Raja Casablanca wakejeli graphics za Simba

Zaidi sana wametusaidia kuitangaza Serengeti na Mlima Kilimanjaro...
Hizi ndiyo njia smart za kutangaza utalii, halafu siku ya game, watazamaji wanakumbushwa "Visit Tanzania". Simba kweli wanaliweka taifa mbele!
 
Nitawaachia wenyewe mtafute Kunta Kinte ni nani ila nitakwambia kwa nini yule mtu ni wa kijani. Yule mpayukaji ni wa kijani kutaka kuonyesha kuwa graphics za Simba ni cheap na za kizamani, kwamba hazijafanywa vizuri.
I think umeelewa tofauti: Kwa wale wajuzi wa historia watakubaliana na mimi kuwa Kunta Kinte ni mtu anayeheshimika sana katika harakati kupinga na kukataa Utumwa. Huyu Jamaa ni Shujaa. Hata katika movie zote zenye Character yake "Kinta Kunte" mara kwa mara huonekana ni Shujaa.

Matumizi ya Rangi ya Kijani, Ni rangi yao ya Utambulisho. Kama ilivyo kwa Simba(Red), Yanga(Yellow and Green).

So yule jamaa wa Kijani ni ishara ya kuonesha hii inazungumzwa na wao(Raja 💚)
 
Sawa. Namfahamu Kunta Kinte vizuri ila kwa case hii huyo Kunta Kinte anayemuongelea ndiyo Simba? Naweza kukubaliana na wewe na idea yako ya kijani kama utambulisho wao. Big up kwa kuupanua mjadala kwa angle tofauti.
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣Kunta Kinte tena,
 
Mboni Posta yao ni nzuri sana wanatutangazia utalii wa nje & ndani, shida ipo wapi? Mimi sijaona ubaya wowote wakitaka hata Kituro tutawapeleka
Matangazo ya Raja aisee Yako poa sana ni tangazo fupi ila linavuta hisia na kuleta furaha nimewapenda sana ningependa Hawa watu wapewe u abalozi wa utalii na mapokezi ya heshima
 
Sawa. Namfahamu Kunta Kinte vizuri ila kwa case hii huyo Kunta Kinte anayemuongelea ndiyo Simba? Naweza kukubaliana na wewe na idea yako ya kijani kama utambulisho wao. Big up kwa kuupanua mjadala kwa angle tofauti.
Naomba nitumie matukio kidogo ili kuonesha ukuu wa jina la Kunta Kinte.

Baada ya kila alichokifanya huyu mwanaume "Kunta Kinte" basi baade kuna kitabu(I think ni Novel inaitwa ROOTS) ilitupa Story nzima ya huyu jamaa.

Baadae wakaleta mfululizo wa movies za "Roots" wengine wamezipa jina la Kunta Kinte kabisa. Basi ndizo zilimpa umaarufu na kuacha vyema kabisa Legacy yake "Kunta Kinte".

Baadae Rappers; Akiwemo Kendrick Lamar, pale walipotaka kuonesha ukuu wa mtu mweusi basi walitumia jina la "Kunta Kinte" Kuonesha ni Exceptional BlackMan(Mtu mweusi wa kipekee). Kendrick anamoja ya hitsong inaitwa "Kunta Kinte"

So, baada ya kutumia sana katika hiphop verses baadae hili jina likaanza kutumika kama Pride ya Africans. Ili kuonesha kumkubali mtu mweusi alinayefanya makubwa basi wanam-refer kama "Kunta Kinte" - The Pride of Africans/Blacks.

So, Kwa ufupi jina la Kunta Kinte ni ishara ya Ukuu wa mtu mweusi/Exceptional Blackmanhood.

I think hapo nimeeleweka.

Niseme kitu kimoja Raja na Simba-hawa ni marafiki sana, pia wanashare marafiki kama TP Mazembe, Al Hilal na Al Ahly.

Oh, Comment imekua ndefu. Haya nitaeleza wakati mwingine.
 
Historia nzuri na sikupingi ulichoandika. Swali langu bado haujalijibu, jamaa yetu wa kijani alilitumia jina hilo la Kunta Kinte kumaanisha nini?

Usihofu, wewe andika kwa urefu tu tulio na interest tupo tutasoma.
 
Kwa Mkapa hatoki mtu. Shujaa Kunta Kinte anakuja kuondoa huo unyonge kama alivyokataa Utumwa.
Ni mtazamo tu baada ya kupitia michango mbali mbali.
 
Kwa Mkapa hatoki mtu. Shujaa Kunta Kinte anakuja kuondoa huo unyonge kama alivyokataa Utumwa.
Ni mtazamo tu baada ya kupitia michango mbali mbali.
🤣🤣🤣🤣🤣Haya yote yasingetokea kama Kunta angekubali jina la Toby…
 
Poster yao kali saaana ila sijaelewa hiyo mistari ya kushoto ina maana gani. Ndiyo maana nasema ni kejeli tu kuonyesha "hivi ndiyo jinsi ya kutengeneza poster sasa"
Broo watu wanaomiliki viwanja tena vya kisasa hawawezi kulingana na Simba aisee
 
Nilichopenda kwenye game hii ya Simba na Raja AC ni mahusiano mapya ya kiushindani yaliyojengeka kati ya timu hizi mbili.

Unaona kabisa huu ni utani wa jadi unaoenda kujengwa. Simba wasiachie hili lipite, utani huu utaisaidia huko mbeleni katika kukuza jina lake Afrika. Ni muhimu hili inabidi lifanyike sambamba na kuwa na kikosi cha viwango. Katika Africa wapinzani wa jadi huwa ni timu zinazocheza ligi moja ya ndani, hii inaweza kuwa aina mpya ya kukuza soka la Afrika.

 
Historia nzuri na sikupingi ulichoandika. Swali langu bado haujalijibu, jamaa yetu wa kijani alilitumia jina hilo la Kunta Kinte kumaanisha nini?

Usihofu, wewe andika kwa urefu tu tulio na interest tupo tutasoma.
kwamba wanakuja kumpiga mtu mweusi na kuiteka himaya yake,ndo maana waliposhinda wamepost tai amekua mfalme ktk serengeti na sio simba
 
hapo tai kawa mfalme,kampindua simba ((mfalme wa pori)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…