BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Imetolewa mara ya mwisho: 21.10.2008 0004 EAT
• Rasilimali zilizopo zinavyoweza kulikomboa Taifa
Na Glory Mhiliwa
Majira
BALOZI wa Marekani hapa nchini Marc Green na mwaharakati wa haki za Wamarekani weusi nchini Marekani Mch Jesse Jackson ni miongoni kati ya watu kutoka Bara la Ulaya kuhoji Tanzania kuwa masikini.
BALOZI Marc Green anasema kuwa Tanzania inakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha kuwa inasonga mbele kimaendeleo kwa kutumia rasilimali zake ipasavyo.
Anasema kuwa Tanzania ni mojawapo kati ya nchi zilizo nyuma kimaendeleo hata orodha ya nchi masikini duniani inathibitisha hilo.
'Tanzania ni nchi ya 159 ya kimasikini kati ya nchi 177 orodha hii inaonesha kuwa Tanzania ipo mwisho kabisa zinahitajika juhudi katika kuondoka mkiani na kufikia kileleni," alieleza Balozi Green.
Balozi Green anasema kuwa kama Tanzania inampango madhubuti wa kuondokana na umasikini kuna haja kwa Tanzania kutumia ipasavyo rasilimali zake ili kuliwezesha Taifa kuondokana na umasikini.
Anatanabaisha kuwa Tanzania ni nchi iliyobarikiwa kwa kuwa na udongo mzuri unaofaa kwa kilimo na wenye rutuba nzuri na mvua zinazonyesha kwa wakati.
"Kilimo chenyewe kinaweza kulipatia Taifa hili maendeleo ukiachilia mbali sekta nyinginezo kama sekta ya madini ama viwanda, udongo wa Tanzania bado unarutuba inayofaa kwa kustawisha mazao tofauti na nchi nyingine ambazo udongo wake haufai kwa kilimo," anasema Balozi Green.
Anasema kuwa ikiwa kilimo kitapewa kipaumbele zaidi kinaweza kutosheleza mahitaji ya ndani na sanjari na soko la nje hususani kwa baadhi ya mazao kama vile zao la kahawa ambalo likiboreshwa litaweza kuongeza kasi ya mauzo kwa nje ya nchi.
Akizungumzia sekta nyingine ambazo nazo zikitumika ipasavyo kwa maslahi ya Taifa Balozi Green anasema kuwa sekta ya madini ni sekta ambayo inaouwezo wa kuifikisha mbali Tanzania lakini kama sekta hiyo itatumika kama kiongozi wa maendeleo ya kiuchumi.
Anasema kuwa ni muhimu kwa manufaa ya vizazi vijavyo mikakati endelevu ya kukuza uchumi wa Tanzania ikaanza kuchukua sura mpya kuanzia sasa hivi.
Naye Mwanaharakati wa haki za Wamarekani weusi Mchungaji Jesse Jackson katika kipindi cha mkutano wa Leon Sullivan ambapo alishiriki ikiwa ni mara yake ya kwanza kutembelea Tanzania aliungana na Balozi Green katika kuitaka Tanzania kutumia rasilimali zake ipasavyo ili kuweza kuondokana na umasikini.
Mchungaji Jesse anasema kuwa kupitia mkutano wa nane wa Leon Sullivan ameweza kutembelea eneo la maajabu ya nane ya Dunia ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na kubaini kuwa Tanzania ina rasilimali nyingi za kuiwezesha kuondokana na umasikini.
Anasema kuwa Ngorongoro ni mahali pekee duniani ambapo panaonesha historia ya binadamu wa kale waliokuwa wakiishi kwenye bustani moja wanyama binadamu bila ya kudhuriana.
"Dunia nzima hakuna mahali ambapo utakuta binadamu na wanyama wanaishi kwa pamoja bila ya kudhuriana tena wanachangia maji kwa pamoja hii inatukumbusha historia ya kwenye biblia ya bustani ya Edeni, anasema Mchungaji Jesse.
Anasema Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) ndiyo Eden hai iliyopo duniani na hakuna mahala pengine inapatikana zaidi ya Tanzania ingawa haifahamiki kama ilivyo na umuhimu kwa Dunia nzima.
