Rais wa Burkina Faso akopa Tractors 400 ili nchi yake iwe na Maendeleo Mazuri

Rais wa Burkina Faso akopa Tractors 400 ili nchi yake iwe na Maendeleo Mazuri

Ukikopa kumbuka kulipa, ngoja atafute sifa. Atashangaa na mvua hazinyeeshi baada ya kukopa matreka. Muda wa kulipa ukifika tunaanza kulia lia ohoo mtusamamehe, unajua sisi ni taifa changa.
 
Huyu kijana anauongozi wa mihemuko sana kawaida kwa viongozi wa bala hili la giza
Roho mbaya maskini tuliojaliwa wa africa kuona anguko la mwingine daah africa aliyeturoga kwa kwel atusamehe et mihemuko mungu akileta viongozi wenye maono wanapigwa spana wataitwa magaid na madikiteta utasikia wanapenda sifa kisa tu atabana wala rushwa na magaidi sasa wew huko bukinafaso wakifeli wew kinakuuma nini utapungukiwa nini utapata kitu gani.....
 
Hao ndiyo viongozi tunaotaka.%kubwa ya waafrica wamejiajiri kupitia kilimo.hapo atarahisisha kilimo Kwa Nchi yake.Siyo kama sisi hapa tumezungukwa na maziwa pande zote lakini viongozi bado wamelala usingizi
 
Huyu kijana anauongozi wa mihemuko sana kawaida kwa viongozi wa bala hili la giza

Alichukua uongozi kijeshi hivyo anaongoza kibabe, kila anachoamua yeye ndio kinafanyika, hawezi akashaurika, ukimbishia unalo.
Madikteta wote huwa na nia nzuri za kizalendo lakini ile kutishaurika au kubishiwa huwa wanaharibu, akiamua kununua mindege hata kama haina tija ananunua tu.
Na hulazimisha kila awe chawa.
 
Alichukua uongozi kijeshi hivyo anaongoza kibabe, kila anachoamua yeye ndio kinafanyika, hawezi akashaurika, ukimbishia unalo.
Madikteta wote huwa na nia nzuri za kizalendo lakini ile kutishaurika au kubishiwa huwa wanaharibu, akiamua kununua mindege hata kama haina tija ananunua tu.
Na hulazimisha kila awe chawa.
Kwani unafikir ulaya maendeleo yalipatikana kutokana demokrasia wanayoihubir?? Au husomi historia ndugu Afrika inahitaji watu kama kina Gaddafi, Maguful Kagame na makatili wengine tukishaendelea huko mbeleni ndio tutaongelea demokrasi...
 
Lengo sio lingine bali ameona chakula kingi kinanunuliwa kutoka nje kwa kutumia hela za ziada huku zingine zikipigwa
Ameamua walime ili wazalishe chakula kingi ndani ya nchi
Sio matrekta tu pia katoa na pikipiki nyingi sana kwa ajili ya mabwana shamba hata baiskeli nafikiri
Kama watapambana bila kuhujumu au kuiba basi wataweza maana wapo 24m tu sio wengi hivyo
 
Kwani unafikir ulaya maendeleo yalipatikana kutokana demokrasia wanayoihubir?? Au husomi historia ndugu Afrika inahitaji watu kama kina Gaddafi, Maguful Kagame na makatili wengine tukishaendelea huko mbeleni ndio tutaongelea demokrasi...

Haya mambo ya one man show sio ya zama hizi, kwamba uchukue nchi kijeshi kisha uanze kulazimisha kila unachoamka nacho.
 
Roho mbaya maskini tuliojaliwa wa africa kuona anguko la mwingine daah africa aliyeturoga kwa kwel atusamehe et mihemuko mungu akileta viongozi wenye maono wanapigwa spana wataitwa magaid na madikiteta utasikia wanapenda sifa kisa tu atabana wala rushwa na magaidi sasa wew huko bukinafaso wakifeli wew kinakuuma nini utapungukiwa nini utapata kitu gani.....
Kabisa, hiyo ni roho mbaya, kijana huyo kafanya vizuri sana kuliko kukopa fedha za kuwezesha semina, kulipa posho na kununua vifaa vya kijeshi
 
Back
Top Bottom