Rais Samia, The Royal Tour isiache maeneo haya...

Rais Samia, The Royal Tour isiache maeneo haya...

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Amani iwe nawe Mama yangu!

Kwanza napenda kukupongeza kwa hii creativity kubwa uliyokuja nayo ya kushiriki na kuiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia kupitia program maarufu ya “The Royal Tour”

Program hii kwa ufahamu wangu imezinyanyua nchi nyingi sana katika sekta ya Utalii na Uwekezaji Mf. Ni Israël waliyofanya kupitia Waziri Mkuu Mstaafu kipindi Benjamin Netanyahu mwaka 2014, Rwanda kupitia Paul Kagame mwaka 2018 na Jordan ambao walifanya kupitia Mfalme wao.

Kwa miaka mingi sana, Tanzania tumekuwa tukilalamika kuwa tuna rasilimali nyingi, wanyama, mito na mabonde Ila Serikali yetu imekuwa ikilala katika kutumia vitu hivyo na kulinufaisha Taifa.

Kwa upande wa vivutio, Tanzania tuna vivutio vingi na vizuri kuliko nchi za Morroco,Misri, Algeria na South Africa ila hata siku moja hatujawai kufikisha hata Watalii Mil 2 kutembelea nchi yetu. Nchi hizi nilizozitaja kwa mwaka zinapokea Watalii si chini ya Milioni 5.

Swali nililokuwa ninajiuliza siku nyingi ni Je endapo sekta yetu ya utalii ingekuwa inaingiza at least watalii milioni 3 Au 4 tu kwa mwaka , Leo hii Tanzania tungekuwa wapi? Kwa maana pamoja na sekta hii kuongoza katika kuchangia pato la Taifa kwa miaka mingi kabla ya corona, Tanzania hatukuwai kufikisha watalii hata Mil 2 kwa mwaka.

Pamoja na kutoa pongezi zangu kwako Mama Samia kwa hii creativity ambayo hakika nina uhakika wa asilimia 100 itaenda kuipaisha zaidi na zaidi Tanzania , naomba katika ziara yako hii usisahau kuwapitisha watu hawa kwenye maeneo haya

1. Vitalu vya Gesi LIndi na Mtwara ili kuonesha kwa kiasi gani nchi yetu ina huu utajiri wa Gesi. Ikumbukwe, pamoja na changamoto za kiuchumi za dunia, Gesi ni bidhaa adhimu sana

2. Mashamba ya wananchi na Wawekezaji ya Parachichi katika Mikoa ya Njombe na Iringa. Hii ni Kwa sababu sasa hivi duniani Parachichi inafahamika Kama Dhahabu ya Kijani na ndo tunda lenye thamani zaidi kutokana na demand yake huko duniani. Ni wakati sasa Dunia ioneshwe bidhaa hii adhimu inapatikana kwa wingi na ubora unaotakiwa hapa Tanzania ili watu wa Dunia waje kuifuata hapa Tanzania na wananchi wetu waizalishe kwa wingi.

Kwenye hili usisahau pia kuwapitisha kwenye mashamba ya Korosho Kwa sababu korosho pia ni bidhaa iliyokuwa na demand kubwa

3. Madini ya Chuma, Nickel na Dhahabu. Mama Dunia sasa ina uhitaji sana wa haya Madini, ni vizuri kuitangazia dunia kupitia programs hii kuwa yanapatikana kwa wingi hapa Tanzania na Dunia inakaribushwa kuyanunua kupitia masoko maalum tuliyoyaanzisha. Si vibaya wapiga picha wa Royal Tour wakafika kwenye haya Masoko kwenye mikoa kama Mwanza na Geita kuchukua video za masoko husika.

4. Viwanda vya bidhaa mbalimbali za Tanzania ikiwemo maeneo huru ya uwekezaji yaliyotengwa na Tanzania. Naomba pia uwapitishe wapiga picha hawa kwenye haya maeneo, wajionee kwa Jinsi gani tunaza

Mwisho napenda kumalizia kwa kusema, una kwenda vizuri, Mwenyezi Mungu akutangulie kwenye majukumu yako na Tanzania izidi kufaidika zaidi kiuchumi na kimaendeleo
 
Tunapaswa pia kuiandaa sekta yetu ya utalii iwe ijijengee uwezo wa kukabiliana na ongezeko la ujio wa watalii: miundombinu, mahoteli, ufanisi ktk utendaji kazi, nk.
 