Alieleza kwake kuushangazwa na Wamasai kuishi kwa pamoja na wanyamapori, mifugo ya Wamasai kula kwenye malisho ya pamoja na wanyamapori bila ya kudhuriana wakati maeneo mengine binadamu na wanyamapori ni maadui.
Aliitaka Serikali kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara katika hifadhi zote kama ilivyo kwa NCAA hali aliyoelezea kuwa itachangia katika kuongeza kiwango cha watalii kwa mwaka wanaotembelea vivutio vya Tanzania.
"Hiki ni kigezo tosha kwa kuwaleta watalii wengi kuja hapa Tanzania kutembelea hifadhi hii ambayo yenyewe inaouwezo wa kuendesha uchumi wa Taifa hili," Mchungaji Jackson anaelezea maoni yake.
Alieleza kuwa Tanzania inatakiwa kujitangaza zaidi ili mataifa kutoka nchi zilizoendelea kama Marekani na China kufahamu vivutio vilivyopo Tanzania hali itakayosababisha kuongezeka kwa watalii watakaokuwa wakitembelea hifadhi za hapa nchini.
Hata hivyo Mchungaji Jesse alisema kuwa Tanzania inajivunia kuwa na vivutio vingi vya wanyama kuliko nchi nyingine yoyote Barani Afrika.
Anasema kuwa kupitia rasilimali wanyama Tanzania kimapato inao uwezo mkubwa wa kusonga mbele zaidi kiuchumi kupitia mapato ya watalii wanaotembelea hifadhi hizo.
"Hifadhi za wanyama Afrika zipo nyingi zikitumika ipasavyo zenyewe zinatosha kabisa kuliondoa bara la Afrika katika lindi la umasikini lakini kama vitatangazwa na nchi zilizoendelea kuvitambua," anasema.
Hata hivyo alisema kuwa nchi yake ya Marekani kwa mujibu wa Kaimu Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Bw Benard Murunya ndiyo inayoongoza kwa raia wake kutembelea hifadhi hiyo.
• Rasilimali zilizopo zinavyoweza kulikomboa Taifa
Na Glory Mhiliwa
Majira
BALOZI wa Marekani hapa nchini Marc Green na mwaharakati wa haki za Wamarekani weusi nchini Marekani Mch Jesse Jackson ni miongoni kati ya watu kutoka Bara la Ulaya kuhoji Tanzania kuwa masikini.
BALOZI Marc Green anasema kuwa Tanzania inakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha kuwa inasonga mbele kimaendeleo kwa kutumia rasilimali zake ipasavyo.
Anasema kuwa Tanzania ni mojawapo kati ya nchi zilizo nyuma kimaendeleo hata orodha ya nchi masikini duniani inathibitisha hilo.
'Tanzania ni nchi ya 159 ya kimasikini kati ya nchi 177 orodha hii inaonesha kuwa Tanzania ipo mwisho kabisa zinahitajika juhudi katika kuondoka mkiani na kufikia kileleni," alieleza Balozi Green.
Balozi Green anasema kuwa kama Tanzania inampango madhubuti wa kuondokana na umasikini kuna haja kwa Tanzania kutumia ipasavyo rasilimali zake ili kuliwezesha Taifa kuondokana na umasikini.
Anatanabaisha kuwa Tanzania ni nchi iliyobarikiwa kwa kuwa na udongo mzuri unaofaa kwa kilimo na wenye rutuba nzuri na mvua zinazonyesha kwa wakati.
"Kilimo chenyewe kinaweza kulipatia Taifa hili maendeleo ukiachilia mbali sekta nyinginezo kama sekta ya madini ama viwanda, udongo wa Tanzania bado unarutuba inayofaa kwa kustawisha mazao tofauti na nchi nyingine ambazo udongo wake haufai kwa kilimo," anasema Balozi Green.
Anasema kuwa ikiwa kilimo kitapewa kipaumbele zaidi kinaweza kutosheleza mahitaji ya ndani na sanjari na soko la nje hususani kwa baadhi ya mazao kama vile zao la kahawa ambalo likiboreshwa litaweza kuongeza kasi ya mauzo kwa nje ya nchi.
