Rais wa Urusi, Vladimir Putin 'Chupuchupu' kuuawa

Rais wa Urusi, Vladimir Putin 'Chupuchupu' kuuawa

Annunaki

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2021
Posts
2,042
Reaction score
3,674
Habari kutoka Shirika la habari la Reuters zinaeleza kwamba Jasusi mbobezi, Rais wa Urusi, Vladimir Putin alinusirika Kuuawa mwanzoni kabisa mwa mgogoro wa Vita ya Ukraine.

Kwa sasa Putin inawezekana ndiye Rais anayeishi kwa wasiwasi mkubwa kuliko Marais wote wa nchi nyingine duniani.

Putin kwa sasa ni kama anapambania uhai wake, inawezekana maisha yake yapo hatarini kuliko hata ya Zelensky au kiongozi mwingine yeyote yule wa Kremlin.

______________

Vladimir Putin: Rais wa Urusi 'chupuchupu' kuuawa

Rais wa Urusi Vladimir Putin alinusurika katika jaribio la mauaji muda mfupi baada ya kuanza kwa vita nchini Ukraine, afisa mkuu wa jeshi la Ukraine amesema. Baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa, vikiwemo NDTV na New York Post, vimeripoti habari hiyo leo, vikilinukuu gazeti la Ukraine la Ukrainska Pravda.

Jenerali Kyrylo Budanov, mkuu wa upelelezi wa ulinzi wa Ukraine, amefichua habari kuhusu jaribio la kumuua Putin ambalo halikufaulu. Alisema tukio hilo lilitokea katika eneo la Caucasus.

Habari hizo zinakuja huku kukiwa na mvutano unaoongezeka kati ya Urusi na Ukraine, pamoja na kuongezeka kwa uvumi kuhusu afya ya Putin. Eneo la Caucasus, ambako lilifanyika jaribio la kumuua Putin muda mfupi baada ya kuzuka kwa uhasama nchini Ukraine mnamo Februari 24, liko kati ya Bahari Nyeusi na Bahari ya Caspian.

Taarifa gani hasa zilitolewa na afisa huyu wa upelelezi?

Jenerali Kyrylo Budanov alizungumzia suala hilo katika mahojiano na gazeti la mtandaoni la Ukrainska Pravda.

"Kulikuwa na jaribio la kumuua Putin ... kulingana na maajenti wa Caucasus, si muda mrefu sana uliopita," Bw Budanov alinukuliwa akisema na gazeti la Ukraine.

"Habari hizi hazikuwekwa wazi. Ilikuwa ni kitendo kilichoshindwa kabisa, lakini jaribio hilo lilifanyika kweli ... Ilikuwa takriban miezi miwili iliyopita," aliongeza.

Madai hayo bado hayajathibitishwa na vyanzo huru, lakini habari hizo zinakuja wiki chache baada ya ripoti kuibuka kuwa Bw Putin alifanyiwa upasuaji wa kutoa mafuta kwenye tumbo lake.

Operesheni hiyo "ilifanikiwa sana na hakukuwa na athari", kulingana na ripoti hiyo. Taarifa kuhusu upasuaji wa Putin zilichapishwa kwenye kituo cha Telegram cha SVR, ambacho kinashirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi.

Kulikuwa na taarifa nyingine kutoka kwa mfanyabiashara tajiri ambaye ni rafiki wa karibu wa Putin, ambaye alisema kuwa "Putin anaumwa sana na saratani ya damu".

Mapema mwezi huu, Bw Budanov, katika mahojiano na Sky News, alisema vita vya Ukraine vitakuwa na awamu mpya katikati ya Agosti na vitamalizika mwishoni mwa mwaka, na kusababisha mabadiliko ya utawala nchini Urusi.

Pia alisema kuwa "mapinduzi ya kijeshi" yalikuwa yanaendelea na kwamba hii haiwezi kusitishwa.

Chanzo: BBC
Screenshot_20220525-125152_1.jpg
 
Hi i wewe huu ushabiki unaouoleta humu unanufaika nao kwa lipi?

Kila siku habari mbaya za urusi ina maana wao hakuna successiful story uliyoiona kwa urusi?

Jaribu basi kuandika stori zilizobalansika na zenye kua na uhakika, hayo mahaba yako peleka kwa mkeo hatutaki stori za mihemko hapa
 
Hi i wewe huu ushabiki unaouoleta humu unanufaika nao kwa lipi?

Kila siku habari mbaya za urusi ina maana wao hakuna successiful story uliyoiona kwa urusi?

