Ramadhan Special Thread

Umesomeka jamaa
 
Reactions: PNC
Cha kuwakumbusha ndugu zanguni, mfungo wa ramadhani sio adhabu ila ni nafasi mola wetu mlezi anatupa ili tujikurubishe kwake na kumuomba msamaha na kuomba rehma na kuwekwa mbali na moto wa jehanamu,

Funga inaendana na SALA, kama Husali ndugu zangu basi hakika wewe unashinda na njaa wala hupati thawabu zozote zaidi ya kujiongezea mzigo wa dhambi, nasisitiza tena FUNGA inaenda sambamba na SALA 5.

Sala ndio sehemu pekee ya mja kuongea na Mola wake, tuache uvivu kipindi hiki, tuamkeni usiku na kujipendekeza kwa mola wetu, mwezi ni mmoja tu, hivyo tuutumieni ipasavyo, omba chochote kwa Mola wako, mwambie chochote anakusikia.

Tukatazane mabaya na tuamrishane yaliyo mema.
 
Mkuu sala haiondoi funga

Hizo ni ibada mbili tofauti

Ila inashauriwa ukifunga uswali maana utapata thawabu nyingi sana

Ila ukifunga na usiswali funga yako inakubalika kama kawaida cha muhimu uwe umetia nia na umejizuia na yale yote yanayotengua funga.
 
Pia nawahusia mama zetu/dada zetu na mabinti zetu wazingatie sana suala la stara maana stara kwa wanawake wengi wanaona ni mtihani mzito sana wamepewa

Wanawake wengi ndio chanzo kikubwa cha kutengua funga za watu kwa kutozingatia uvaaji wa kiheshima unaofata misingi ya dini yetu ya kiislamu
 

SWALI: Ipi hukumu ya mwenye kufunga Ramadhwaan bila ya Swalaah au akaswali katika Ramadhwaan na haswali (miezi) mingine?

JIBU: Ama Swawm yake, Zakaah yake, Hajj yake au yasiyokuwa hayo katika ´amali zake bila ya Swalaah hazitomfaa. Kwa kuwa la sahihi ni kuwa mwenye kuacha Swalaah ni kafiri, kutokana na dalili maalumu, miongoni mwazo ni Hadiyth: "Ahadi iliyoko baina yetu na wao (makafiri) ni Swalaah, mwenye kuiacha amekufuru."

Na Hadiyth: "Baina ya mtu na kafiri na shirki ni kuacha Swalaah."

Hadiyth hizi mbili ni sahihi na dalili zake ziko wazi.
 
Hadith of Prophet (peace and blessings of Allah be upon him)
The one who disdains the prayers will receive fifteen punishments from Allah. Six punishments in this lifetime, three while dying , three in the grave and three on the Day of Judgement.
The six punishments in this life:
1. Allah takes away blessings from his age (makes his life misfortunate)
2.Allah does not accept his plea (du'a)
3.Allah erases the features of good people from his face.
4.He will be detested by all creatures on earth.
5.Allah does not reward him for his good deeds (no thawab)
6.He will not be included in the du'a (supplications) of good people.
The three punishments while dying:
1. He dies humiliated.
2. He dies hungry.
3. He dies thirsty. Even if he drinks the water of all the seas he will still be thirsty.
The three punishments in the grave:
1. Allah tightens his grave until his chest ribs come over each other.
2. Allah pours on him fire with embers.
3. Allah sets on him a snake called "the brave", "the bold" which hits him from morning until afternoon for leaving the Fajr (early morning) prayer, from the afternoon until Asr (late afternoon) for leaving the Dhuhr (noon) prayer and so on. With each strike he sinks 70 yards under the ground.
The three punishments on the day of judgement:
1. Allah sends who would accompany him to hell pulling him on the face.
2. Allah gives him an angry look that makes the flesh of his face fall down.
3. Allah judges him strictly and orders him to be thrown in hell.
 
Mkuu hili suala limekuwa likileta mkanganyiko mkubwa sana baina ya wanazuoni

Wapo wanaodai ukifunga na usiposwali ,funga yako itakuwa ni batili na wana hoja zao kuhusu hilo

Pia wapo wanaodai ukifunga na usiposwali funga yako inakubalika kama kawaida na hawa pia wana hoja zao mf wa moja za hoja zao.

Hawa wanadai funga na swala ni nguzo mbili tofauti katika zile nguzo tano za uislamu

1)Kutoa shahada

2) kuswali

3)kutoa zakka

4)kufunga mwezi mtukufu wa ramadan na

5)kuhijji makka kwa wenye uwezo
 
Hadithi ndio hizo nimekupa, kazi kwako sasa kuzipitia kwa utulivu, "Tofauti yenu na wao ni SALAH"
pia Allah (s.w)ameweka wazi hukumu kua asiyeswali basi amemfutia amali zake zooote duniani na akhera vipi tena hao wanazuoni waseme funga inakubalika na wakati amali zimeshafutwa??? kwa hiyo asiyeswali hata awe mwema kiasi gani hana anachoandikiwa mpaka atubu na kuanza kusali,

"Hakuna m'bora kati yenu isipokua MCHA MUNGU" Qur'an.

Kila la kheir.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…