Rais Samia Suluhu Hassan awaapisha Viongozi mbalimbali walioteuliwa hivi karibuni

Hakuna kitu Wakenya wanaogopa Kama Tanzania...wewe ukikutana na Mkenya anafanya umbeya dhidi ya TZ mwambie wewe nyang'au nyamaza, pumbavu wewe...nakwambia ataondoka Bila kubisha
Ukisikia wapi kwamba wakenya huwa wana muda huo wa 'umbeya'? Hizo ni swag zenu tu nyie wanaume wa kutafuna chipsi mayai.
 
namkubali sana mama. ameanza kwa gia nzuri. kila kitu kiko biΓ©n.
 
Kumbe kweli sio watu wote waloko karibu na wewe basi wanakubaliana na kile ambacho unakifanya, wengine ni kupuuza tu wanapuuza
 
Hongera to Mheshimiwa Suluhu, a very wise woman indeed
 
Yakisimamiwa kwa ufasaha ufanisi utaonekana...
 
KUHUSU KUTUMIA NGUVU NYINGI KULIKO AKILI KWENYE ULIZI WA MADNI
Mirerani tumejenga ukuta, kuta la kwelikweli tukaweka na Majeshi lakini Madini yanatoroshwa kama mwanzo, tukibahatika kuliona linaoneshwa hili hapa, piga picha, bonge la Tanzanite, tunajua mabonge mangapi yamepitishwa chini kwa chini yakatoka?, hatujui”

β€œNdani ya Mirerani kuna vitaru, kitaru C kimewekwa akiba lakini sasa kimeanza kuvamiwa, nataka niseme sitaki kuona mkono wa Mtu kwenye kitalu C, walioanza kugawa vitaru kwenye hilo eneo acheni kina matumizi yake”———Rais Samia



KUHUSU WAWEKEZAJI KUMNYWA

β€œWawekezaji wanalalamika sana kumekuwa na urasimu mkubwa Tanzania, kodi kwa Wawekezaji hazieleweki, napokea taarifa kutoka kwa Wasaidizi wangu, Wafanyabiashara wanataka kuniona niwahakikishie kama watafanya kazi kwa utulivu ili warudi Tanzania”——-Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi wapya Ikulu Dar es salaam leo

β€œWawekezaji wanataka kuja Tanzania lakini kwa mambo yetu wanakimbia, tuvute tena uwekezaji, tupate ajira,fedha izunguke,uchumi ukue, nikiwa Makamu wa Rais kuna Mwekezaji alikuja, sijui alitishwa nini!, nadhani kaambiwa tutakupiga kosa la uhujumi uchumi, akaondoka”———Rais Samia

β€œVibali vya kazi vimekuwa janga, wanaosimamia vibali vya kazi wamejigeuza Miungu Watu , wamegeuza mradi, Mtu anawekeza mnalazimisha aweke Mtanzania, kila Mwekezaji ana haki ya kuweka Mtu anayemuamini yeye kwanini umlazimishe?, mtende haki”———Rais Samia

β€œTunataka Wawekezaji wa-enjoy Tanzania, Makampuni yanafungwa Ndugu zangu sio uongo, tukiweka vikwazo tunawarudisha nyuma, wakiondoka uchumi wetu unashuka, ajira zinapungua na mzunguko wa pesa unapungua na hiki ndio kilio kikubwa cha Watanzania kuwa mifuko mitupu”———Rais Samia
#MillardAyoIkuluUPDATES


CORONA



Tutaunda Kamati ya Wataalamu kuhusu Covid 19 watuambie kitaalamu hayo yanayopendekezwa na Ulimwengu kuja kwetu yapoje, hatuwezi kujitenga tu kama Kisiwa na hatuwezi kupokea yanayoletwa bila kuweka cha kwetu, bila kufanya utafiti wa kwetu”———Rais Samia

β€œRais Kikwete alituambia akili za kuambiwa changanya na zako, tuweke na zetu tuwe na msimamo maalum unaoeleweka, sio tunasoma tu mambo ya Covid 19 Ulimwenguni, Tanzania deshi deshi deshi haieleweki, tueleweke kama tunakubali au tunakataa”———Rais Samia



TRA KUTUMIA VITISHO NA MABAVU KUKUSANYA KODI

β€œTRA agizo langu kwenu ni kuacha matumizi ya ubabe na mabavu kwenye kukusanya kodi haisaidii, mtakwenda mtambinya Mtu, mtamkamua, mtamtisha na kupiga uhujumu uchumi anaogopa kwenda Jela atajikwangua atalipa lakini unaua biashara anafunga, kesho nani anakulipa kodi?”——-Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi wapya Ikulu Dar es salaam leo


UHURU WA KUTOA MAONI BILA HOFU YA KUMNYWA

β€œWizara ya Habari, nasikia kuna Vyombo vya Habari mmevifungia, sijui Viji- TV vya mikononi vile, vifungulieni lakini wafuate sheria na miongozo ya Serikali, tusiwape mdomo wa kusema tunabinya Uhuru wa Vyombo vya Habari, tusifungie tu kibabe”———Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi Wapya leo Ikulu Dar es salaam


MABANDO

β€œKuhusu suala la mabando kulizuka rabsharabsha juzi hapa, Wananchi wakapiga kelele mkalituliza, kalifanyieni kazi lisizuke namna ile mpo mnaangalia hawa Watu wanakuja tu na mambo yao mpaka Wananchi washtuke na nyie ndio mnashtuka, kakaeni nao”———Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi Ikulu Dar es salaam leo

 
Mama yupo vizuri tunamuunga mkono 100%.
 
JPM alinena Kuhusu TRA Tanzania Acheni kodi za dhuluma KWA WANANCHI na Wafanyabiashara wa Nje na ndani, hata Rais wetu Mpendwa Mama Suluhu Samia amenena Lazima msikie bana, anyway Nina imani na mwigulu Nchemba
"Naitazama Tanzania yetu nzuri kwa jicho chanya....Itoshe tu kusema:-
Nawasalimu kwa Jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania-Kazi iendelee

Naa Rais wa awamu ya sita Rais Mama Suluhu Samia"
 
Yamekuwa hayo

Hata the late alikuwa na pambio lake la chini ya tani moja hakuna kusumbuliwa ushuru, ila ukiwauliza wasafirisha mizigo kuhusu utekelezaji wake, ni sifuri.

Nchi inaendeshwa kwa mujibu wa sheria, na Taasisi zote za serikali zinasimamia sheria na si mapambio.
 
πŸ™πŸ™πŸ™
 
Mhe. Rais ameagiza vyombo vya habari vilivyofungiwa wakati wa hayati Dr Magufuli vifunguliwe. Ila wizara iwafungulie na kuhakikisha wanafuata sheria na miongozo ya serikali. 'Vyombo vya habari visifungiwe kibabe'. Lengo ni wasipewe mdomo wa kuwa tunabinya vyombo vya habari. Hivi ni akina nani hao wasipewe mdomo, 'mabeberu' au akina 'shangazi'?

Sheria nyingi za Tanzania ni kandamizi, bila kubadili sheria na miongozo bado vyombo vya habari na uhuru wa maoni itakuwa ni shida tu.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…