Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 15,819
- 33,255
Amani iwe nawe Mama yangu!
Kwanza napenda kukupongeza kwa hii creativity kubwa uliyokuja nayo ya kushiriki na kuiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia kupitia program maarufu ya “The Royal Tour”
Program hii kwa ufahamu wangu imezinyanyua nchi nyingi sana katika sekta ya Utalii na Uwekezaji Mf. Ni Israël waliyofanya kupitia Waziri Mkuu Mstaafu kipindi Benjamin Netanyahu mwaka 2014, Rwanda kupitia Paul Kagame mwaka 2018 na Jordan ambao walifanya kupitia Mfalme wao.
Kwa miaka mingi sana, Tanzania tumekuwa tukilalamika kuwa tuna rasilimali nyingi, wanyama, mito na mabonde Ila Serikali yetu imekuwa ikilala katika kutumia vitu hivyo na kulinufaisha Taifa.
Kwa upande wa vivutio, Tanzania tuna vivutio vingi na vizuri kuliko nchi za Morroco,Misri, Algeria na South Africa ila hata siku moja hatujawai kufikisha hata Watalii Mil 2 kutembelea nchi yetu. Nchi hizi nilizozitaja kwa mwaka zinapokea Watalii si chini ya Milioni 5.
Swali nililokuwa ninajiuliza siku nyingi ni Je endapo sekta yetu ya utalii ingekuwa inaingiza at least watalii milioni 3 Au 4 tu kwa mwaka , Leo hii Tanzania tungekuwa wapi? Kwa maana pamoja na sekta hii kuongoza katika kuchangia pato la Taifa kwa miaka mingi kabla ya corona, Tanzania hatukuwai kufikisha watalii hata Mil 2 kwa mwaka.
Pamoja na kutoa pongezi zangu kwako Mama Samia kwa hii creativity ambayo hakika nina uhakika wa asilimia 100 itaenda kuipaisha zaidi na zaidi Tanzania , naomba katika ziara yako hii usisahau kuwapitisha watu hawa kwenye maeneo haya
1. Vitalu vya Gesi LIndi na Mtwara ili kuonesha kwa kiasi gani nchi yetu ina huu utajiri wa Gesi. Ikumbukwe, pamoja na changamoto za kiuchumi za dunia, Gesi ni bidhaa adhimu sana
2. Mashamba ya wananchi na Wawekezaji ya Parachichi katika Mikoa ya Njombe na Iringa. Hii ni Kwa sababu sasa hivi duniani Parachichi inafahamika Kama Dhahabu ya Kijani na ndo tunda lenye thamani zaidi kutokana na demand yake huko duniani. Ni wakati sasa Dunia ioneshwe bidhaa hii adhimu inapatikana kwa wingi na ubora unaotakiwa hapa Tanzania ili watu wa Dunia waje kuifuata hapa Tanzania na wananchi wetu waizalishe kwa wingi.
Kwenye hili usisahau pia kuwapitisha kwenye mashamba ya Korosho Kwa sababu korosho pia ni bidhaa iliyokuwa na demand kubwa
3. Madini ya Chuma, Nickel na Dhahabu. Mama Dunia sasa ina uhitaji sana wa haya Madini, ni vizuri kuitangazia dunia kupitia programs hii kuwa yanapatikana kwa wingi hapa Tanzania na Dunia inakaribushwa kuyanunua kupitia masoko maalum tuliyoyaanzisha. Si vibaya wapiga picha wa Royal Tour wakafika kwenye haya Masoko kwenye mikoa kama Mwanza na Geita kuchukua video za masoko husika.
