Rais Uhuru Kenyatta akutana na Rais wa Baraza la Ulaya

Rais Uhuru Kenyatta akutana na Rais wa Baraza la Ulaya

Ikaria

Member
Joined
Jul 17, 2019
Posts
93
Reaction score
238
Rais Uhuru Kenyatta leo tarehe 9 Machi, 2021 amefanya kikao na Rais wa Baraza la Ulaya Charles Michel katika Ikulu ya Nairobi.

Viongozi hao wamejadili masuala pana yanayohusu uhusiano wa Kenya na Umoja wa Ulaya yakiwemo:

• Kukuza uhusiano wa sekta binafsi ya Kenya na Umoja wa Ulaya ili kubuni nafasi za ajira.

• Kujenga ushirikiano wa Kenya na EU kwenye masuala yanayohusu kanda ya Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.

• Kushirikiana katika kufufua uchumi wa Kenya na EU hasa katika kipindi hiki cha Covid19.

Rais Charles Michel alikuwa ameandamana na Simon Mordue, Balozi wa EU nchini Kenya.

Aidha pia katika kikao hicho walikuwepo Raychelle Omamo, ambaye ni Waziri wa mambo ya nje wa Kenya pamoja na Adan Mohamed, Waziri wa utangamano wa Afrika Mashariki.

Kenyatta.jpg
 
Hivi wa kwetu yuko wapi ?au anapalilia mbaazi nini? Hapo utashangaa anakuja na povu la mabeberu

Haya tulisha yafanya sana enzi za jk. Wee hukumbuki kuna siku tuliwakusanya marais (wa marekani) wawili wastaafu na mmoja alikuwa madarakani. Tukawaleta Ubungo wakacheza na mpira. Tena baada ya wiki moja akaja rais wa china. Yaani mambo yalikuwa bam bam. Sasa tumeona ngoja tujaribu kitu tofauti.
 
Haya tulisha yafanya sana enzi za jk. Wee hukumbuki kuna siku tuliwakusanya marais (wa marekani) wawili wastaafu na mmoja alikuwa madarakani. Tukawaleta Ubungo wakacheza na mpira. Tena baada ya wiki moja akaja rais wa china. Yaani mambo yalikuwa bam bam. Sasa tumeona ngoja tujaribu kitu tofauti.
kipindi hicho alikuwa bado analima mbaazi kwao kijijini.hana habari huyu.
 
Haya tulisha yafanya sana enzi za jk. Wee hukumbuki kuna siku tuliwakusanya marais (wa marekani) wawili wastaafu na mmoja alikuwa madarakani. Tukawaleta Ubungo wakacheza na mpira. Tena baada ya wiki moja akaja rais wa china. Yaani mambo yalikuwa bam bam. Sasa tumeona ngoja tujaribu kitu tofauti.
sema tu ukweli ndugu... kwa sasa mumedorora mbaya sana mpaka munaonekana vichaa/ wendawazimu kwenye uso wa dunia. mbali na hivo pia, mkulu na kutema yai, ni kama maji na mafuta
 
Mwingine akutana na malaika israel
 
Back
Top Bottom