Rais Samia: Wanaofanya biashara wakiulizwa kuhusu kodi wanasema kuna maelekezo kutoka "juu". Sijawahi kutoa maelekezo mtu asilipe kodi!

Rais Samia: Wanaofanya biashara wakiulizwa kuhusu kodi wanasema kuna maelekezo kutoka "juu". Sijawahi kutoa maelekezo mtu asilipe kodi!

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Leo akiwa anazungumza, Rais Samia amesema kuwa kuna wale wafanyabiashara ambao wakitakiwa kutoa kodi wanasema kuna maelekezo kutoka juu.

Rais Samia amesema kuwa kwa Tanzania, uongozi wa juu kwenye serikali ya Tanzania ni nafasi ya Rais na kwa kuwa yeye ndio Rais amesema wazi kuwa hajawahi kuagiza mtu yeyote asilipe kodi

 
Ibada ya kujitakasa kwa muda.

Then mambo yakisha tiki, Business as usual.
 
Kuna mfanyabiashara kabisa anaweza kuyasema hayo bila kuiogopa taasisi?
 
Mh. alipaswa kujua aliyejuu yake na anayetoa hayo maelekezo ili tukomeshe hizi tabia za kuhujumu uchumi
 
Hii mbinu Huwa inatumika maeneo mengi sana sio tuu Kwa wakwepa.kodi Bali Hadi Kwa Polisi wanaotaka Kukamata Baadhi ya watu au kuzuia jambo Fulani.

Sasa Leo Mkuu wa Nchi amekataa kutoa kibali Cha maelekezo kutoka Juu kwamba ni janja janja ya watu wachache kukwepa kuwajibika.

Swali:

Je Wananchi waanze kukaidi Kauli za maelekezo kutoka Juu?

======
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameelezea kukerwa na matumizi ya kauli ya “maelekezo kutoka juu” kama kisingizio cha kukwepa kodi na kufafanua kuwa hajawahi kutoa maagizo kama hayo.

Akizungumza Alhamisi, Januari 23, 2025, katika hafla ya utoaji wa tuzo kwa walipa kodi bora wa mwaka 2023/2024, iliyofanyika katika Ukumbi wa The Super Dome, Masaki, jijini Dar es Salaam, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kila mfanyabiashara kulipa kodi bila upendeleo.

“Mimi sijawahi kutoa maelekezo mtu asilipe kodi, na ikitokea haja ya kufanya hivyo, shirika au mtu asilipe kodi, nitafanya kwa maandishi na sio mtu aje kwa mdomo. Maelekezo kutoka juu, mimi sijawahi kufanya hivyo,” amesema Rais Samia, akihimiza uwajibikaji wa kodi.

Aidha, Rais Samia ameeleza kuwa ukwepaji kodi unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara unaondoa usawa katika biashara na kuwaumiza wale wanaofuata sheria kwa kulipa kodi.

Rais ametoa wito kwa watendaji wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha usimamizi wa haki katika ulipaji kodi na kuhakikisha kila mfanyabiashara anachangia maendeleo ya taifa kwa kufuata taratibu zilizopo
Screenshot 2025-01-24 105306.png
 
Hii mbinu Huwa inatumika maeneo mengi sana sio tuu Kwa wakwepa.kodi Bali Hadi Kwa Polisi wanaotaka Kukamata Baadhi ya watu au kuzuia jambo Fulani.

Sasa Leo Mkuu wa Nchi amekataa kutoa kibali Cha maelekezo kutoka Juu kwamba ni janja janja ya watu wachache kukwepa kuwajibika.

Swali:

Je Wananchi waanze kukaidi Kauli za maelekezo kutoka Juu?

======
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameelezea kukerwa na matumizi ya kauli ya “maelekezo kutoka juu” kama kisingizio cha kukwepa kodi na kufafanua kuwa hajawahi kutoa maagizo kama hayo.

Akizungumza Alhamisi, Januari 23, 2025, katika hafla ya utoaji wa tuzo kwa walipa kodi bora wa mwaka 2023/2024, iliyofanyika katika Ukumbi wa The Super Dome, Masaki, jijini Dar es Salaam, Rais Samia amesisitiza umuhimu wa kila mfanyabiashara kulipa kodi bila upendeleo.

“Mimi sijawahi kutoa maelekezo mtu asilipe kodi, na ikitokea haja ya kufanya hivyo, shirika au mtu asilipe kodi, nitafanya kwa maandishi na sio mtu aje kwa mdomo. Maelekezo kutoka juu, mimi sijawahi kufanya hivyo,” amesema Rais Samia, akihimiza uwajibikaji wa kodi.

Aidha, Rais Samia ameeleza kuwa ukwepaji kodi unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara unaondoa usawa katika biashara na kuwaumiza wale wanaofuata sheria kwa kulipa kodi.

Rais ametoa wito kwa watendaji wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha usimamizi wa haki katika ulipaji kodi na kuhakikisha kila mfanyabiashara anachangia maendeleo ya taifa kwa kufuata taratibu zilizopo
View attachment 3212279
Bora maana inatumika na wahuni wengi kuumiza watu
 
Wakuu,

Leo akiwa anazungumza, Rais Samia amesema kuwa kuna wale wafanyabiashara ambao wakitakiwa kutoa kodi wanasema kuna maelekezo kutoka juu.

Rais Samia amesema kuwa kwa Tanzania, uongozi wa juu kwenye serikali ya Tanzania ni nafasi ya Rais na kwa kuwa yeye ndio Rais amesema wazi kuwa hajawahi kuagiza mtu yeyote asilipe kodi

Magu alijitahidi kwenye hili watu wakambeza, hatutaki Kodi za mabavu, sasa hivi MTU huyo huyo anasema watu walipe kodi, yaani mpaka machinga. Na Magu alianza na vitambulisho vya machinga 20,000 kwa Mwaka , sasa hivi wangekuwa wameisha ingia kwenye mfumo.
 
Umeletewa demand notice kwenye karatasi unaijibuje kuwa silipi kwa maelekezo kutoka juu? Migogoro wa kikodi wa "Raisi alisema" upo zaidi kwenye lile suala la kodi ya miaka mi5 nyuma. Raisi aweke clear kama inawezekana.
 
Back
Top Bottom