Rais Samia Suluhu Hassan amekuja kuizika kabisa CHADEMA

Rais Samia Suluhu Hassan amekuja kuizika kabisa CHADEMA

Lizaboni

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2013
Posts
33,895
Reaction score
20,392
Wadau, amani iwe kwenu.

Katika historia ya upinzani nchini, mwaka 2015 ulikuwa ni uchaguzi ambao ulitushughulisha sana wana CCM. Hata hapa kwenye jukwaa mijadala ilikuwa ni mikali na mnyukano kati ya CCM na CHADEMA ulikuwa wa wazi.

Nakumbuka wakati huo ukianzisha mjadala wa kumshambukia kiongozi wa CCM ama upinzani thread ilikuwa inatembea sana.

Hali ya kisiasa wakati huo ilibebwa na uamuzi wa Lowasa kuhamia CHADEMA. Ni kwa mazingira hayo hata sisi ndani ya CCM tuligawanyika na ndo maana upinzani ulipata nguvu.

Binafsi nilikuwa ni wafia chama hasa wa kambi ya CCM. Nikawa natumia nondo nilizokuwa nazo kumgonga hasa Lowasa. Nilifanikiwa kupata mikakati yake mingi na kuiumbua kabla haijafanikiwa. Aisee nilitisha sana wakati ule.

Baada ya CCM kuibuka ushindi katika uchaguzi ule, binafsi niliona nimeshamaliza kazi na nikaamua kuja hapa Uingereza kujiendeleza kimasomo na kula bata.

Uchaguzi wa 2020 haukuwa na upinzani kabisa isipokuwa CHADEMA walibebwa na tukio la Lissu kupigwa risasi ambalo wao wenyewe ndio walilitengeneza kwa maslahi yao ya kisiasa. Bahati mbaya sana mtaji huo haukuwalipa na CCM tukashinda kwa kimbunga.

Uchaguzi wa 2025 nauona ukiwa wa upande mmoja kwa asilimia 95. Mtaji wa risasi za Lissu haupo tena na CHADEMA hawana agenda za kuwaambia wananchi. Kila wanalofikiria mama keshatangulia kitambo. Si mmewaona juzi kwenye mkutano wao wa hadhara! Wamebaki kuisifi CCM na Rais mama Samia. Kawazidi kete. Kwa sasa watajitutumua kiasi ila kampeni za 2025 mtaona zitakavyododa kwa upande wao.

Hongera sana Mheshimia Mama Samia. CHADEMA mwendo wameumaliza
 
Wananchi wameamua kujiongeza vingine,, hizi siasa wote matapeli tu sio side A wala side B sahivi saka ugali wako na wanao tu hata kama hali ndo hivyo
 
Nchi imepiga hatua kubwa sana kimaendeleo. Wananchi bado wana imani na CCM na mama ndiye kaja kuizika kabisa CHADEMA
 
Chadema bado tuna imani nao na Mama anaupiga mwingi kwanza ni mpenda haki hivyo ccm mnaumia maana mlimpenda yule katili lakini mama ni chaguo la Mungu mwenyewe
 
Nchi imepiga hatua kubwa sana kimaendeleo. Wananchi bado wana imani na CCM na mama ndiye kaja kuizika kabisa CHADEMA
Siasa za maji taka zilishakwisha, Labda kama haukuwa Tanzania miaka saba ya Magufuli

Sema jalada la Magufuli limefungwa rasmi

Chadema ife au ccm ife, Watu hatutaki tena siasa za utekaji watu Siasa za Wasiojulikana, Siasa za kuharibu biashara za watu

Tulikuwa na siasa zetu safi kabla ya 2015 za utani na kutaniana
 
Hatuhitaji story za Abunuwasi hapa JF na siasa za maji taka tena iwe za ccm au Chadema au chama chochote

Siasa za maji taka za Kutishia watu, zimemtesa mpaka Max Melo

CCM na Chadema vilishazikwa kwa miaka saba na JPM, Unataka vizikwe mara ngapi?

Wana ccm walijitoa ufahamu kwa kuogopa Kutekwa na kujazana uwanjani kuimba kwa ajili ya bombardier sio watu wazima mpaka watoto, Unashangaa kweli nchi hii tunaimba nyimbo na kuacha kazi kisa bombadier

Wana chadema nao wali unga juhudi kuogopa kutekwa

Siasa zenu za maji taka zimeharibu uchumi wa nchi, Leo tunaanza upya kabisa kutengeneza taasisi imara na urafi na mataifa makubwa

CCM mlisababisha watu wafurahie vifo vya viongozi wao wakati wa awamu ya tano

Taifa lilijaa ukabila na kila aina ya ujinga na upumbavu kwa miaka saba ya JPM

Mama anairudisha nchi kwenye siasa zake safi, Wewe unasema anaizika chadema

Mbinu za kuizika Chadema zilipofeli mkaanza Kuteka wananchi na kubaka

CCM yenyewe watu walishindwa kuizika mpaka sasa ipo, Waliotaka kuizika ccm wote hawapo na ccm ipo

Siasa zenu za maji taka zilizalisha watu kama akina Sabaya, Makonda, Mnyeti

Leo hapa JF ukiongelea story za kuzika chama unaonekana una matatizo makubwa kichwani

Siasa za maji taka za awamu ya tano ziliwatesa wana ccm kama akina Mzee Kinana, Mzee Makamba na Bernard Membe

Siasa za maji taka ziliitesa Chadema kama akina Mbowe kuitwa Gaidi na Lissu kupigwa risasi

