King Kong III
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 56,205
- 79,515
...unaelewa maana ya neno elimu bure?....kama serikali kupitia Kodi zetu imeshindwa kuleta viti na kuongeza madarasa inataka wananchi ndio wajikamua walete inawezaje kusema inatoa elimu bure?...ebu waulize viongozi wako wakati wanapewa elimu bure walikuwa wanaenda na viti shuleni wakati huo? iweje sasa tuko uchumi wa kati tunalazimisha mwananchi huyu mnyonge atoe elfu 50 ya kiti na elfu 10 ya ujenzi hapo bado michango ya maji mlinzi umeme na pesa za kila wiki za kuandaa mitihani ya majaribio... ushabiki kwenye elimu mtaliangamiza taifa tangazeni elimu ya kuchangia ili wazazi wajipqnge mapema kuliko kutangaza elimu bure wakati mnawavizia wazazi mashuleni wakileta watoto wanakutana na michango mingiSasa kwani kupeleka kiti cha kukalia mwanao nalo la kulalamika? Kwa kweli watanzania tumeambukizwa ujinga na tumekuwa wajinga webkama hupeleki kiti na meza mwanao atakaa chini nani unamkomoa?
Propaganda haijawahi shinda Hali halisiElimu bure ni kuwaonea waalmu ili kupata cheap popularity.
Kwa nini wasingesikiliza maoni ya wadau kwanza?
... wakati mnatangaza kwa vibesi kwamba mnatoa elimu bure mlikuwa mnataka kumfurahisha nani kama mlifahamu jeuri hiyo hamnayo?...acheni kucheza na maisha ya watoto wetu bora mngesema mapema wazazi wakajipangaYaani kutoa elfu 15 unapiga makelele ,mambo mengine yanatia hasira sana,nani alikwambia shule bure? Kama unaona kutoa elfu 15 nyingi mpeleke efeme akademia wakakupasue na ada ya milioni 2 ndio akili ikukae sawa.
Kuna mtendaji wa kata fulani Mkoa nilipo kaleta barua ya kuomba mchango kwa ajili ya shule ili imfikie boss wangu,tangu mwezi wa 12 nnayo na siifikishi kwa boss,maana hela kutoka serekali kuu zinatutosha hakuna haja ya kuwaumiza wengine na michango isiyo kuwa na kichwa wala mkia.Kuna wakati kelele za wapinzani huwafanya mawaziri wasilale lakini siyo sasa!
... wakati mnatangaza kwa vibesi kwamba mnatoa elimu bure mlikuwa mnataka kumfurahisha nani kama mlifahamu jeuri hiyo hamnayo?...acheni kucheza na maisha ya watoto wetu bora mngesema mapema wazazi wakajipanga
Inasikitisha yaani tamko mpaka litolewe na rais, hivi hao mawaziri walikuwa wapi???? Ina maana hawakuwa wanajua???
Msamehe hajui nini maana ya elimu bure na inawezekana anaishi kwa wifi hajui shida wanazokutana nazo wazazi wanapopeleka watoto wao shule hii mada inamzidi umri alipaswa akae kimya waongee wazazi/walezi sio walelewa inatia hasira Sana unapeleka mtoto shule unaambiwa utoe elfu 50 ya kiti na elfu 10 ujenzi ulipie maji na michango kede kede Mimi nimekutana nayo leo 14/01)2021 kangaye secondaryWe uko nchi gani?
Mbona michango ni nchi nzima
...uko sahihi ndg michango mashuleni sasa imekuja kwa kasi ya uchumi wa kati...tanesco ndo imeoza kabisa licha ya kusema nguzo bure hata ukilipia utakaa mpaka usahau kupata huduma Nina zaidi ya miezi 2 dana dana kibao wanatengeneza mazingira ujisachiTatizo mnawasikiliza sana wanasiasa,wanasiasa ni watu wa longolongo kupiga tantalila kudanganya wajinga! wao wanapiga longolongo kwenye majukwaa lakini field ni tofauti sasa ndio uanze kuelewa.
