Itakuwa chaguo lake alikosa, halafu hii inakufanya uhonge watu wachache zaidi ili kumpata mlengwa wako, maana wakiwa ni madiwani wote gharama zinakuwa kubwa halafu utakuwa unabahatisha.Hii anafanya kwa kumuondoa mayor wa sasa wa jiji la dar es salaam
kwa Kua Hana uwezo wa kumtumbua imebidi ageuze mchezo, sijui kamkosea nini Yule kijana
Hata mimi nilijua ni siasa zao za kijambazi tuView attachment 1711695
Hamtaki huyu omary ndio hizo vigisu zote na kumtumbua hawezi, inabidi ageuze mchezo jiwe bwana sometimes Ana Chuki za ajabu sana , sijui ni binadamu wa aina gani Yule
Si hiyo wilaya ya Ilala ndiyo inayobeba jiji la Dar es Salaam. Wilaya zingine zote ni manispaa.wilaya ya dodoma ni jiji, wilaya za kongwa na chamwino sio majiji, wilaya ya mbeya ni jiji, wilaya za rungwe na kyela sio majiji, wilaya ya Tanga ni jiji, wilaya za lushoto na koogwe sio majiji, ombeni mpate wilaya ya Daslamu kwanza kabla ya kulia lia. Wa Mwanza mjiandae, mnafuatia nyinyi.
Kwani jiji la mwanza kuna wilaya/mji unaitwa mwanza ?Mkoa wa Tanga kuna mji unaitwa Tanga ambao ndiyo jiji la tanga, Mkoa wa Dodoma kuna mji unaitwa Dodoma ambao ndiyo jiji la Dodoma, je mbona Mkoa wa Dar es Salam jiji lake linaitwa Ilala?
Shida unayopata tu ni kwamba kiswahili kina ishia neno Jiji lakini tukipata kiswahili cha Metropolitan basi ndio Dar es SalaamMji wa Dar es Salaam ulikuwa ni sehemu tu ya mkoa wa Pwani, kutokana na idadi yake kubwa ya watu wanasiasa waliamua ujitenge ili uwe mkoa unaojitegemea. Ilala, Kinondoni, Temeke na Ubungo ilikuwa ni mitaa tu ya mji wa Dar es salaam ambayo baadae wanasiasa waliigeuza kuwa wilaya/halmashauri ili kusogeza karibu huduma kwa wananchi.
Ilala, Kinondoni na Ubungo ni mitaa/wilaya ambazo zimeshikana zinazounda jiji la Dar es Salaam, hivyo wanashirikiana kwenye mambo mengi sana ikiwemo stend kuu, mabenki, shule, nk. Hivyo kuifanya Ilala pekee kuwa jiji na nyingine kubaki kuwa halmashauri ni sawa lakini kutaleta mtafaruku wa kiutendaji muda sio mrefu ambao unaweza kusababisha Rais ajae baada ya muda wako kwisha akaamua vinginevyo tena.
Maswali tunayojiuliza wananchi ni je:
1. Mamlaka ya jiji la Ilala hayatafika kwenye halmashauri nyingine?
2. Je, Ilala, Kinondoni, Temeke, Ubungo na Kinondoni zina vyanzo sawa vya mapato ya kujiendesha? Au zitagawanaje mapato?
3. Itakuwaje kama siku moja Ubungo, Temeke, Kinondoni, na Kigamboni pia zikipata hadhi ya kuwa majiji? Tutakuwa na majiji 4 yaliyoko karibu?
4. Je, jina la Dar es Salaam litatumika tukimaanisha sehemu gani kati ya hizi halmashauri?
Kwa maoni yangu mimi, kwakuwa Dar es Salaam imeungana kuanzia Kigamboni, Ilala, Ubungo na Temeke ni rahisi sana kuzivunja halmashauri zote zilizopo sasa na kulibakisha jiji la Dar es Salaam likiwa moja tu Dar es Salaam tu na kata zake ili kupunguza mzigo wa matumizi ya kuwa na wakuu wa Wilaya, wakurugenzi wa Wilaya, na watendaji wengine kwenye halmashuri which are more cost kuliko matumizi ya jiji bila halmashauri.
Kuvunja halmashauri zote na kubakisha jiji kunaokoa pesa nyingi zaidi kuliko kuvunja jiji na kubakisha Ilala kama jiji na halmashauri za Temeke, Ubungo, Kinondoni na kigamboni.
Kama hoja ni kubana matumizi ya uendeshaji wa Dar es Salaam basi tuvunje halmashauri zote ibaki moja tu ya jiji la Dar es Salaam na madiwani wa kuchaguliwa kwenye kata za Dar es Salaam.
Mkoa wa dsm ulipaswa kuwa unajumlisha wilaya za dsm mjini, kibaha, mkuranga, kisarawe, bagamoyo. Hivyo wilaya ya dsm ndiyo ingetakiwa iwe jiji. Lakini kusema Masaki, Mbezi Beach, Kawe, Ununio, Bunju, Chuo kikuu cha Mlimani, Mlimani City Mall na Lugalo haviko jijini ni kukaribisha mashaka yanayohitaji kufanyiwa kazi siku za usoni na watu wengine.Dar es salaam ni mkoa kamili kiutawala, kwani RC Kunenge anatawala mkoa upi?
Huo mfano sio sahihi kidogo. Dar salaam ni tofauti na hiyo mikoa mingine unayoitaja. Mbeya, chunya, tukuyu, mbalali haukua mji mmoja kama ilivyo Ilala, temeke, ubungo, kinondoni. Hivyo huwezi kuita wilaya za dodoma, mpwapwa, kondoa, bahi sijui na wapi jiji la dodoma. Maana geografically ziko mbali sana. Hii ni tofauti na dar es salaam ambayo ilala, ubungo, temeke, kinondoni ambayo ilikuwa mitaa tu ndani ya mji mmoja.Hujui complications za ki-administration na ubebaji wajibu,muingiliano wa kiutendaji na utupianaji Moira ulokuwepo maana we haupo kwenye ngazi ya utawala
Hoja ya dsm imeungana jua tuu tz bars yote imeungana! Kuna watu wamekuwa wakipigania vyeo kwajili ya ulaji kiujanja janja wamestopishwa
Mbona mikoa mingine mambo nihivyo na uongozi umekuwa rahisi? Makao makuu yamkoa ndiyo yanapewa ujiji sio mkoa mzima MF Dodoma jiji pale center lkn huko mf Kondoa kuna ujiji gani?? Mwanza jiji ukerewe kunaujiji gani?? Ilikuwa in janjajanja tuu zakutafuta mavyeo bilakazi