Rais Uhuru Kenyatta atoa amri ya kufungwa kwa boda ya Kenya-Tanzania na Kenya-Somalia kwa siku thelathini

Rais Uhuru Kenyatta atoa amri ya kufungwa kwa boda ya Kenya-Tanzania na Kenya-Somalia kwa siku thelathini

pingli-nywee

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
11,923
Reaction score
13,350
Huu ndio muendelezo wa mapigo ya kuipuuza kuibeza na kuiita Corona kaugonjwa kadogo. Sasa hasara itatuandama sisi sote, wakenya kwa watanzania, baada ya rais Kenyatta kufunga boda kati ya Kenya na Tanzania na pia Kenya-Somalia. Amri ambayo itadumu kwa siku thelathini zijazo.

Sio jambo njema wala la kufurahiwa ila haina budi kufikia maamuzi kama haya ili kujilinda dhidi ya maambukizi zaidi ya Corona. Ikitiliwa maanani kwamba Kenya imetimiza hatua nyingi, kwenye malengo yake ya vita dhidi ya maambukizi ya Corona. Hatua zote hizo na shughuli zote hizo zitakua za bure iwapo tutalegeza kamba. Hadi leo hii kwenye boda Kenya imewazuia madereva 78 kuingia nchini, baada ya wao kupatikana wana virusi vya Corona.

 
Ni haki yake hata hivyo, kila mtu ana haki ya kuamua nani aingie na yupi asiingie nyumbani kwake, binafsi sioni tatizo hapo, so far so good, ila waathirika wakubwa hapo ni chadema, au niseme wapiga kura wa chadema wao ndio waliojazana Kenya, lkn cha ajabu wamejaa hapa kushangilia, ...

Low IQ!
 
sasa wacha tuone vile joto la jiwe atasema!
Hapo hamjafunga mpaka. Sisi tunasema kwamba Kenya haiwezi kusurvive bila chakula na raw materials kutoka Tanzania, ndio sababu amesema "except cargo vehicles", kama ninyi ni wababe kwanini msifunge mpaka "completely?", yaani msiruhusu Gari wala mtu yeyote kupita? Kenya bila Chakula cha Tanzania, raw materials na kuitumia ardhi ya Tanzania kupitisha bidhaa zake kwenda nchi za kusini, uchumi wake hauwezi kusimama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi Kama Tanzania tunalishaa Kenya, tukifunga mpaka watakufa. Wacha tuone Kama mnatulisha nyie

Sent using Jamii Forums mobile app
Sanasana mumezuia wale wakenya pale Kajiado kuvuka kuingia Tanzania kwenda kunywa pombe upande wa Tanzania, kwanini msizuie hata "Cargo vehicles" kuingia Kenya?, ninyi bila chakula cha Tanzania hamuwezi kuishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
siku 30 tu.basi vizuri
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio protokali za kiserikali, siku 30 kwanza ila haimaanishi kwamba ndio itakuwa mwisho. Wakitaka baada ya hizo siku 30 wanafanya extension ya siku zingine. Kama ilivyokuwa kwa curfew, ambayo ilikuwa ya siku 21 na marufuku ya safari za ndege nje ya nchi ambayo ilikuwa ya siku 30 hapo awali.
 
Sanasana mumezuia wale wakenya pale Kajiado kuvuka kuingia Tanzania kwenda kunywa pombe upande wa Tanzania, kwanini msizuie hata "Cargo vehicles" kuingia Kenya?, ninyi bila chakula cha Tanzania hamuwezi kuishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kizungu uelewi ama nini? Mipaka imefungwa completely,hakuna ata mizigo inakubaliswha kuingia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo hamjafunga mpaka. Sisi tunasema kwamba Kenya haiwezi kusurvive bila chakula na raw materials kutoka Tanzania, ndio sababu amesema "except cargo vehicles", kama ninyi ni wababe kwanini msifunge mpaka " completely?", yaani msiruhusu Gari wala mtu yeyote kupita? Kenya bila Chakula cha Tanzania, raw materials na kuitumia ardhi ya Tanzania kupitisha bidhaa zake kwenda nchi za kusini, uchumi wake hauwezi kusimama.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tumefunga mipaka kwa wabeba korona! awe dereva wa lori au yeyote yule toka Tanzania. Akipimwa mpakani apatikane positive hakuna kuingia anabaki kutolea povu hapo mpakani.
 
Ni kizungu uelewi ama nini? Mipaka imefungwa completely, hakuna ata mizigo inakubaliswha kuingia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kenya haina uwezo wa kuzuia "Cargo vehicle" kutoka Tanzania kuja Kenya, bila chakula cha Tanzania Kenya haiwezi kusurvive. Kenya siku ikifunga mipaka na Tanzania "total closure", ndani ya wiki moja kutatokea " Civil disobedience " na Serikali itapinfuliwa. Msikilize vizuri Uhuru Kenyatta anasema "Except for Cargo vehicles", Hahahaha, hahahaha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom