Rais wa Algeria akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Tax katika Ikulu ya Algiers

Rais wa Algeria akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Tax katika Ikulu ya Algiers

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Waziri Tax.JPG
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Abdelmadjid Tebboune amekutana Kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax (Mb.) alipomtembelea Ikulu Jijini Algiers, Algeria tarehe 1 Agosti 2023.

Mazungumzo hayo yamefanyika pembezoni mwa Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Algeria unaofanyika kuanzia tarehe 30 Julai 2023 hadi 1 Agosti 2023.

Mazungumzo ya viongozi hao yalijikita katika kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kirafiki na kidiplomasia ili kuweza kutekeleza diplomasia ya uchumi kwa maslahi mapana ya nchi zao.

Tax.JPG

Aidha, katika kuendelea kuimarisha ushirikiano Mhe. Waziri Dkt. Tax pamoja na majukumu mengine, atafungua rasmi Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 2 Agosti 2023 Jijini Algiers.

Ufunguzi rasmi wa ofisi za ubalozi huo ni hatua muhimu hasa wakati huu ambapo viongozi hao wamekubaliana kuinua uchumi kupitia sekta za biashara, uwekezaji, nishati, madini, elimu, sayansi na teknolojia, afya na utalii.
 
Back
Top Bottom