Rais wa Senegal, Bassirou Faye: Ufaransa ifunge kambi zake za kijeshi nchini Senegal. Hii ni nchi huru; hatukubaliani na uwepo wa kambi hizo

Kila siku wanatamba
 
Utawala wa ndugu Macron umekumbwa na balaa gani, mbona anapoteza makoloni yake tofauti na watangulizi wake Kina De Gaulle, Chiraq etc
Mapinduzi ya Sahel yameamsha wengi. Pia internet na social media sasahivi hudanganyi mtu. Taarifa zote tunazo. Pia tunakumbuka Ufaransa ilivyochangia pakubwa yaliyotokea Libya mwaka 2011. Na pia inasemekana kuna mkono wa Bwana Putin ingawa hilo siwezi kuthibitisha
Kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho
 
Hivi umeuona umasikini uliopo Yemen?!

Hivi mnafikiri US akiamua kuingia Yemen na kuwaondoa hao Wahouthi atashindwa?!
Unadhani hatamani kuwaondoa eeenh Yale mabomu waliokua wanawapiga Wahouthi tokea mwaka 2014 mpaka 2021 unadhani walikua anania nao gani
 
Utawala wa ndugu Macron umekumbwa na balaa gani, mbona anapoteza makoloni yake tofauti na watangulizi wake Kina De Gaulle, Chiraq etc
Kwakweli sijajua macron anakumbwa nanini ila nakumbuka kuna day nilisikiliza uchambuzi DW pale kuna jamaa kama sijakosea anaitwa Ahmed Salim mwamba alielezea tu kwamba Watawala vijana wamechoshwa na sera za ufaransa ufaransa wana sera moja Ile ya pesa sijui jamaa aliichambua vyema nimeisahau tu hakuna mkoloni mzuri ila mkoloni mfaransa hafai hafai hafai na hapo west Africa anaondoka jumla ni suala la muda tu kwa sasa anaendelea kumzibia awepo hapo ni Nigeria 🇳🇬 kama Senegal 🇸🇳 atafanya kweli basi na Nigeria anafuata na akisepeshwa na Nigeria kwisha habari zake yaani
 
Kuna mikataba ya uhuru ambayo nchi zilizokuwa makoloni ya Ufaransa zililazimishwa kusaini Ili zipate uhuru. Zote zilisaini isipokuwa Guinea, Morocco na Algeria. Na pia hao ambao hawakusaini haikuwa rahisi walipoteza mamilioni ya raia Ili wapate uhuru bila kusaini hiyo mikataba. Ukiisoma utamwaga machozi. Ufaransa anachokifanya ni zaidi ya unyonyaji. Hamna lugha ya kuelezea. Acha wamfukuze tu. WAMECHOKA
 
Unadhani hatamani kuwaondoa eeenh Yale mabomu waliokua wanawapiga Wahouthi tokea mwaka 2014 mpaka 2021 unadhani walikua anania nao gani
US ni Superpower ikiamua kuwachakaza hao Houthi anaweza.
 
Asee wafaransa washenzi sana kwakweli
 
.mrusii balaaa huyooo anaingiza timu
 
 

Attachments

  • 89C5054F-64C0-4369-A9C8-D85CE41105AA.jpeg
    63.1 KB · Views: 1
Ufaransa kakaliwa kooni kila pembe wanamkataa safi sanaaa watu Wanaanza kujitambua
Kituo kinachofuata ni Mauritania na Chad +Gambia
Mfaransa ni mshenzi sana yaani huyu ndio mkoloni mpuuzi ambaye bado naendelea kukumbatia makoloni yake kama mali yake , yaani hiyo west Africa ,Central na North aliimegea kipande kikubwa na bado anaendelea kukikumbatia mpaka leo
Mpuuzi sana
Wafurushwe huko kama walivyotimuliwa mali ,bukina , Niger
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…