Rais Yoweri Museven: Wabunge wa Bunge la Ulaya wapunguze ujuaji

Rais Yoweri Museven: Wabunge wa Bunge la Ulaya wapunguze ujuaji

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amelikosoa bunge la Umoja wa Ulaya baada ya kuitaka serikali yake kusitisha mradi wa kimkakati wa bomba la mafuta na nchi jirani ya Tanzania.

Wiki mbili zilizopita wabunge wa Umoja wa Ulaya walipitisha azimio la onyo la ukiukwaji wa haki za binadamu na hatari ya kijamii na kimazingira inayoletwa na mradi huo.

"Baadhi ya wabunge hawa wa EU hawawezi kuvumilia na wana makosa kiasi kwamba wanafikiri wanajua kila kitu lakini wanapaswa kutulia," Bw Museveni alisema katika mkutano wa kila mwaka wa kilele wa kimataifa wa mafuta na gesi wa Uganda



Aliongeza: "Huu ndio uwanja wa vita usio sahihi kwao. Natumai washirika wetu wataungana nasi kwa uthabiti na kuwashauri. Kwetu sisi, tunaendelea na programu yetu."

Makundi ya kutetea haki za binadamu yanasema baadhi ya watu 100,000 wako katika hatari ya kuhamishwa makazi yao na wamewataka wakandarasi, Kampuni ya Total Energies ya Ufaransa na Shirika la Mafuta la China National Offshore Oil Corporation, kusitisha mradi wa $10bn (Tsh. Bilioni 23) hadi wapate njia mbadala.

Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki utaenea kilomita 1,443 (maili 896) kutoka Ziwa Albert magharibi mwa Uganda hadi bandari ya Tanga ya Tanzania kwenye Bahari ya Hindi.
 
Kwa hili nipo pamoja na mseven.. Wao walipo tutawala Kwa miongo kadhaa huku wamasai wa Tanzania wakitengwa na wenzao wa Kenya hawakujua kama kuna haki za binadamu
 
Kwa hili nipo pamoja na mseven.. Wao walipo tutawala Kwa miongo kadhaa huku wamasai wa Tanzania wakitengwa na wenzao wa Kenya hawakujua kama kuna haki za binadamu
Haki za binadamu kwa definition ya EU Ni wanaume kwa wanaume waruhusiwe kufirana.
 
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amelikosoa bunge la Umoja wa Ulaya baada ya kuitaka serikali yake kusitisha mradi wa kimkakati wa bomba la mafuta na nchi jirani ya Tanzania.

Wiki mbili zilizopita wabunge wa Umoja wa Ulaya walipitisha azimio la onyo la ukiukwaji wa haki za binadamu na hatari ya kijamii na kimazingira inayoletwa na mradi huo.

"Baadhi ya wabunge hawa wa EU hawawezi kuvumilia na wana makosa kiasi kwamba wanafikiri wanajua kila kitu lakini wanapaswa kutulia," Bw Museveni alisema katika mkutano wa kila mwaka wa kilele wa kimataifa wa mafuta na gesi wa Uganda



Aliongeza: "Huu ndio uwanja wa vita usio sahihi kwao. Natumai washirika wetu wataungana nasi kwa uthabiti na kuwashauri. Kwetu sisi, tunaendelea na programu yetu."

Makundi ya kutetea haki za binadamu yanasema baadhi ya watu 100,000 wako katika hatari ya kuhamishwa makazi yao na wamewataka wakandarasi, Kampuni ya Total Energies ya Ufaransa na Shirika la Mafuta la China National Offshore Oil Corporation, kusitisha mradi wa $10bn (Tsh. Bilioni 23) hadi wapate njia mbadala.

Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki utaenea kilomita 1,443 (maili 896) kutoka Ziwa Albert magharibi mwa Uganda hadi bandari ya Tanga ya Tanzania kwenye Bahari ya Hindi.

Kwani Loliondo waliondolewa wananchi wangapi?
 
Yule mtikisa wezere hajaenda kweli kusaga kunguni huko kwa mabwana zake
 
Kwa hili nipo pamoja na mseven.. Wao walipo tutawala Kwa miongo kadhaa huku wamasai wa Tanzania wakitengwa na wenzao wa Kenya hawakujua kama kuna haki za binadamu
Kwa akili nyepesi ni rahisi kukubaliana na Mzee Kaguta. Lakini tujiulize, kwanini mafuta yanachimbwa Ziwa Albert Uganda na kupelekwa Bandarini Tanga?

Jibu la swali hapo juu ni kwamba yanapelekwa Bandarini Tanga ili yakauzwe sehemu mbalimbali duniani. Ni ukitazama kwa makini zaidi utagundua wame target soko la Ulaya. Na hao hao ndio unasema wasiwababaishe. Mkiishamalize kujenga mtawauzia akina nani? Mugabe na wapambe wake waliwafukuza walowezi wa kizungu kwenye mashamba yao, wakayamiliki wao halafu eti baadae wanatafuta masoko Ulaya kwa wazungu hao hao waliowafukuza. Waulize kama waliyapata.
 
Awamu ya tano wasingethubutu kuja na hizi ngonjera zao.
Tena magu angezitisha kbsa baadh ya mrad ya kimkakati ili kufinance bomba Hilo x[emoji23][emoji23] Kam wazungu wangezinguaa

Alfu mbn naona figure ndogo tu billion 23 au imo kwa dola

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kumbe Mu7 mtu mbad ! Mzee anamipasho mikali kawapiga spana kali sana mabeberu ..
 
Back
Top Bottom