Leo unakuja hapa eti Mama anaizika Chadema, hujui tayari maziko ya ccm na chadema yalikwisha fanyika

Mama Samia na Freeman Mbowe ndio Mashujaa kwa sasa wanafukua tena makaburi na kuwaambia wana ccm na chadema amkeni aliyewazuia Yeye hayupo tena

Wewe kwa sasa kubali au kataa Mama Samia na Mbowe ndio wataleta katiba mpya, Wamesha anza kuonyesha njia kuwa Polisi na Raia wanaweza cheka si umeona mikutano ya chadema
 
Kila kitu unachokisikia yawezekana ukakakielewa au ukawa hujakielewa hivyo usikurupuke jipe muda maana kwa siasa zetu za Tanzania na tunavyozifahamu na naamin wananchi wengi wameelewa siasa zetu na wanasiasa wetu tulionao kwa sasa,tunaweza kudhani tunayowaza ndio wanayowaza watanzania kumbe ikawa sivyo,hivyo muda utatuambia vizuri kabisa nn kitajiri.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Katika historia ya upinzani nchini, mwaka 2015 ulikuwa ni uchaguzi ambao ulitushughulisha sana wana CCM. Hata hapa kwenye jukwaa mijadala ilikuwa ni mikali na mnyukano kati ya CCM na CHADEMA ulikuwa wa wazi.

Uchaguzi wa 2025 nauona ukiwa wa upande mmoja kwa asilimia 95. CHADEMA hawana agenda za kuwaambia wananchi. Wamebaki kuisifu CCM na Rais mama Samia.

Hongera sana Mheshimia Mama Samia. CHADEMA mwendo wameumaliza
Naunga mkono hoja
P
 
Nchi imepiga hatua kubwa sana kimaendeleo. Wananchi bado wana imani na CCM na mama ndiye kaja kuizika kabisa CHADEMA
Umeamua tu kuchekesha watu. Ndo hivi ulikua masomoni uingereza? Ama kweli kusoma na kuelimika ni vitu viwili tofauti kabisa. Nchi kupiga hatua ni chama kukubalika?
Unasifia chama kinachobebwa na uwepo wa Katibu mbovu na yenye kukibeba chama kilichopo madarakani kwa 99.5%? Unasifia vitu vya ajabu sana. Tupateni katiba inayobalansi(mpya) uone jinsi uhalisia utakavyokua.
 
Kuna ACT,cut,nccr nk.... Lkn cdm asbh, mchana, jioni usiku, ukiwa na mumeo, ukiwa chooni....dah cdm raha sana inajitangaza yenyewe 😅
 
Hata kama Chadema itazikwa kama ulivyotabiri ingawa siamini huo utabiri lakini Upinzani Nchini utakuwepo na utaongezeka zaidi kutokana na hali za maisha kuendelea kuwa duni kwa wananchi wengi na wachache kunufaika zaidi na zaidi !!
 
CDM wanatengeneza tukio la mauaji vyombo vyote vya usalama wa Taifa letu wakashindwa kuwabaini wahusika? Bas CDM wana nguvu kuliko taasis ya usalama wa Taifa letu. Na hii ni htr san kama imefikia hatua CDM wanaweza fanya lolote na hakuna wa kushtaki au kuwakamata.
Wadau, amani iwe kwenu.

Katika historia ya upinzani nchini, mwaka 2015 ulikuwa ni uchaguzi ambao ulitushughulisha sana wana CCM. Hata hapa kwenye jukwaa mijadala ilikuwa ni mikali na mnyukano kati ya CCM na CHADEMA ulikuwa wa wazi.

Nakumbuka wakati huo ukianzisha mjadala wa kumshambukia kiongozi wa CCM ama upinzani thread ilikuwa inatembea sana.

Hali ya kisiasa wakati huo ilibebwa na uamuzi wa Lowasa kuhamia CHADEMA. Ni kwa mazingira hayo hata sisi ndani ya CCM tuligawanyika na ndo maana upinzani ulipata nguvu.

Binafsi nilikuwa ni wafia chama hasa wa kambi ya CCM. Nikawa natumia nondo nilizokuwa nazo kumgonga hasa Lowasa. Nilifanikiwa kupata mikakati yake mingi na kuiumbua kabla haijafanikiwa. Aisee nilitisha sana wakati ule.

Baada ya CCM kuibuka ushindi katika uchaguzi ule, binafsi niliona nimeshamaliza kazi na nikaamua kuja hapa Uingereza kujiendeleza kimasomo na kula bata.

Uchaguzi wa 2020 haukuwa na upinzani kabisa isipokuwa CHADEMA walibebwa na tukio la Lissu kupigwa risasi ambalo wao wenyewe ndio walilitengeneza kwa maslahi yao ya kisiasa. Bahati mbaya sana mtaji huo haukuwalipa na CCM tukashinda kwa kimbunga.

Uchaguzi wa 2025 nauona ukiwa wa upande mmoja kwa asilimia 95. Mtaji wa risasi za Lissu haupo tena na CHADEMA hawana agenda za kuwaambia wananchi. Kila wanalofikiria mama keshatangulia kitambo. Si mmewaona juzi kwenye mkutano wao wa hadhara! Wamebaki kuisifi CCM na Rais mama Samia. Kawazidi kete. Kwa sasa watajitutumua kiasi ila kampeni za 2025 mtaona zitakavyododa kwa upande wao.

Hongera sana Mheshimia Mama Samia. CHADEMA mwendo wameumaliza
 
Back
Top Bottom