Akizungumzia sekta nyingine ambazo nazo zikitumika ipasavyo kwa maslahi ya Taifa Balozi Green anasema kuwa sekta ya madini ni sekta ambayo inaouwezo wa kuifikisha mbali Tanzania lakini kama sekta hiyo itatumika kama kiongozi wa maendeleo ya kiuchumi.
Anasema kuwa ni muhimu kwa manufaa ya vizazi vijavyo mikakati endelevu ya kukuza uchumi wa Tanzania ikaanza kuchukua sura mpya kuanzia sasa hivi.
Naye Mwanaharakati wa haki za Wamarekani weusi Mchungaji Jesse Jackson katika kipindi cha mkutano wa Leon Sullivan ambapo alishiriki ikiwa ni mara yake ya kwanza kutembelea Tanzania aliungana na Balozi Green katika kuitaka Tanzania kutumia rasilimali zake ipasavyo ili kuweza kuondokana na umasikini.
Mchungaji Jesse anasema kuwa kupitia mkutano wa nane wa Leon Sullivan ameweza kutembelea eneo la maajabu ya nane ya Dunia ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na kubaini kuwa Tanzania ina rasilimali nyingi za kuiwezesha kuondokana na umasikini.
Anasema kuwa Ngorongoro ni mahali pekee duniani ambapo panaonesha historia ya binadamu wa kale waliokuwa wakiishi kwenye bustani moja wanyama binadamu bila ya kudhuriana.
"Dunia nzima hakuna mahali ambapo utakuta binadamu na wanyama wanaishi kwa pamoja bila ya kudhuriana tena wanachangia maji kwa pamoja hii inatukumbusha historia ya kwenye biblia ya bustani ya Edeni, anasema Mchungaji Jesse.
Anasema Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) ndiyo Eden hai iliyopo duniani na hakuna mahala pengine inapatikana zaidi ya Tanzania ingawa haifahamiki kama ilivyo na umuhimu kwa Dunia nzima.
Alieleza kwake kuushangazwa na Wamasai kuishi kwa pamoja na wanyamapori, mifugo ya Wamasai kula kwenye malisho ya pamoja na wanyamapori bila ya kudhuriana wakati maeneo mengine binadamu na wanyamapori ni maadui.
Aliitaka Serikali kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara katika hifadhi zote kama ilivyo kwa NCAA hali aliyoelezea kuwa itachangia katika kuongeza kiwango cha watalii kwa mwaka wanaotembelea vivutio vya Tanzania.
"Hiki ni kigezo tosha kwa kuwaleta watalii wengi kuja hapa Tanzania kutembelea hifadhi hii ambayo yenyewe inaouwezo wa kuendesha uchumi wa Taifa hili," Mchungaji Jackson anaelezea maoni yake.
Alieleza kuwa Tanzania inatakiwa kujitangaza zaidi ili mataifa kutoka nchi zilizoendelea kama Marekani na China kufahamu vivutio vilivyopo Tanzania hali itakayosababisha kuongezeka kwa watalii watakaokuwa wakitembelea hifadhi za hapa nchini.
Hata hivyo Mchungaji Jesse alisema kuwa Tanzania inajivunia kuwa na vivutio vingi vya wanyama kuliko nchi nyingine yoyote Barani Afrika.
Anasema kuwa kupitia rasilimali wanyama Tanzania kimapato inao uwezo mkubwa wa kusonga mbele zaidi kiuchumi kupitia mapato ya watalii wanaotembelea hifadhi hizo.
"Hifadhi za wanyama Afrika zipo nyingi zikitumika ipasavyo zenyewe zinatosha kabisa kuliondoa bara la Afrika katika lindi la umasikini lakini kama vitatangazwa na nchi zilizoendelea kuvitambua," anasema.
Hata hivyo alisema kuwa nchi yake ya Marekani kwa mujibu wa Kaimu Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Bw Benard Murunya ndiyo inayoongoza kwa raia wake kutembelea hifadhi hiyo.