-Waziri anasema shule bure ukienda shule michango kama yote.
-Waziri anasema nguzo za umeme ni bure ,ukienda tanesco nguzo zinauzwa.
-Waziri anasema wazee na watoto hospital ni bure lakini ukienda lazima ulipe pesa.
Kwahiyo usiwasikilize wanasiasa wakipayuka majukwaani.
Kweli kabisaPropaganda haijawahi shinda Hali halisi
Muongo huyu.Hueleweki. Mara unasema hawatoi risiti wanaandika kwenye daftari, mara umeshindwa ku attach. Tuelewe nini sasa?
Kwani kuchangia hela ya kiti atakacho kalia mwanao au ujenzi wa darasa atakalotumia mwanao kuna ubaya?Msamehe hajui nini maana ya elimu bure na inawezekana anaishi kwa wifi hajui shida wanazokutana nazo wazazi wanapopeleka watoto wao shule hii mada inamzidi umri alipaswa akae kimya waongee wazazi/walezi sio walelewa inatia hasira Sana unapeleka mtoto shule unaambiwa utoe elfu 50 ya kiti na elfu 10 ujenzi ulipie maji na michango kede kede Mimi nimekutana nayo leo 14/01)2021 kangaye secondary
Ukweli ni kuwa Mh. Rais amefuta michango ya shule za serikali - video hiyo hapo juu. Kusema kamati za shule na wazazi wanakubaliana si kweli kwani shule na kamati zake nao wamegeuka wapigaji wanakaa na kutengeneza mihutasari feki na kuifanya imekubaliwa na wazazi. Hii nchi ni zaidi ya uijuavyo. Hata hivyo Rais ameshasema mwanafunzi asikataliwe shuleni eti hana mchango lakini hayo yapo kama mtoa hoja alivyoleta hoja yake.Mkuu inaonesha una sababu zako nyuma ya pazia. Ikiwa Huna ushahidi unafanya uchochezi. Hiyo michango ni Kwa ajili ya nini na Nani walikubaliana, ni wazi wenyewe au walimu ndo wameibua wenyewe? Ni vema ukawa na maelezo yaliyojitosheleza
Exactly mkuu siasa za hovyo hovyo tumeziweka ktk jambo hili la msingi.....Kuna siku nimehudhuria mkutano wa wazazi kule Tabora. Taarifa ya mkuu wa shule ilifanya kila mzazi atokwe na jasho. Shule inatakiwa itafute vyanzo ili kulipa walinzi, wapishi, walimu wa ziada (volunteers), repair ya vyoo, kujenga fence n.k. Bila mkuu wa shule kuwa mbunifu hamna kitu. Bila wazazi kujiongeza hamna kitu. Ukisikia shule imefaulisha, kuna kazi ya ziada inayofanywa na kamati ya wazazi kwa kushirikiana na shule. Tuache mchezo jamani. Huku kulalamika ni siasa za wivu.
Wewe ni mpumbavu ni hilo tu....unaelewa maana ya neno elimu bure?....kama serikali kupitia Kodi zetu imeshindwa kuleta viti na kuongeza madarasa inataka wananchi ndio wajikamua walete inawezaje kusema inatoa elimu bure?...ebu waulize viongozi wako wakati wanapewa elimu bure walikuwa wanaenda na viti shuleni wakati huo? iweje sasa tuko uchumi wa kati tunalazimisha mwananchi huyu mnyonge atoe elfu 50 ya kiti na elfu 10 ya ujenzi hapo bado michango ya maji mlinzi umeme na pesa za kila wiki za kuandaa mitihani ya majaribio... ushabiki kwenye elimu mtaliangamiza taifa tangazeni elimu ya kuchangia ili wazazi wajipqnge mapema kuliko kutangaza elimu bure wakati mnawavizia wazazi mashuleni wakileta watoto wanakutana na michango mingi