Rais Samia, zile pesa ulizoziita za dhulma walizopokwa wafanya biashara na TRA itapendeza kama mtawarudishia wenyewe

Rais Samia, zile pesa ulizoziita za dhulma walizopokwa wafanya biashara na TRA itapendeza kama mtawarudishia wenyewe

gimmy's

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2011
Posts
3,312
Reaction score
3,345
Nawasalimu kwa jina la jamuhuri ya muungano wanajukwaa.

Ndugu zangu kwanza nitaanza kwa ku declear interest kwamba mimi ni mwana CCM ambae nilikuwa simuungi na sikubaliani na hayati Magufuli bila kificho kwani matendendo yake na uongozi wake haukuwa mzuri kwa maono yangu.

Kwa maono yangu awamu ya tano iliendesha nchi kimabavu pasipo kufuata utawala wa sheria sambamba na ukiukwaji wa haki za raia,uhuru wa habari uliminywa,uminywaji wa demokrasia na ukandamizwaji wa vyama vya siasa,ikiwemo na uvurugwaji wa uchumi wa raia.

Juzi mh raisi wetu mama Samia amesikika alipokuwa anaongea na wazee wa Dar es Salaam akisema amedhamiria kutatua kero zilizokuwepo na moja ya kero alizozitaja ni kukomesha pesa walizokuwa wanapokwa wafanya biashara na TRA kupitia kitengo maarufu kama task force.

Mh raisi samia si mara ya kwanza kulizungumza hili la TRA kwani nakumbuka hata siku ya kuapisha baraza lake la mawaziri alilizunguza kwa msisitizo kwamba mwenendo wa TRA si mzuri kwani imepokonya pesa wafanyabiashara kwakuwatishia kuwafungulia kesi za uhujumu uchumi.

Binafsi nimpongeze sana mh raisi kwa kuliona hili,lakini kwanini kusiundwe tume ifuatilie wale wote waliodhulumiwa pesa zao wakarudishiwa?

Mh raisi kuna wafanya biashara wengi wamekufa kwa pressure baada ya kufilisiwa na TRA,serikali ingerudisha pesa kwa wajane na watoto wa marehemu.Wapo wajane leo wameachiwa watoto na leo wanashindwa hata kulipa ada kwasababu ya dhulma za TRA.

Mh Rais kukiri kwamba kuna dhulma imetendeka halafu kusichukuliwe hatua zakuirudisha hii pesa ya dhulma kwa walengwa sio sawa.

Yote kwa yote tunafarijika sana kupata raisi mwenye hekima na busara,mh raisi hawa wachunga ng'ombe wachache wanaompinga humu mitandaoni ni vema akawapuuza.

Mungu na ambariki Rais wetu asiwe na kiburi,tambo na majigambo kwani kwa yaliyopita tumejifunza mengi.

Asante.
 
Imetoka hiyo ikirudi panchaaaa

Ova
 
Naunga mkono hoja.Kwa mfano wale wafanyabiashara wa kubadilisha dola..
 
Hivi mnajua wafanya biashara wengi hawalipi kodi? hivi unajua 90% ya wafanya biashara kariakoo hawalipi kodi? hivi unajua 97% ya biashara za wa Tanzania wenye asili ya kihindi hawalipi kodi? hivi unajua 100% ya biashara za mabasi hawalipi kodi bado wanatumia daftari kukatisha ticket? Rais Samia bado hawajui wafanya biashara wa Tz labda kama anataka kuendesha serikali kwa njia ya kuomba omba, msitetee kitu ambacho hamkijui, nimeajiliwa miaka 11 na nikaacha, niko na kampuni yangu nafanya biashara najua michezo ya wafanya biashara, Tanzania hii sio ya kukusanya tri2 kwa Mwezi kama hao wafanya biashara unao watetea watalipa kodi.
 
Hivi mnajua wafanya biashara wengi hawalipi kodi? hivi unajua 90% ya wafanya biashara kariakoo hawalipi kodi? hivi unajua 97% ya biashara za wa Tanzania wenye asili ya kihindi hawalipi kodi? hivi unajua 100% ya biashara za mabasi hawalipi kodi bado wanatumia daftari kukatisha ticket? Rais Samia bado hawajui wafanya biashara wa Tz labda kama anataka kuendesha serikali kwa njia ya kuomba omba, msitetee kitu ambacho hamkijui, nimeajiliwa miaka 11 na nikaacha, niko na kampuni yangu nafanya biashara najua michezo ya wafanya biashara, Tanzania hii sio ya kukusanya tri2 kwa Mwezi kama hao wafanya biashara unao watetea watalipa kodi.
Mmmh, hizo takwimu umezitoa wapi ndugu?
 
Hivi mnajua wafanya biashara wengi hawalipi kodi? hivi unajua 90% ya wafanya biashara kariakoo hawalipi kodi? hivi unajua 97% ya biashara za wa Tanzania wenye asili ya kihindi hawalipi kodi? hivi unajua 100% ya biashara za mabasi hawalipi kodi bado wanatumia daftari kukatisha ticket? Rais Samia bado hawajui wafanya biashara wa Tz labda kama anataka kuendesha serikali kwa njia ya kuomba omba, msitetee kitu ambacho hamkijui, nimeajiliwa miaka 11 na nikaacha, niko na kampuni yangu nafanya biashara najua michezo ya wafanya biashara, Tanzania hii sio ya kukusanya tri2 kwa Mwezi kama hao wafanya biashara unao watetea watalipa kodi.
Ungekua unajua utitiri wa kodi kwenye biashara za Tanzania usingeandika haya
Unasema watu wa mabasi hawalipi kodi kwa kuwa tu wanatumia kitabu, lakini kuna kodi kibao wanalipa , we umeangalia kodi moja tu.

Punguzeni utitiri wa kodi , mtaona good response
N.b kama hujawahi kuuza hata genge huwezi nielewa
 
Mmmh, hizo takwimu umezitoa wapi ndugu?
Ingia kwenye biashara ufe na cheko, nyie mna tetea kitu ambacho hamkijui, wahindi wanafanya biashara without proper documentations, tena anakuambia with or what without VAT? ukisema with VAT ana kimbia
 
Hivi mnajua wafanya biashara wengi hawalipi kodi? hivi unajua 90% ya wafanya biashara kariakoo hawalipi kodi? hivi unajua 97% ya biashara za wa Tanzania wenye asili ya kihindi hawalipi kodi? hivi unajua 100% ya biashara za mabasi hawalipi kodi bado wanatumia daftari kukatisha ticket? Rais Samia bado hawajui wafanya biashara wa Tz labda kama anataka kuendesha serikali kwa njia ya kuomba omba, msitetee kitu ambacho hamkijui, nimeajiliwa miaka 11 na nikaacha, niko na kampuni yangu nafanya biashara najua michezo ya wafanya biashara, Tanzania hii sio ya kukusanya tri2 kwa Mwezi kama hao wafanya biashara unao watetea watalipa kodi.
Mabasi hayalipi kabisa kodi hizi takwemu mnaytoaga wapi nyi waongo
 
Back
Top Bottom