Ramadhani Brothers kukutana na rungu kodi zaidi ya 180M kwenye 600M waliyoshinda

Ebhana ahsante
 
Wengi nnaona wanapondea kodi kwa kigezo haifanyi kazi inayokusudiwa tu.


Ni wakati sasa serikali iwe bunifu kuongeza kusifia miradi iliyofanywa na serikali na kuboresha huduma zinazotolewa na serikali ili kila mmoja aone anaumiliki na kuujenga uchumi wa nchi yake mwenyewe.

Ona kama enzi za Magu, wakijenga reli inatangazwa hadi hadi basi, wakileta ndege ni sherehe ya kitaifa kabisa😅..... akikamatwa fisadi basi kila mtu atajua jinsi takukuru na usalama walivyo active. Aamini unavyoamini lakini nakuambia haya mambo ya hii aya ni muhimu sana kujenga morali ya kitaifa watu walipe kodi.

Japan na Ujerumani mtu akilipa kodi anajichukulia kama yupo vitani anaipigania nchi yake kabisa. Hiyo haiji hivihivi inahitaji ukweli kiasi uliodhibitiwa na propaganda ikibidi
Uhakika bro
Mshauri binafsi wa kwenye sredi kwan nn🤨
 
Kuna nchi kusini mwa Africa kodi zinalipwa ,viongozi wanafuga vitambi uchwara ndani ya magari ya mwingereza huku wananchi wakilia gizani kama tola , ukiwaona ndani ya viwalo unaweza sema wapo seriously 😭😭.
 
Kwani bado wana mpango wa kurudi bongo, watakuwa wapumbavu, wakae huko ndio kwenye chaneli za pesa.
 
Hakuna kitu inauma kama kulipishwa kodi kandamizi halafu ikifika mwisho wa mwaka ukabahatika kusoma au kusikiliza ripoti za mkaguzi wa serikali(CAG)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…