Rais wa Shirikisho la soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe kuwania tena Urais 2025
Rais wa sasa wa Shirikisho la soka Afrika (CAF), Patrice Motsepe ametangaza kuwania tena kiti hicho katika uchaguzi utakao fanyika Machi 2025.
kufuatia maombi kutoka kwa wanachama wa CAF, marais wa vyama vya kanda na washikadau Hatimaye Rais wa CAF DR Motsepe, amekubali kuwa mgombea katika uchaguzi huo.
Ikumbukwe Motsepe ndiye tajiri namba 1 kwa watu weusi pale nchini Afrika Kusini akiwa na utajiri wa dola bilioni 3 sawa na Tsh. Trilioni 8.2.