Rais Samia Suluhu umenena vyema tuweke tofauti na chuki kando, Je waliopoteza ndugu zao na waliojeruhiwa unawasaidia vipi? Ulipaswa kusema neno

Rais Samia Suluhu umenena vyema tuweke tofauti na chuki kando, Je waliopoteza ndugu zao na waliojeruhiwa unawasaidia vipi? Ulipaswa kusema neno

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Wanabodi ni wazi kabisa pamoja na kuwa tuko kwenye msiba mkubwa kitaifa lakini bado kuna tofauti kubwa na chuki ndani ya jamii yetu.

Ni katika utawala wa awamu ya tano ile ngwe ya kwanza kulitokea sintofahamu ambazo kwa ujumla zilileta kilio na maumivu katika jamii yetu. Maana kuna watu walipotea mpaka leo hatujui wapo wapi.

Zipo maiti ziliokotwa katika fukwe za bahari na mto ruvu. Pia kuna watu wengi ambao ndugu zao wanadai walipoteza maisha wakiwa mikononi mwa vyombo vya dola hususani polisi. Pia tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi lilileta hofu na chuki kubwa.

Leo alipomaliza kuhutubia rais Samia Suluhu ameligusia juu ya kuanza upya na kuacha togauti na chuki zilizopo. Maana mpaka anasema hivyo lazima atakuwa amepewa taarifa kuwa chuki na tofauti zipo

Sasa je, watanzania waliopoteza ndugu zao, waliojeruhiwa , na ambao walipoteza haki zao mpaka kunakuwa na chuki rais wetu mpya anawasaidia vipi? Au ndio imetoka?
 
Mpeni mama Samia muda; akishapata makamu wake ndipo tutakapoanza kuona muelekeo wa serikali yake!! Mungu atunusuru na kuturudisha enzi za Vasco Dagama!!! Vasco Dagama anampigia chepuo mtu wake Nchimbi; mama chonde epukana na kikombe hicho cha makundi ndani ya ccm ama sivyo kazi yako itakuwia ngumu.
 
Mie nilimwelewa pale mwishoni mwa hotuba yake aliposema ataendelea kudumisha na kuboresha utawala bora ili tuwe na umoja wa kitaifa,pia nadhani hakuwa na mood ya kuongea sana.

Ila pia ingekuwa ni kuwakimbiza wale waliotenda maovu kwa wenzao kama angetangaza mapema hivi kwamba atadili nao,nadhani apewe muda.
 
Siyo kila kitu lazima kisemwe
Kusema sema tu hovyo inaitwa kuropoka
Ukiwa kiongozi lazima uzingatie Sana ni Nini useme wapi hiyo ndiyo hekima
 
Mpeni mama Samia muda; akishapata makamu wake ndipo tutakapoanza kuona muelekeo wa serikali yake!! Mungu atunusuru na kuturudisha enzi za Vasco Dagama!!! Vasco Dagama anampigia chepuo mtu wake Nchimbi; mama chonde epukana na kikombe hicho cha makundi ndani ya ccm ama sivyo kazi yako itakuwia ngumu.
Nchimbi na Lukuvi nani ana afadhali?
 
Nchimbi na Lukuvi nani ana afadhali?
Hakuna mwenye afadhali hapo kati ya hao!! Nchi hii ina watu wenye uwezo mkubwa sana wa kuweza kumsaidia mama Samia kazi yake kuwa rahisi ,mmoja wao ni huyo waziri wa usafirishaji. Dr. Chamliho:

Huyu kwanza hana makundi, mtendaji mahiri na msomi pia, muadilifu na sio ambitious kwamba anaweza kumyumbisha boss wake!! NCHIMBI ni nyoka ambae anaweza kumyumbisha mama Samia kwa malengo yake na genge lake ya kisiasa ya muda mfupi na mrefu pia.

Lukuvi hafai kwasababu hana upeo na ni mnafiki sana.
 
Mie nilimwelewa pale mwishoni mwa hotuba yake aliposema ataendelea kudumisha na kuboresha utawala bora ili tuwe na umoja wa kitaifa,pia nadhani hakuwa na mood ya kuongea sana...
Kuna watu hatujui wapo wapi? Wazima au wamekufa?
 
Lukuvi ni mjivuni,jua yote afai,abakie wizara hio hio tu
 
Wasiojulikana ni lzm washughulikiwe hilo lipo wazi,unaanza na Boss wao aliyebaki atawataja wote.Kama walivyofanya Gambia wapo ndani hadi kesho.
 
Mpeni mama Samia muda; akishapata makamu wake ndipo tutakapoanza kuona muelekeo wa serikali yake!! Mungu atunusuru na kuturudisha enzi za Vasco Dagama!!! Vasco Dagama anampigia chepuo mtu wake Nchimbi; mama chonde epukana na kikombe hicho cha makundi ndani ya ccm ama sivyo kazi yako itakuwia ngumu.
Automatically Mama anaenda kuwa TV huku remote ikiwa Msoga. Kundi la kina JK ndiyo mtu wao huyu, nina uhakika tunarudi kwenye enzi za Vasco Dagama kwa namna mpya kabisa.
 
Mlio karibu na mama mkumbusheni bado tunakumbuka ile ahadi aliyotuahidi ya milioni 150 kwa kila kijiji.


JESUS IS LORD.
 
Back
Top Bottom