Tunapaswa pia kuiandaa sekta yetu ya utalii iwe ijijengee uwezo wa kukabiliana na ongezeko la ujio wa watalii: miundombinu, mahoteli, ufanisi ktk utendaji kazi, nk.
Umesema ya kweli Kabisa. Jitihada hizi za kuitangaza vyema Tanzania ni lazima ziende sambamba na uboreshwaji mkubwa wa miundombinu kama barabara na mahoteli kuelekea kwenye vivutio vyetu na uboreshwaji zaidi wa mazingira ya uwekezaji bila kusahau kubana zaidi mianya ya Wizi na upoteaji wa mapato
 
Hiyo miradi sioni maana ya kuitangaza kama bado hatujui namna bora ya kuisimamia (mapato) ili iwe na tija kwa mwananchi wa kawaida, madini wameyatoa kwa 10% leo tumebakiwa na mashimo tu, hiyo gas nayo nasikia ilishatolewa kwa wachina toka enzi za JK, Magufuli akasema hatuna chetu tena, binafsi naona anachokifanya Rais huko mikoani ni kuuza sura tu na kujipiga selfie.
 
Naomba afike na kule Mbeya, kuna ziwa linaitwa Ngosi, na kule Songwe kwenye kimondo. Ila ziwa nasikia lina masharti ya kufika huko😂
 
Hiyo miradi sioni maana ya kuitangaza kama bado hatujui namna bora ya kuisimamia (mapato) ili iwe na tija kwa mwananchi wa kawaida, madini wameyatoa kwa 10% leo tumebakiwa na mashimo tu, hiyo gas nayo nasikia ilishatolewa kwa wachina toka enzi za JK, Magufuli akasema hatuna chetu tena, binafsi naona anachokifanya Rais huko mikoani ni kuuza sura tu na kujipiga selfie.
Hoja zako zimejaa speculations bila facts na ushahidi
 
Naomba afike na kule Mbeya, kuna ziwa linaitwa Ngosi, na kule Songwe kwenye kimondo. Ila ziwa nasikia lina masharti ya kufika huko😂
Nyanda za Juu kusini akitembelea hifadhi ya Maua na Wanyama Kitulo, Hifadhi ya Ruaha pamoja na Kimondo cha Mbozi itakuwa vizuri sana.

Ila fursa za Kilimo cha Parachichi kwenye mikoa ile ni vizuri zaidi itangazwe maana parachichi kwa sasa ndo zao lililo na faida zaidi Dunia na linahitajika sana!
 
Tunapaswa pia kuiandaa sekta yetu ya utalii iwe ijijengee uwezo wa kukabiliana na ongezeko la ujio wa watalii: miundombinu, mahoteli, ufanisi ktk utendaji kazi, nk.
kweli kabisa unaweza kuta wanajua ila wanaona hamna vitu tunavyojiongeza.

pia na customer care zero kwa hawa watu ndio maana nasikia wakiondoka wana pacent ndogo yakurudi tena kutokana nakukuta mamb ya ajbu sn

pia tujitaidi kutafuta international hospital karb yao pia kuna watali wanaishia nairobi kutokana na afya zao na uwakika wa hospital ya nairobi

nashanga mama leo ameenda mererani kutangaza alafu anaongea na wananchi pale anasema kuna migogoro sn pale bado hawajatatua alafu anataka wawekezaji
sijue umeona wapi shamba lenye migogoro likauzika vizur

mama anatakiwa ahakikishe bidhaa iko vizur kabla haija ingia sokoni kutangazwa
kwani wateja ni watangazaji wazur kama wameridhika na bidhaa
 
Kuna watalii wanaohitaji kutangaziwa kuja kuangalia vitalu vya gesi, mashamba ya mikorosho na maparachichi? Gesi si tayari ina wenyewe wawekezaji swali la kujiuliza wanaendeleza huo uwekezaji kwa kasi gani na kwa nini?
 
