Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Rais Samia amewahasa wananchi wa Korogwe na Tanga kwa ujumla kwenda kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura, mchakato ambao unasimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi ukiwa unaendelea kwa sasa huko mkoani Tanga.
Rais Samia alisema:
"Niwakumbushe kile kijambo chetu cha mwezi wa 10 mwaka huu, kama jina lako haliko kwenye daftari la wapiga kura hutaweza kupata ile haki. Sasa kama unafurahia miradi na maendeleo inayoletwa Korogwe hakikisha unaenda kujiandikisha kwenye daftari na siku ikifika umetoka unaaenda kupiga kura
"Kwa hiyo tume itazunguka kurekebisha taarifa na kuchukua majina mapya ya wapiga kura. Mtoke mkajiandikishe wananchi kila mwenye sifa, kajiandikisheni ili mpate sifa na mpate haki ya kupiga kura"
Rais Samia amewahasa wananchi wa Korogwe na Tanga kwa ujumla kwenda kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura, mchakato ambao unasimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi ukiwa unaendelea kwa sasa huko mkoani Tanga.
Rais Samia alisema:
"Niwakumbushe kile kijambo chetu cha mwezi wa 10 mwaka huu, kama jina lako haliko kwenye daftari la wapiga kura hutaweza kupata ile haki. Sasa kama unafurahia miradi na maendeleo inayoletwa Korogwe hakikisha unaenda kujiandikisha kwenye daftari na siku ikifika umetoka unaaenda kupiga kura
"Kwa hiyo tume itazunguka kurekebisha taarifa na kuchukua majina mapya ya wapiga kura. Mtoke mkajiandikishe wananchi kila mwenye sifa, kajiandikisheni ili mpate sifa na mpate haki ya kupiga kura"