Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 22,168
- 39,118
Tuisila Kisinda anapewa pasi na Fiston Mayele hatua chache toka katikati ya uwanja kuelekea lango la Mbeya City. Anakokota mpira kuelekea pembeni huku kila Mtu akiamini lengo lake ni kupiga krosi. Ghafla anakatisha kuingia kati na kuamua kushoot na mpira unampita kipa na kuingia wavuni.
Mshika kibendera aliyekuwa pembeni sambamba na mchezaji wa mwisho wa pili (Second last defender) wa Mbeya City anarudi katikati kuashiria goli ni halali turudi tuanze mpira. Awali Kayoko anaonekana kukubaliana naye kwa kuonyesha mkono wake wa kulia mpira upelekwe kati, lakini ghafla anabadili maamuzi na kunyoosha mkono juu kuashiria kuna mushikeri kwenye uhalali wa bao hilo, anamnyooshea mkono Mayele na kumwambia wewe uliingilia mchezo ukiwa offside.
Hili ni somo muhimu sana kwetu. Kumbe mwamuzi wa kati anaweza kumpinga mshika kibendera kuhusu offside na akaamua vinginevyo ikaonekana hakuna shida.
Waamuzi wengine wajifunze kwa Kayoko, si kila maamuzi ya offside yategemee mshika kibendera, kama unaona anazingua badili maamuzi maana mwisho wa siku utalaumiwa wewe mwamuzi wa kati.
Asante KAYOKO kwa somo zuri.
Mshika kibendera aliyekuwa pembeni sambamba na mchezaji wa mwisho wa pili (Second last defender) wa Mbeya City anarudi katikati kuashiria goli ni halali turudi tuanze mpira. Awali Kayoko anaonekana kukubaliana naye kwa kuonyesha mkono wake wa kulia mpira upelekwe kati, lakini ghafla anabadili maamuzi na kunyoosha mkono juu kuashiria kuna mushikeri kwenye uhalali wa bao hilo, anamnyooshea mkono Mayele na kumwambia wewe uliingilia mchezo ukiwa offside.
Hili ni somo muhimu sana kwetu. Kumbe mwamuzi wa kati anaweza kumpinga mshika kibendera kuhusu offside na akaamua vinginevyo ikaonekana hakuna shida.
Waamuzi wengine wajifunze kwa Kayoko, si kila maamuzi ya offside yategemee mshika kibendera, kama unaona anazingua badili maamuzi maana mwisho wa siku utalaumiwa wewe mwamuzi wa kati.
Asante KAYOKO kwa somo zuri.