Rais Samia unapozungumza na wanafunzi wa elimu ya juu usisahau fedha za mafunzo kwa vitendo (field)

Momazi

Member
Joined
Jan 5, 2023
Posts
48
Reaction score
54
Rais Samia mama yetu tunatambua nia yako njema ni kuiona Tanzania ikisonga mbele na kuondoa manung'uniko mengi.

Mama wewe ni mfariji mkuu tunaomba unapokuwa unazungumza na wanafunzi wa vyuo hapo Dodoma uliangalie suala gumu ambalo tulikabiliana nalo mwaka jana tulipokuwa katika mafunzo kwa vitendo (field).

Hali ilikuwa mbaya kwani hatukuwa na hela ya field, hivyo tunaomba huruma yako tuangaliwe kwa jicho la pili maana unakuta shule nyingi hazitoi full acomodation.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…