhamira ya taasisi hiyo kwa Taifa letu.
Ni Whistle blower!
 
Kubadilisha mawaziri huwa siyo issue kabisa kwani bado atapata mawaziri kutoka kule kule CCM. Ishu ni kuwasimamia bila woga wala aibu kama ambavyo Magufuli alivyokuwa- hadi hata Mama Samia mwenyekwe aliwahi kukiri kuwa Magufuli aliwanyoosha- hata Mama Samia Suluhu naye alivyooka wakati wa Magufuli! Sasa na yeye ni wajibu wake, inabidi awanyooshe hao mawaziri kwanza, hata kama atatumia mawaziri wale wale mradi awanyooshe kwanza. magufuli alikuwa ni no-nosense man, Samia anatakiwa pia kuwa ni no-nosense woma; nchi yetu haiendelei kwa kubadilisha mawaziri inaendelea kwa mawazir walioko kufanya kazi kweli.
View attachment 1739977
Huu ni ushamba! Uongozi haufanikiwa kwa kufokea watu na kuwadhalilisha watu wazima wenzio! Inatosha kufuata sheria na taratibu katika kuhakikisha kila waziri na manaibu wao wanatekeleza wajibu wao. Ukiona mtu ana uongozi wa aina hii yaani 'populist' ni hatari kwa ustawi wa nchi. Kama wengu tulivyoshuhudia nchi ilivyopelekwa kishamba na huyo mwendazake!
 
Huu ni ushamba! Uongozi haufanikiwa kwa kufokea watu na kuwadhalilisha watu wazima wenzio! Inatosha kufuata sheria na taratibu katika kuhakikisha kila waziri na manaibu wao wanatekeleza wajibu wao. Ukiona mtu ana uongozi wa aina hii yaani 'populist' ni hatari kwa ustawi wa nchi. Kama wengu tulivyoshuhudia nchi ilivyopelekwa kishamba na huyo mwendazake!
Basi hujui uongozi bali unajua siasa na kubembelezana. Uongozi ni stick and carrot!!

Jeshini huwa kuna kozi inaitwa ledareship; mojawapo ya tenets za leadership ni kwa leader kuwa above wale anaowaongoza. Leaders wa jeshini hufundishwa kutumia njia kama uwatupa lupango mara kadhaa wafuasi wao wasiofuata oda zao - yaani stick.
 
Basi hujui uongozi bali unajua siasa na kubembelezana. Uongozi ni stick and carrot!!

Jeshini huwa kuna kozi inaitwa ledareship; mojawapo ya tenets za leadership ni kwa leader kuwa above wale anaowaongoza. Leaders wa jeshini hufundishwa kutumia njia kama uwatupa lupango mara kadhaa wafuasi wao wasiofuata oda zao - yaani stick.
Hizo zama zenu za stick leadership zimepitwa na wakati! Kiongozi ni Sawa na Sisi, hayupo above, tunatofautiana majukumu tu! Tukipata kiongozi anayeelewa kwamba binadamu wote ni Sawa, tutapata maendeleo!
 
Mama Anacheza game kwa umakini sana,anajua hawezi Watema MATAGA kwa sasa,anawahitaji kupanga safu yake,along the way,mchele na pumba utajitenga tu

Hata hawa activists wa mitandaoni ameanza nao vizuri,full kuwapiga chenga,Kuna msemo mmoja niliusikia Aliutoa Jk Juzi Kati kwenye mazishi naona ndio unafanya kazi sasa,MSICHEZE NGOMA YA ADUI,Mpaka Msigwa kapigwa chenga Jana.

Kwa kifupi Ana washauri wazuri,teuzi zilizofanyika sasa ni kujitoa lawama,ila anajua alichofanya,ndio maana mwisho Alitoa angalizo..
Report ya TAKUKURU Ikitoka,itabeba wengine,anakutoa ofisini kwa ushahidi,inaonekana anaanza kuzipa taasisi meno kama ataendelea hivi

Itamlazimu,nasema tena,Itamlazimu Kuheshimu KATIBA Sababu namna ya alivyopata Urais wake kuna watu Wamesimamia na kuheshimu Misingi hiyo ya KATIBA,Pasi na Shaka hili ni deni Kubwa sana alilonalo..

KERO ZA MUUNGANO Ameishaanza kuzivalia njuga Kabla hata hajaanza,Ni mzanzibari,kwa teuzi alizofanya tutegemee mabadiliko mengi kwenye muungano,rejea Maagizo aliyotoa kwa Waziri wa fedha..

Kwa kifupi huyu Mama KATIBA ataitendea haki,kwa mawazo yangu,ni kitu kiko kichwani mwake kabisa,rejea slip tongue aliyoifanya jana katika teuzi za Baraza la mawaziri..

Niwatakie siku njema...
🙏🙏
 
mpaka leo hujawahi kumwelewa tu?
Hivi Kigogo2014 ni nani? Nabii? Mtabiri wa Taifa? Whistle blower? Mshauri? Mkosoaji? Au mtukanaji? Natamani kujua hasa nini kusudi, dhamira ya taasisi hiyo kwa Taifa letu.
 
Huu ni ushamba! Uongozi haufanikiwa kwa kufokea watu na kuwadhalilisha watu wazima wenzio! Inatosha kufuata sheria na taratibu katika kuhakikisha kila waziri na manaibu wao wanatekeleza wajibu wao. Ukiona mtu ana uongozi wa aina hii yaani 'populist' ni hatari kwa ustawi wa nchi. Kama wengu tulivyoshuhudia nchi ilivyopelekwa kishamba na huyo mwendazake!
Mkuu Mungu ameturudisha kwenye dunia, Tupo na binadamu wenzetu, Sisi siyo kisiwa tena!
 
Back
Top Bottom