Nilichokielewa hapo kwenye hiyo video ni kwamba, Chedi Benz.
1/Anajiamini.
2/Anajitambua.
3/Ana matatizo.
4/Anaomba msaada.
5/Anatupenda sote
USHAURI wangu kwetu sisi sote...
-Tumuelewe
-Tumsaidie
-Tumwombee.
-Tumuunge mkono.
-Tumpende
*NOTE.
1/Ni jambo la kawaida kabisa kwa mtumiaji wa madawa ya kulevya kukana kuwa anatumia au anaendelea kutumia madawa(Hivyo tusishangae hilo!)
2/Ni jambo la kawaida kwa mtumiaji wa madawa ya kulevya kutibiwa na kupona lakini baada ya muda kurudia tena kutumia hayo madawa. Zaidi ya 60% huwa hivyo.(Hivyo tusishangae hilo!)
3/Madawa ya Kulevya humuathiri mtu KIAKILI, KIMWILI na KIJAMII. Hivyo tiba yake huhitaji mchanganyiko wa mambo mengi sana na huwa ni mchakato wa muda mrefu(Hivyo kila mbinu zitumike kumsaidia muathirika wa madawa ya kulevya).
4/Kumkatia tamaa muathirika wa madawa ya kulevya ni sawa na kumpa tiketi ya kumuangamiza zaidi. (Hivyo tusikate tamaa kabisa)
5/Mtu aliyeathirika na Madawa ya kulevya anaweza kutibiwa kwa namna mbali mbali na kupona kabisa japokuwa inaweza kuchukua muda na kutokuonyesha matumaini mazuri kwenye hatua za mwanzoni (Hivyo tukazane zaidi na zaidi kuwasaidia kisaikologia, kijamii na kimatibabu)