Rais wa Marekani Joe Biden aanguka jukwaani

Rais wa Marekani Joe Biden aanguka jukwaani

Kinyungu

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2008
Posts
19,484
Reaction score
38,416
Leo Rais Biden wa USA ameanguka jukwaani wakati akisalimiana na Wahitimu wa chuo cha kijeshi cha Anga huko Colorado, chanzo cha kuanguka hakijulikani kama amejikwaa au ni umri mkubwa kiasi kwamba anapoteza balance. Mara baada ya kuanguka maafisa wa usalama wamemsaidia kuinuka fasta na kumpeleka sehemu ya kukaa. Jionee mwenyewe jinsi alivyoanguka






My take: Biden amezeeka sana asigombee tena urais Mwakani. Atafia jukwaani huyu

=========

Bwana Biden, ambaye ni Rais mwenye umri mkubwa zaidi nchini akiwa na miaka 80, alisaidiwa kuinuka na kuonekana kuwa salama baada ya kuanguka alipokuwa akirejea kwenye kukaa baada ya kuhutubia kwenye Mahafali ya Chuo cha Kijeshi cha Anga huko Colorado (US Air Force Graduation Ceremony).

Alionekana akirudi kiti chake bila msaada na baadaye akakimbia kurudi kwenye msafara wake wa magari baada ya sherehe kumalizika muda mfupi baada ya tukio hilo.

Ripoti ya kikundi cha waandishi wa habari wa Ikulu ya White House ilisema awali kwamba Bwana Biden alijikwaa kwenye mifuko miwili nyeusi ya mchanga alipokuwa akitoka jukwaani. Mwandishi wa kikundi hicho aliongeza kuwa Rais hakujibu maswali aliporejea kwenye ndege yake.

Msemaji wa vyombo vya habari vya Ikulu ya White House, Karine Jean-Pierre, alisema Bwana Biden alikuwa "Vizuri kabisa" na alipanda ndege huku akionyesha "Tabasamu kubwa".

"Nilitegwa na mchanga," alidokeza Biden akiwa na tabasamu kwa waandishi wa habari alipofika nyumbani katika Ikulu ya White House siku hiyo jioni.

Mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu ya White House alisema awali "Rais yuko sawa".

Wakosoaji wamesema kwamba Bwana Biden ni mzee sana kuwania muhula wa pili kama Rais.

Uchunguzi wa hivi karibuni unaonyesha kuwa wapiga kura wengi nchini Marekani wanahofia umri wake mkubwa. Atakuwa na umri wa miaka 82 mwanzoni mwa muhula wake wa pili ikiwa atashinda.

Kujikwaa huko, pamoja na misukosuko ya awali kama kuporomoka kutoka kwenye baiskeli yake na kupanda ngazi za Air Force One, inaweza kuongeza wasiwasi huo.

BBC
 
duh aiseee.
.
20230521_214422.jpg
 
HII NI MARA YA NNE

Mar 2021 alianguka kwenye ngazi za ndege


Jun 2022 alianguka akiwa kasimamisha baiskeli


Feb 2023 alianguka mara 3 kwenye ngazi za ndege


Jun 2023 Leo, kaanguka kwenye mahafali ya jeshi la anga


Hapo ni nje ya matukio mengi mno ya kupoteza kumbukumbu ( juzi kasema mtoto wake mzima wa afya kwamba kafariki )

Media zina double standards sana, Kuna kipindi trump alitembea kama ananyata hivi wakati anashuka ngazi sababu ngazi zilikuwa na maji huku yeye kavaa viatu vya leather (hakuanguka) Media zikapiga kelele mwezi mzima kwamba ni mgonjwa ajiuzuru uraisi, Ingetokea kaanguka ingekuwa habari ya mwaka mzima. Ila kwa Biden hili ni tukio la nne kudondoka media zipo kimyaaa!!!

Siasa za marekani Media zinashambulia sana chama cha republicans wanaotaka kuiweka nchi kwenye mstari ila kinawapa sana promo chama cha Democrats wanaoharibu nchi kwa ushoga, kufundisha watoto wa chekechea s*x, kupromote utoaji wa mimba holela, n.k. kipindi cha trump ilikuwa rahisi mno kubrain wash hata wabongo wamchukie Trump bila kujua ukweli kwamba Mwamba anapigwa vita sababu ya kupinga mambo ya hovyo ya democrats.
 
Leo Rais Biden wa USA ameanguka jukwaani wakati akisalimiana na Wanafunzi wa chuo cha kijeshi huko USA, chanzo cha kuanguka hakijulikani kama amejikwaa au ni umri mkubwa kiasi kwamba anapoteza balance. Mara baada ya kuanguka maafisa wa usalama wamemsaidia kuinuka fasta na kumpeleka sehemu ya kukaa. Jionee mwenyewe jinsi alivyoanguka
View attachment 2642962





My take: Biden amezeeka sana asigombee tena urais Mwakani. Atafia jukwaani huyu

Amejikwaa ni kawaida huyo sio malaika..

Uzuri wenzetu wapo simple na wanauelewa mzuri sana hata hawajataka kumuarakisha kusimama au kuzibaziba camera ila mpaka yy mwenyewe alivyoonesha yupo teyar kusimama wakamsaidia sasa.
 
Amejikwaa ni kawaida huyo sio malaika..

Uzuri wenzetu wapo simple na wanauelewa mzuri sana hata hawajataka kumuarakisha kusimama au kuzibaziba camera ila mpaka yy mwenyewe alivyoonesha yupo teyar kusimama wakamsaidia sasa.
Ni kweli kujikwaa ni kawaida ila inaonekana huyu stress za kazi pia zinamzidia na umri unachangia . Anastahili kupumzika acheze na vitukuu sasa.
 
Leo Rais Biden wa USA ameanguka jukwaani wakati akisalimiana na Wahitimu wa chuo cha kijeshi cha Anga huko Colorado, chanzo cha kuanguka hakijulikani kama amejikwaa au ni umri mkubwa kiasi kwamba anapoteza balance. Mara baada ya kuanguka maafisa wa usalama wamemsaidia kuinuka fasta na kumpeleka sehemu ya kukaa. Jionee mwenyewe jinsi alivyoanguka
View attachment 2642962





My take: Biden amezeeka sana asigombee tena urais Mwakani. Atafia jukwaani huyu

Noop ametekwa na kamba
 
Leo Rais Biden wa USA ameanguka jukwaani wakati akisalimiana na Wahitimu wa chuo cha kijeshi cha Anga huko Colorado, chanzo cha kuanguka hakijulikani kama amejikwaa au ni umri mkubwa kiasi kwamba anapoteza balance. Mara baada ya kuanguka maafisa wa usalama wamemsaidia kuinuka fasta na kumpeleka sehemu ya kukaa. Jionee mwenyewe jinsi alivyoanguka
View attachment 2642962





My take: Biden amezeeka sana asigombee tena urais Mwakani. Atafia jukwaani huyu

Uzee umezidi huyu. Hafai wala kugombea urais mwakani.
 
Back
Top Bottom