4. Viwanda vya bidhaa mbalimbali za Tanzania ikiwemo maeneo huru ya uwekezaji yaliyotengwa na Tanzania. Naomba pia uwapitishe wapiga picha hawa kwenye haya maeneo, wajionee kwa Jinsi gani tunaza
Mwisho napenda kumalizia kwa kusema, una kwenda vizuri, Mwenyezi Mungu akutangulie kwenye majukumu yako na Tanzania izidi kufaidika zaidi kiuchumi na kimaendeleo
Kwanza napenda kukupongeza kwa hii creativity kubwa uliyokuja nayo ya kushiriki na kuiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia kupitia program maarufu ya “The Royal Tour”
Program hii kwa ufahamu wangu imezinyanyua nchi nyingi sana katika sekta ya Utalii na Uwekezaji Mf. Ni Israël waliyofanya kupitia Waziri Mkuu Mstaafu kipindi Benjamin Netanyahu mwaka 2014, Rwanda kupitia Paul Kagame mwaka 2018 na Jordan ambao walifanya kupitia Mfalme wao.
Kwa miaka mingi sana, Tanzania tumekuwa tukilalamika kuwa tuna rasilimali nyingi, wanyama, mito na mabonde Ila Serikali yetu imekuwa ikilala katika kutumia vitu hivyo na kulinufaisha Taifa.
Kwa upande wa vivutio, Tanzania tuna vivutio vingi na vizuri kuliko nchi za Morroco,Misri, Algeria na South Africa ila hata siku moja hatujawai kufikisha hata Watalii Mil 2 kutembelea nchi yetu. Nchi hizi nilizozitaja kwa mwaka zinapokea Watalii si chini ya Milioni 5.
Swali nililokuwa ninajiuliza siku nyingi ni Je endapo sekta yetu ya utalii ingekuwa inaingiza at least watalii milioni 3 Au 4 tu kwa mwaka , Leo hii Tanzania tungekuwa wapi? Kwa maana pamoja na sekta hii kuongoza katika kuchangia pato la Taifa kwa miaka mingi kabla ya corona, Tanzania hatukuwai kufikisha watalii hata Mil 2 kwa mwaka.
Pamoja na kutoa pongezi zangu kwako Mama Samia kwa hii creativity ambayo hakika nina uhakika wa asilimia 100 itaenda kuipaisha zaidi na zaidi Tanzania , naomba katika ziara yako hii usisahau kuwapitisha watu hawa kwenye maeneo haya
1. Vitalu vya Gesi LIndi na Mtwara ili kuonesha kwa kiasi gani nchi yetu ina huu utajiri wa Gesi. Ikumbukwe, pamoja na changamoto za kiuchumi za dunia, Gesi ni bidhaa adhimu sana
2. Mashamba ya wananchi na Wawekezaji ya Parachichi katika Mikoa ya Njombe na Iringa. Hii ni Kwa sababu sasa hivi duniani Parachichi inafahamika Kama Dhahabu ya Kijani na ndo tunda lenye thamani zaidi kutokana na demand yake huko duniani. Ni wakati sasa Dunia ioneshwe bidhaa hii adhimu inapatikana kwa wingi na ubora unaotakiwa hapa Tanzania ili watu wa Dunia waje kuifuata hapa Tanzania na wananchi wetu waizalishe kwa wingi.
Kwenye hili usisahau pia kuwapitisha kwenye mashamba ya Korosho Kwa sababu korosho pia ni bidhaa iliyokuwa na demand kubwa
3. Madini ya Chuma, Nickel na Dhahabu. Mama Dunia sasa ina uhitaji sana wa haya Madini, ni vizuri kuitangazia dunia kupitia programs hii kuwa yanapatikana kwa wingi hapa Tanzania na Dunia inakaribushwa kuyanunua kupitia masoko maalum tuliyoyaanzisha. Si vibaya wapiga picha wa Royal Tour wakafika kwenye haya Masoko kwenye mikoa kama Mwanza na Geita kuchukua video za masoko husika.
4. Viwanda vya bidhaa mbalimbali za Tanzania ikiwemo maeneo huru ya uwekezaji yaliyotengwa na Tanzania. Naomba pia uwapitishe wapiga picha hawa kwenye haya maeneo, wajionee kwa Jinsi gani tunaza
Mwisho napenda kumalizia kwa kusema, una kwenda vizuri, Mwenyezi Mungu akutangulie kwenye majukumu yako na Tanzania izidi kufaidika zaidi kiuchumi na kimaendeleo