Jaribu basi kuandika stori zilizobalansika na zenye kua na uhakika, hayo mahaba yako peleka kwa mkeo hatutaki stori za mihemko hapa
Habari nzuri za Urusi zipo nyingi tu, ila mimi pro Ukraine siyo jukumu langu kuzileta, hizo mnaleta nyie pro Russia. Mimi kama pro Ukraine kazi yangu ni kuleta habari nzuri za Ukraine na mbaya kama hizi za Urusi.

Hizi habari ni njema sana kwetu sisi tunao muunga mkono wa Ukraine, habari njema za Urusi mnatakiwa mlete nyinyi pro Russia.

Kwhy tuvumiliane tu hamna namna.
 
Habari kutoka Shirika la habari la Reuters zinaeleza kwamba Jasusi mbobezi, Rais wa Urusi, Vladimir Putin alinusirika Kuuawa mwanzoni kabisa mwa mgogoro wa Vita ya Ukraine.

Kwa sasa Putin inawezekana ndiye Rais anayeishi kwa wasiwasi mkubwa kuliko Marais wote wa nchi nyingine duniani.

Putin kwa sasa ni kama anapambania uhai wake, inawezekana maisha yake yapo hatarini kuliko hata ya Zelensky au kiongozi mwingine yeyote yule wa Kremlin.

______________

Vladimir Putin: Rais wa Urusi 'chupuchupu' kuuawa

Rais wa Urusi Vladimir Putin alinusurika katika jaribio la mauaji muda mfupi baada ya kuanza kwa vita nchini Ukraine, afisa mkuu wa jeshi la Ukraine amesema. Baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa, vikiwemo NDTV na New York Post, vimeripoti habari hiyo leo, vikilinukuu gazeti la Ukraine la Ukrainska Pravda.

Jenerali Kyrylo Budanov, mkuu wa upelelezi wa ulinzi wa Ukraine, amefichua habari kuhusu jaribio la kumuua Putin ambalo halikufaulu. Alisema tukio hilo lilitokea katika eneo la Caucasus.

Habari hizo zinakuja huku kukiwa na mvutano unaoongezeka kati ya Urusi na Ukraine, pamoja na kuongezeka kwa uvumi kuhusu afya ya Putin. Eneo la Caucasus, ambako lilifanyika jaribio la kumuua Putin muda mfupi baada ya kuzuka kwa uhasama nchini Ukraine mnamo Februari 24, liko kati ya Bahari Nyeusi na Bahari ya Caspian.

Taarifa gani hasa zilitolewa na afisa huyu wa upelelezi?

Jenerali Kyrylo Budanov alizungumzia suala hilo katika mahojiano na gazeti la mtandaoni la Ukrainska Pravda.

"Kulikuwa na jaribio la kumuua Putin ... kulingana na maajenti wa Caucasus, si muda mrefu sana uliopita," Bw Budanov alinukuliwa akisema na gazeti la Ukraine.

"Habari hizi hazikuwekwa wazi. Ilikuwa ni kitendo kilichoshindwa kabisa, lakini jaribio hilo lilifanyika kweli ... Ilikuwa takriban miezi miwili iliyopita," aliongeza.

Madai hayo bado hayajathibitishwa na vyanzo huru, lakini habari hizo zinakuja wiki chache baada ya ripoti kuibuka kuwa Bw Putin alifanyiwa upasuaji wa kutoa mafuta kwenye tumbo lake.

Operesheni hiyo "ilifanikiwa sana na hakukuwa na athari", kulingana na ripoti hiyo. Taarifa kuhusu upasuaji wa Putin zilichapishwa kwenye kituo cha Telegram cha SVR, ambacho kinashirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi.

Kulikuwa na taarifa nyingine kutoka kwa mfanyabiashara tajiri ambaye ni rafiki wa karibu wa Putin, ambaye alisema kuwa "Putin anaumwa sana na saratani ya damu".

Mapema mwezi huu, Bw Budanov, katika mahojiano na Sky News, alisema vita vya Ukraine vitakuwa na awamu mpya katikati ya Agosti na vitamalizika mwishoni mwa mwaka, na kusababisha mabadiliko ya utawala nchini Urusi.

Pia alisema kuwa "mapinduzi ya kijeshi" yalikuwa yanaendelea na kwamba hii haiwezi kusitishwa.

Chanzo: BBCView attachment 2238039
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]utapata tabu sana Safari hiii ....Z
 
Back
Top Bottom