Rais Samia, Umoja wa wanawake wa CCM na Jumuiya ya wazazi mnapata wapi nguvu ya kufumbia macho kauli ya Chalamila?

Rais Samia, Umoja wa wanawake wa CCM na Jumuiya ya wazazi mnapata wapi nguvu ya kufumbia macho kauli ya Chalamila?

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Kwa kweli inashangaza jinsi CCM ilivyogeuka na kuwa chama kisichojali habari za wananchi.

Inashangaza nchi hii ina Rais mwanamke, ina Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) ina jumuia ya wazazi lakini leo hii wote hao wanashindwa kutoa kauli kukemea kauli ya kifedhuli, ya kibaradhuli na ya kibri kikubwa sana ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kwa mama mjamzito anayehitaji kujifungua lakini hana uwezo.

Hebu tujiulize ingekuwa ni uwenyekiti wa Nyerere au CCM ya Nyerere, huyu mkuu wa mkoa wa Dar es salaam angeweza kutoa kauli ya kiburi namna hii.

Chalamila anamwambia mama mjamzito ambaye mi masikini kuwa kama huna hela kamwambie mumeo akupasue yeye mwenyewe kwa mkasi.

Maneno gani hayo!

Inakuwaje kwa Samia ambaye ni mwanamke, tena ni mama, answezaje kufumbia macho kauli kama hii?

Inakuwaje umoja wa eanaeake wa CCM na jumuia ya wazazi inafumbia macho kauli hii?

Tafsiri tunayoipata ni kuwa wote hao wanaunga mkono kauli ya Chalamila. Na ndiyo malipo yao kwa Watanzania.

Sikitiko kubwa lililoje nchini!
 
Albert akeshe na kuomba hili lipite kimya kimya.
Kiongozi mzuri kabisa mwenye future kubwa huko mbele, alitenguliwa mara ya kwanza ukuu wa Mkoa MWANZA kwa sababu ya kauli yake, this time around kauli yake tena imemuweka kitimoto.

Albert ela za jiji la DSM ndio zimechanganya na kumfanya awe na dharau kwa watu wasio na kipato. Kauli hii sio ya kwanza, wala ya pili, kumekuwa na kauli tata toka kinywani mwake mara kwa mara hivi karibuni.

Hadi najiuliza, watu wanaomzunguka hawamwambii unakoelekea kisiasa kutakucost???? Au ndio unafiki wanataka atoke jijini?
 
Kwa kweli inashangaza jinsi CCM ilivyogeuka na kuwa chama kisichojali habari za wananchi.

Inashangaza nchi hii ina Rais mwanamke, ina Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) ina jumuia ya wazazi lakini leo hii wote hao wanashindwa kutoa kauli kukemea kauli ya kifedhuli, ya kibaradhuli na ya kibri kikubwa sana ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kwa mama mjamzito anayehitaji kujifungua lakini hana uwezo.

Hebu tujiulize ingekuwa ni uwenyekiti wa Nyerere au CCM ya Nyerere, huyu mkuu wa mkoa wa Dar es salaam angeweza kutoa kauli ya kiburi namna hii.

Chalamila anamwambia mama mjamzito ambaye mi masikini kuwa kama huna hela kamwambie mumeo akupasue yeye mwenyewe kwa mkasi.

Maneno gani hayo!

Inakuwaje kwa Samia ambaye ni mwanamke, tena ni mama, answezaje kufumbia macho kauli kama hii?

Inakuwaje umoja wa eanaeake wa CCM na jumuia ya wazazi inafumbia macho kauli hii?

Tafsiri tunayoipata ni kuwa wote hao wanaunga mkono kauli ya Chalamila. Na ndiyo malipo yao kwa Watanzania.

Sikitiko kubwa lililoje nchini!
Hiyo kauli angeitoa Makonda ingekuwa hatari sana!
 
Mkuu wa mkoa wa Dar anayedharau wanawake wenye uchungu wa uzazi, wasio na hela ya kuwawezesha kupata huduma za uzazi salama.
 
Hao umoja wa wanawake ndani ya CCM ndio waliomshikia bango Paul Makonda mpaka kumpeleka kamati ya maadili kisa tu kumwambia yule dada kwamba ana mke mzuri kuliko yeye ajabu kauli ya Chalamila wanaiona Iko sawa.

Bongo bila kuwa mnaofikir Maisha hayaendi.
 
Lakini tuna Rais wa ajabu sana, kiongozi uliyemteua anatukana hadharani uko kimya inakaribia wiki sasa..halafu ni juzi tu umependekezwa kuwa mgombea wa urais 2025..hivi mgombea ndio anabehave hivi kwa wapiga kura..? Hivi wazanzibar na waislamu ndio wako na kiburi namna hii? It's peculiar..!
 
Kama WASIRA anateuliwa kuongoza chama na vijana wanashangilia undhani Kuna mwenye akili timamu kwenye hicho chama???
 
Back
Top Bottom