Rais Uhuru Kenyatta amsamehe Diwani aliyemwambia 'aache kuvuta bangi'

Rais Uhuru Kenyatta amsamehe Diwani aliyemwambia 'aache kuvuta bangi'

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
1470382711671.jpg
Rais Uhuru Kenyatta amemsamehe diwani kutoka Kisii ambaye alimtusi kwa kumwambia aache kuvuta bangi.

Mnamo Agosti 28'2013 akiwahutubia wakazi wa Kerera, diwani wa Kiogoro Samuel Aboko Onkwani alinukuliwa akisema, "wale wako karibu na Rais Uhuru Kenyatta wanapaswa kumshauri aache kuvuta bangi."

Matamshi ya Bw Onkwani yalimfanya ashtakiwe kwa kudhalilisha mamlaka ya afisa wa umma kinyume na kipengele cha Penal Code.

Alhamisi katika mkutano na madiwani wa Kisii na Nyamira, Rais Kenyatta alitangaza msamaha kwa diwani huyo na kumwambia asahau yaliyopita. "Sahau yaliyopita na turidhiane"Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Kidigitali katika Ikulu Denis Itumbi alimnukuu Rais Kenyatta.

Bw Onkwani ambaye alikuwa miongoni mwa madiwani wa Kisii na Nyamira waliomtembelea Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi alionekana akisalimiana na kupeana pambaja na Rais Kenyatta kama ishara ya msamaha.

Kesi dhidi ya diwani huyo ilikuwa bado inaendelea kortini japo kupitia mawakili Gideon Nyambati na Isaiah Mosota, diwani huyo alikuwa amekanusha mashtaka hayo.

Madiwani 58 kutoka Kaunti ya Kisii na wenzao 29 kutoka kaunti ya Nyamira walikutana na Rais Kenyatta na Naibu Rais William Ruto kupanga ziara ya Rais maeneo hayo na kujadiliana kuhusu miradi ya maendeleo atakayozindua.
 
Hahahaha aiseee huo ndio ubinadamu sio kila kitu kutumia nguvu kubwa kwa sababu tu una nguvu hiyo ila huyo jamaa lazima anakula sana majani


Pambaja ni kitu gani ??
 
Hahahaha aiseee huo ndio ubinadamu sio kila kitu kutumia nguvu kubwa kwa sababu tu una nguvu hiyo ila huyo jamaa lazima anakula sana majani
Mkuu huogopi matamshi tata..!?
 
View attachment 376327Rais Uhuru Kenyatta amemsamehe diwani kutoka Kisii ambaye alimtusi kwa kumwambia aache kuvuta bangi.

Mnamo Agosti 28'2013 akiwahutubia wakazi wa Kerera, diwani wa Kiogoro Samuel Aboko Onkwani alinukuliwa akisema, "wale wako karibu na Rais Uhuru Kenyatta wanapaswa kumshauri aache kuvuta bangi."

Matamshi ya Bw Onkwani yalimfanya ashtakiwe kwa kudhalilisha mamlaka ya afisa wa umma kinyume na kipengele cha Penal Code.

Alhamisi katika mkutano na madiwani wa Kisii na Nyamira, Rais Kenyatta alitangaza msamaha kwa diwani huyo na kumwambia asahau yaliyopita. "Sahau yaliyopita na turidhiane"Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Kidigitali katika Ikulu Denis Itumbi alimnukuu Rais Kenyatta.

Bw Onkwani ambaye alikuwa miongoni mwa madiwani wa Kisii na Nyamira waliomtembelea Rais Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi alionekana akisalimiana na kupeana pambaja na Rais Kenyatta kama ishara ya msamaha.

Kesi dhidi ya diwani huyo ilikuwa bado inaendelea kortini japo kupitia mawakili Gideon Nyambati na Isaiah Mosota, diwani huyo alikuwa amekanusha mashtaka hayo.

Madiwani 58 kutoka Kaunti ya Kisii na wenzao 29 kutoka kaunti ya Nyamira walikutana na Rais Kenyatta na Naibu Rais William Ruto kupanga ziara ya Rais maeneo hayo na kujadiliana kuhusu miradi ya maendeleo atakayozindua.

MPE HONGERA ZAKE KWA KUPATANA
 
Hahahaha aiseee huo ndio ubinadamu sio kila kitu kutumia nguvu kubwa kwa sababu tu una nguvu hiyo ila huyo jamaa lazima anakula sana majani


Pambaja ni kitu gani ??

Maana yake ni kukumbatia,lakini siyo ile ya mapenzi kati ya Ke na Me la hasha ni ile ya kiushkaji kama wanavyofanyaga vijana kugusana mabegani kwa kiingereza nafikiri itakua ni ku hug.
 
Maana yake ni kukumbatia,lakini siyo ile ya mapenzi kati ya Ke na Me la hasha ni ile ya kiushkaji kama wanavyofanyaga vijana kugusana mabegani kwa kiingereza nafikiri itakua ni ku hug.
Asante Mkuu hilo neno nilikua sijawahi kulisikia ,ama kweli kiswahili kipana
 
Hahahaha aiseee huo ndio ubinadamu sio kila kitu kutumia nguvu kubwa kwa sababu tu una nguvu hiyo ila huyo jamaa lazima anakula sana majani


Pambaja ni kitu gani ??
Hahahah labda pambaja ni ile hug flan ya kugonganisha mabega ile...
huyu jamaa atakuwa anakula sana majani ila kwa faida,ndo mana yuko cool full kusizi,roho ya kirasta ndo mana anasamehe,si unajua zile irie rasta good gwan whatagwan man??!...
siyo kama yule wa nchi flan inaonekana ujanani alikuwa anavuta majani mabichi saiz uzeeni ndo yanakaukia kichwani anawapeleka wananchi wake kwa speed ya mwendokasi.hahaha
 
Hahahah labda pambaja ni ile hug flan ya kugonganisha mabega ile...
huyu jamaa atakuwa anakula sana majani ila kwa faida,ndo mana yuko cool full kusizi,roho ya kirasta ndo mana anasamehe,si unajua zile irie rasta good gwan whatagwan man??!...
siyo kama yule wa nchi flan inaonekana ujanani alikuwa anavuta majani mabichi saiz uzeeni ndo yanakaukia kichwani anawapeleka wananchi wake kwa speed ya mwendokasi.hahaha
napinga always watu wanaokula mmea huwa wako very humbled,ungesema ni mlevi ndomana anapeleka watu puta ningekuelewa maana unaweza kuamka na hangover alafu unahasira utaekutana nae mbele yako atapata shida
 
Asante Mkuu hilo neno nilikua sijawahi kulisikia ,ama kweli kiswahili kipana
Kiswahili kina maneno mengi fasaha ambayo wabongo hatuyatumii mimi mwenyewe nilikuwa sifahamu lakini kila nikitazamaga Tv za wakenya huwa napata misamiati mipya kila mara kwani wao huwa wanatumia sana kiswahili cha kwenye kamusi,kwa hiyo ukiwasikiliza wanaweza kukuacha sana bila kungamua wanasema nini.
 
Hongera Uhuru,wa kwetu hajui kusamehe
 
Maana yake ni kukumbatia,lakini siyo ile ya mapenzi kati ya Ke na Me la hasha ni ile ya kiushkaji kama wanavyofanyaga vijana kugusana mabegani kwa kiingereza nafikiri itakua ni ku hug.
Afadhali mkuu.. si unajua tena sisi watu wa pwani kiswahili chetu
 
Back
Top Bottom