kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Mji wa Dar es Salaam ulikuwa ni sehemu tu ya mkoa wa Pwani, kutokana na idadi yake kubwa ya watu wanasiasa waliamua ujitenge ili uwe mkoa unaojitegemea. Ilala, Kinondoni, Temeke na Ubungo ilikuwa ni mitaa tu ya mji wa Dar es salaam ambayo baadae wanasiasa waliigeuza kuwa wilaya/halmashauri ili kusogeza karibu huduma kwa wananchi.
Ilala, Kinondoni na Ubungo ni mitaa/wilaya ambazo zimeshikana zinazounda jiji la Dar es Salaam, hivyo wanashirikiana kwenye mambo mengi sana ikiwemo stend kuu, mabenki, shule, nk. Hivyo kuifanya Ilala pekee kuwa jiji na nyingine kubaki kuwa halmashauri ni sawa lakini kutaleta mtafaruku wa kiutendaji muda sio mrefu ambao unaweza kusababisha Rais ajae baada ya muda wako kwisha akaamua vinginevyo tena.
Maswali tunayojiuliza wananchi ni je:
1. Mamlaka ya jiji la Ilala hayatafika kwenye halmashauri nyingine?
2. Je, Ilala, Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kinondoni zina vyanzo sawa vya mapato ya kujiendesha? Au zitagawanaje mapato?
3. Itakuwaje kama siku moja Ubungo, Temeke, Kinondoni, na Kigamboni pia zikipata hadhi ya kuwa majiji? Tutakuwa na majiji 4 yaliyoko karibu?
4. Je, jina la Dar es Salaam litatumika tukimaanisha sehemu gani kati ya hizi halmashauri?
Kwa maoni yangu mimi, kwakuwa Dar es Salaam imeungana kuanzia Kigamboni, Ilala, Ubungo na Temeke ni rahisi sana kuzivunja halmashauri zote zilizopo sasa na kulibakisha jiji la Dar es Salaam likiwa moja tu Dar es Salaam tu na kata zake ili kupunguza mzigo wa matumizi ya kuwa na wakuu wa Wilaya, wakurugenzi wa Wilaya, na watendaji wengine kwenye halmashuri which are more cost kuliko matumizi ya jiji bila halmashauri.
Kuvunja halmashauri zote na kubakisha jiji kunaokoa pesa nyingi zaidi kuliko kuvunja jiji na kubakisha Ilala kama jiji na halmashauri za Temeke, Ubungo, Kinondoni na kigamboni.
Kama hoja ni kubana matumizi ya uendeshaji wa Dar es Salaam basi tuvunje halmashauri zote ibaki moja tu ya jiji la Dar es Salaam na madiwani wa kuchaguliwa kwenye kata za Dar es Salaam.
Ilala, Kinondoni na Ubungo ni mitaa/wilaya ambazo zimeshikana zinazounda jiji la Dar es Salaam, hivyo wanashirikiana kwenye mambo mengi sana ikiwemo stend kuu, mabenki, shule, nk. Hivyo kuifanya Ilala pekee kuwa jiji na nyingine kubaki kuwa halmashauri ni sawa lakini kutaleta mtafaruku wa kiutendaji muda sio mrefu ambao unaweza kusababisha Rais ajae baada ya muda wako kwisha akaamua vinginevyo tena.
Maswali tunayojiuliza wananchi ni je:
1. Mamlaka ya jiji la Ilala hayatafika kwenye halmashauri nyingine?
2. Je, Ilala, Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kinondoni zina vyanzo sawa vya mapato ya kujiendesha? Au zitagawanaje mapato?
3. Itakuwaje kama siku moja Ubungo, Temeke, Kinondoni, na Kigamboni pia zikipata hadhi ya kuwa majiji? Tutakuwa na majiji 4 yaliyoko karibu?
4. Je, jina la Dar es Salaam litatumika tukimaanisha sehemu gani kati ya hizi halmashauri?
Kwa maoni yangu mimi, kwakuwa Dar es Salaam imeungana kuanzia Kigamboni, Ilala, Ubungo na Temeke ni rahisi sana kuzivunja halmashauri zote zilizopo sasa na kulibakisha jiji la Dar es Salaam likiwa moja tu Dar es Salaam tu na kata zake ili kupunguza mzigo wa matumizi ya kuwa na wakuu wa Wilaya, wakurugenzi wa Wilaya, na watendaji wengine kwenye halmashuri which are more cost kuliko matumizi ya jiji bila halmashauri.
Kuvunja halmashauri zote na kubakisha jiji kunaokoa pesa nyingi zaidi kuliko kuvunja jiji na kubakisha Ilala kama jiji na halmashauri za Temeke, Ubungo, Kinondoni na kigamboni.
Kama hoja ni kubana matumizi ya uendeshaji wa Dar es Salaam basi tuvunje halmashauri zote ibaki moja tu ya jiji la Dar es Salaam na madiwani wa kuchaguliwa kwenye kata za Dar es Salaam.