Kuna watalii wanaohitaji kutangaziwa kuja kuangalia vitalu vya gesi, mashamba ya mikorosho na maparachichi? Gesi si tayari ina wenyewe wawekezaji swali la kujiuliza wanaendeleza huo uwekezaji kwa kasi gani na kwa nini?
Kwa akili yako ya ushamba unadhani Royal Tour ni utalii tu?

Royal Tour pamoja na kutangaza utalii, inatangaza Pia fursa za kibiashara na uwekezaji Kama ulikuwa hujui mtu uliyejaa chuki na husda dhidi ya Rais Samia
 
kweli kabisa unaweza kuta wanajua ila wanaona hamna vitu tunavyojiongeza.

pia na customer care zero kwa hawa watu ndio maana nasikia wakiondoka wana pacent ndogo yakurudi tena kutokana nakukuta mamb ya ajbu sn

pia tujitaidi kutafuta international hospital karb yao pia kuna watali wanaishia nairobi kutokana na afya zao na uwakika wa hospital ya nairobi

nashanga mama leo ameenda mererani kutangaza alafu anaongea na wananchi pale anasema kuna migogoro sn pale bado hawajatatua alafu anataka wawekezaji
sijue umeona wapi shamba lenye migogoro likauzika vizur

mama anatakiwa ahakikishe bidhaa iko vizur kabla haija ingia sokoni kutangazwa
kwani wateja ni watangazaji wazur kama wameridhika na bidhaa
Eneo la customer care na branding ya biashara kweli ni changamoto kwa Watanzania. Hii ndo sehemu ambayo Wizara ya Viwanda na Biashara ilitakiwa ijikite zaidi katika kuwaelimisha wawekezaji wazawa hapa Tanzania.
 
Eneo la customer care na branding ya biashara kweli ni changamoto kwa Watanzania. Hii ndo sehemu ambayo Wizara ya Viwanda na Biashara ilitakiwa ijikite zaidi katika kuwaelimisha wawekezaji wazawa hapa Tanzania
Kweli kabisa, tunahitaji improvement kubwa na ya haraka sana kwenye customer service, bado tuko nyuma sana.
 
Ingekuwa enzi za Kingwangwala mabango na matangazo yote Royal Tour angeweka picha zake kuanzia airport hadi Katavi na pia angekuwa Dr wa uchumi wa tozo mawe yote ya barabarani yangemkoma, yangeandikwa kama jezi za Makorokoro FC
 
Ruaha National Park
Kitulo Farm
Isimila
Kalenga
Ziwa Mbeya
Daraja la Kiwira
Kimondo cha Mbozi

NYANDA ZA JUU HOYEE...
 
Ingekuwa enzi za Kingwangwala mabango na matangazo yote Royal Tour angeweka picha zake kuanzia airport hadi Katavi na pia angekuwa Dr wa uchumi wa tozo mawe yote ya barabarani yangemkoma, yangeandikwa kama jezi za Makorokoro FC
Dr wa uchumi wa tozo ndo nani huyo?😂😂
 
Kwa akili yako ya ushamba unadhani Royal Tour ni utalii tu?

Royal Tour pamoja na kutangaza utalii, inatangaza Pia fursa za kibiashara na uwekezaji Kama ulikuwa hujui mtu uliyejaa chuki na husda dhidi ya Rais Samia

Nani amchukie kwa sababu gani hasa? Chuki atajitangazia mwenyewe kwa kuongelea vifua vya wanawake wenzake. Au kwa kuuliza maswali ambayo unajua fika utajibiwa kisicho kufurahisha. Rais wa nchi pamoja na vyanzo vyote vya kupewa taarifa unashindwa kujua utajibiwa kitu gani na watu wa Tegeta kuhusu chanjo.

Wanafikiri kupiga picha za sinema na kuonesha Tanzanite inatoka Tanzania ndio kutazuia madini hayo yasitoroshwe, maweee?! Dawa ni kujenga ukuta wa fedha utakao kuwa mrefu kuliko huko zinakotoroshewa wazinunue kwa bei inayozidi huko zinakotoroshewa ziwekwe BOT kwenye hazina ya nchi. Halafu BOT wazidalalie kwenye masoko ya kimataifa. Lakini hilo hawataliweza wanaweza kudhibiti soko la sukari kumuumiza mlaji wa mwisho kwa kutoa vibali vya upendeleo kwa wenye viwanda.
 
Back
Top Bottom