Rais wa Tanzania ni mwajiri au mwajiriwa?

Rais wa Tanzania ni mwajiri au mwajiriwa?

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Ni vigumu kutambua nafasi ya Rais wa Tanzania hasa katima hoja aidha ni mwajiri wa wananchi au ni mwajiriwa wa wananchi.

Marais waliopita wametengeneza dhana kwamba wao ni waajiri wa wananchi huku wanapokuwa kwenye Mikutano ya adhara wakihubiri kwamba wao ni waajiriwa. Rais wa Tanzania anaogopwa na wananchi na awezi kukosolewa anapokwenda mrama, katika mazingira haya utabaini huyu siyo mwajiriwa Bali n mwajiri. Siku zote mwajiriwa umheshimu mwajiri lakini ukiona mwajiriwa anakosa nidhamu kwa mwajiri Basi amechoka kazi.

Kama tunakubaliana huyu Ni mwajiriwa Basi lazima tukubali kwamba anapaswa kukosolewa na kuondolewa madarakani pale inapoonekana afai kufanya kazi tuliyompa. Wananchi kushindwa kumkosoa Rais aidha kwa staha au bila staha Ni kielelezo Cha Rais kugeuka kuwa mwajiri wetu.

Niombe tuanze mchakato wa kujinasua mikononi mwa kuajiriwa na Rais, tuzinduke tuweke mkakati wakumwajiri Rais. Zuma, Trump na Marais wengine wa aina yao wameajiriwa na wananchi. Ni vigumu mtu mmoja kuajiri watu milioni 60+ , huyu ni mwajiriwa wetu na tunapaswa kumwajibisha anapokwenda kombo. Tudai katiba inayotupa mamlaka yakumwajiri Rais
 
Bila katiba rais atakua ndio mwajiri mkuu
Maana sio kwa nafasi hizo alizonazo ambazo ni za kuteua na kuchagua
 
Hii frequency unayotumia iko juu sana ya uelewa wa watu wengi humu. Muda siyo mrefu wengine watakuja kufananisha uraisi na ubaba au umama na hoja za sikio halizidi kichwa. Inabidi uishushe kidogo ili wengi waelewe muktadha wa hoja yako.
 
Raisi wa Tanzania ni Mkoloni wa nchi. Huiba atakavyo, huua atakavyo, hupeleka maendeleo anakopenda, hujenga chochote kwa utashi wake, huchagua Nani awe nani bila kujali ana akiki au Hana. Huwa ndio mkoloni wa kweli wa taifa
 
Raisi wa Tanzania ni Mkoloni wa nchi. Huiba atakavyo, huua atakavyo, hupeleka maendeleo anakopenda, hujenga chochote kwa utashi wake, huchagua Nani awe nani bila kujali ana akiki au Hana. Huwa ndio mkoloni wa kweli wa taifa

Hadi nimemkumbuka Marehem
 
Raisi wa Tanzania ni Mkoloni wa nchi. Huiba atakavyo, huua atakavyo, hupeleka maendeleo anakopenda, hujenga chochote kwa utashi wake, huchagua Nani awe nani bila kujali ana akiki au Hana. Huwa ndio mkoloni wa kweli wa taifa

Hadi nimemkumbuka Marehem
 
Rais wa Tanzania ni mwajiri na mwajiriwa wa watanzania. Ni mwajiri namba moja. Lakini pia ni mwajiriwa namba moja na tunamlipa mshahara kupitia kodi zetu!
 
Back
Top Bottom