Rais wa Ghana, John Mahama ametangaza marufuku ya safari za Ndege za daraja la kwanza kwa Maafisa wa Serikali

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Rais wa Ghana, John Mahama ametangaza marufuku ya safari za Ndege za daraja la kwanza kwa Maafisa wa Serikali wakiwemo Mawaziri ikiwa ni sehemu ya juhudi za kupunguza matumizi ya Serikali.


Aidha Rais Mahama amesisitiza kuwa safari za dharura pekee ndizo zitakubaliwa na lazima zidhinishwe na Ofisi ya mkuu wa Wafanyakazi.


Aliongeza kwa kusema kuwa Maafisa wanapaswa kuepuka matumizi ya anasa na kutumia rasilimali za umma kwa busara akisisitiza kuwa fedha za Serikali zinapaswa kuelekezwa katika kuboresha maisha ya Wananchi wa Ghana badala ya kupotezwa kwenye anasa.
 
hiyo picha ni ya Rais mstaafu wa Ghana ,Nana Akufo-Addo.Jitahidi kufanya utafiti kabla ya kuandika chapisho lolote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…