Raja Casablanca kala chuma tatu usiku

Yanga anachipukia!!?
 
Kufungwa sio ajabu kwenye mpira haswa ikiwa ni ligi kumbuka Argentina na Saudi Arabia juzi tu. Yanga kafungwa na Ihefu na mifano mingi sana
 
wasihadaike na haya matokeo hawa ni watu wa mipango sana
 
Kama unasema Far Rabat ni timu inayochipukia utakuwa mpira haujui wewe. Yaani kwenye ma giants wasitajwe timu zilizobeba makombe, wataje timu zinazoishia robo fainali. Angalia record ya Far Rabat halafu niambie Simba imeifikia hiyo record?
 
Makolo wanaanza kuchanganyikiwa chuma icho apo wydad casablanca lazima mueleze mlifata nini robo fainali ..achaneni na uyo raja alie wanyoosha home and away ..
 
yanga sasa wamejifunza hakuma haja ya kupiga maburineti mochwari magoli tano ya nini sasa kwa wale viguru ihefu
 
Kufungwa sio ajabu kwenye mpira haswa ikiwa ni ligi kumbuka Argentina na Saudi Arabia juzi tu. Yanga kafungwa na Ihefu na mifano mingi sana
Yanga amefungwa na anatetea ubingwa, Argentina alifungwa na alichukua ubingwa ila hawa Raja wanapambana waingie top four mpaka sasa wanashika nafasi ya tano.
N B sikumbuki kama Yanga na Argentina walifungwa magoli mengi hivyo. (Magoli matatu kwa sifuri)
 
Nyie si mnaaminisha watu kwamba Waydad hawezi kufungwa na sisi. Sasa hii ni nini kama sio matokeo ya mpira?
 
Shirikisho ni mashindano ya timu za kati. Ni kama kule ulaya europa ni kwa ajili ya akina sevilla, lakini kwa Man u au juventus ni kufeli. Kwa hiyo kama unajiona ni mkubwa kushiriki shirikisho ni kufeli kwa malengo. Kwani Real Madrid bingwa wa uefa hafungwi pale la liga na akina real betis? Je hiyo inafanya eufa champions ifanane ubora na europa?
 
iyo ndocharacter za timu kubwa madrid mwenyewe jana kala 3 santiago,yanga kashinda moja kwa taabu...ni kawaida kwa mabingwa ku struggle kwa timu za nyumbani
 
Na Ihefu iliyoinyanyasa Yanga imefumuliwa 5-1 na Simba

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Hivi kwa akili yako kuna timu ambayo haifungwi kwenye ligi yoyote duniani? Argentina alifungwa na Saudia, Man City mwenyewe alifungwa na Nottigam Forest, Madrid kafungwa jana, Bayern anaufungwa n.k sembuse Raja?
Vipers, Al Hilal wote waliifunga Yanga na wanafungwa
 

Hata Real mbabe wa UEFA majuz kala chuma tatu na Villarreal Kwahiyo hapa napo tusemaje mzee
 
Ngoja waje wapindue maelezo
Mechi ya Ihefu ilikuwa Yanga ifunge ifikishe unbeaten 50 Kisha party iangushwe uwanjani zigawiwe keki 50 Kila mwanambeya ambae hajawahi kula keki apate ladha adimu.

Mikia waliambiwa kuhusu hii sherehe ya Yanga wakawahi mbeya na waganga 200 kutoka Tanga, Kongo, Nigeria, Kigoma, Pemba na Sumbawanga wakaroga uwanja walivyoweza bilioni mbili ikatoka kidogo wamfilisi Mo.

Muda mchache kabla ya mechi Simba wakagawa bahasha wakahonga wahusika wa soka mechi ikahamishiwa uwanja walioroga na Yanga hawakuona goli wakafungwa sherehe ikafeli mikia wakaruka ruka na kukanyagana, Yanga tukajipanga Tena tunahesabu unbeaten 100 from that match na Ihefu. Zimefika ngapi Sasa?

Simba imebaki jina tu ni debe tupu linavuma hilooo!!
 
Yanga anachipukia!!?
Kwenye michuano ya CAFCL na CAFCC ni kweli kabisa Yanga ana chipukia, na ndiomaana licha ya kushinda kombe mara 28 idadi ambayo ni nyingi kuliko ile ya Simba Sc, mpaka leo hii hajawahi hata kufika robo fainali CAFCL baada ya miaka 20 kupita.

Kwenye michuano ya kimataifa, Yanga ndio kwanza inachipukia.
 
Kwenye hizo takwimu zako za Rabaf nilitegemea nikute moja tu (hiyo ya kuchukua kombe miaka 40 iliyopita), kama ambavyo mmekuwa mkiidaj Simba Sc ilete kombe ndio ieleweke, ila hapo naona mbwembwe nyingi tu za kuonyesha hatua ambazo walikuwa walifikia wanaposhiriki (ambazo kwa Simba Sc hamtaki zitambulike kama achievements) [emoji1]

Giants wa Morocco ni wazee wa Casablanca tu, huyu Rabat ni ana chipukia baada ya kupotea kwa muda mrefu sana. Ni sawa na mtu alazimishe kuwa kwa sasa Enyimba ni Giant wa Nigeria kutokana na makombe aliyowahi kubeba huko 90's.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…