Rasimu hii ya katiba inalenga kulinda maovu ya maraisi wastaafu na wajao tusiwawajibishe!

Rasimu hii ya katiba inalenga kulinda maovu ya maraisi wastaafu na wajao tusiwawajibishe!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184



Sasa nimethibitisha ya kuwa katiba iliyopo ilisiginwa na kutotumika katika kuibadilisha katiba iliyopo kwa sababu ya kumlinda Raisi ambaye atajengewa mazingira ya kila chaguzi zetu atokane na chama tawala cha CCM.


Katika Katiba iliyopo utaratibu wa kuibadilisha katika kwa masuala ya muungano na haya mapendekezo ya tume ya warioba yote ni masuala ya muungano ni shuruti theluthi mbili ya wabunge wote wa bara na theluthi mbili ya wabunge wote wa visiwani waafiki. Utaratibu huo haukufuatwa kwa sababu hakuna mwafaka ndani ya Bunge hili kuhusiana na khoja ya siri ya JK na wenzie ya kumjenga na kumlinda Raisi ajaye ambaye kama rasimu hii itapita lazima ataendelea kutoka ccm na wala siyo vinginevyo.



Swali la kujiuliza JK, Warioba na wapambe wao wanakhofu ya nini baada ya 2015? Ni dhambi zipi wametutendea hadi wajenge mazingira ya kukaza uzi wa kutudhulumu haki zetu za wapigakura hata kuhoji uhalali wa matokeo ya Uraisi na kulazimisha kuyakasimu kwa wagombea kinyume cha katiba hiyohiyo ambayo inasema mamlaka ya dola yanatokana na wananchi wenyewe? Kama wana madhambi ushauri wangu ni watubu tutawasamehe bali wasitegemee kwa kuminya haki za raia ndiyo ufumbuzi wa kudumu wa kulindana utamaduni ambao utapamba moto kama hii rasimu itapita kama ilivyo………..



Kwa JK na wenzie masilahi ya taifa ni kulinda ulaji wao kupitia Raisi ajaye ambaye wathakikisha ni kutoka kwenye chama chao na mazingira anayojengewa ni kama ifuatavyo:



Kuweka mazingira ya kuhakikisha kuwa haki ambazo raia wamepewa zinaporwa papo kwa hapo kwa kujenga mazingira sheria zitaundwa kupora haki hizo:-
1) Ipo ibara inayosema vijana wanayohaki ya kushiriki kwenye Nyanja zote lakini inapokuja uraisi wamewekewa ukomo lazima wazidi miaka 40 na hivyo kuleta ukinzani kwenye katiba hiyo hiyo.

2) Raisi anapoingia madarakani anahitaji zaidi ya asilimia hamsini tena ya wapigakura wote lakini kumng’oa inahitajika mapendekezo ya asilimia 75 ya wabunge wote ambao baadhi ya wao ni wateule wake!

3) Raisi hawezi kushitakiwa kwa makosa ya jinai ambayo ameyatenda akiwa madarakani hadi yawe yameidhinishwa na Bunge ambalo ili lifanye hivyo basi robo tatu yao wawe wamekubali ashitakiwe! Huyu Raisi ni Mungu au ni mwanadamu ambaye anapaswa kuwajibishwa kama mwanadamu mwingine? Ikumbukwe katiba iliyopo ni theluthi mbili tu zinahitajika kumwondoa Raisi madarakani na haya mapendekezo yanalirudisha taifa nyuma kwa kuweka masharti magumu ya kumwajibisha Raisi mkorofi kupitia Bunge.

4) Zipo aya zinasema Raisi hana mamlaka ya kuingilia uteuzi na udhibiti wa nidhamu wa taasisi nynginezo lakini wajibu aliopewa Raisi ni kuwaingilia na hivyo kuleta migongano ndani ya katiba hiyohiyo. Yaelekea inapokuja Raisi migongano imeshamiri ili kumfanya awe juu ya sheria.

5) Majaji wakuu ambao siyo sehemu ya Bunge wanapewa kazi za kumdhibiti Raisi kwa kuchunguza tuhuma dhidi yake kazi ambayo ni ya Bunge hivyo kuleta migongano ya mihimili ya serikali ambayo rasimu hiihii imekataza.

6) Majaji wakuu hawahawa ambao hawajachaguliwa na wananchi sasa wanapewa nafasi ya kuwapora wabunge kazi ya kuidhibiti dola na kufanya kazi ya uchunguzi badala ya kufanyakazi ya kuamua kwenye masuala yasiyo ya kisiasa.

7) Mashitaka dhidi ya Raisi yamewekewa muda wa mwaka mmoja bila ya kujali uhalisia wa matukio yenyewe. Khofu ya Tume ya Warioba ni dhahiri kuwa Raisi ajaye hatakuwa na uhalali na ndiyo maana anahitaji kupewa uhalali na katiba.

8) Kwenye kupinga matokeo ya Uraisi, wapigakura hawana sauti na sauti hiyo imekasimiwa kwa wagombea bila ya kutofautisha haki za wapigakura siyo lazima zioane na za wagombea. Mgombea anaweza kununuliwa lakini wapigakura hakuna anayeweza kuwanunua wote. Isitoshe kwenye rasimu hiyohiyo imebainisha ya kuwa wenye mamlaka ya kuongoza dola ni raia wote lakini inapokuja kupinga uraisi wapigakura ambao ndiyo wamemchagua Raisi wameporwa mamlaka ya kuhimili dola ambayo yamo kwenye hii Rasimu. Migongano hii inaonyesha Tume ya Warioba imejaribu sana kuwalinda maraisi wajao wasiwajibike kwa wananchi. Mpigakura akiona kura yake imeibiwa akae kimya tu huku Rasimu inasema raia wanajukumu la kuilinda na kuitetea katiba hii! Raia wataiteteaje katiba kama hawaruhusiwi kwenda mahakamani kudai haki yao kama wapigakura endapo wanaona kura yao haikuhesabiwa kutokana

9) Haki ya rufani imeporwa kwenye kupinga matokeo ya uraisi lakini kwenye Nyanja nyinginezo zote haki ya rufani ipo. Angalau malalamiko dhidi ya chaguzi za uraisi yangelianzia mahakama ya rufaa na kuweka nafasi ya urani kwenye mahakama ya juu badala ya kuanzia mahakama ya juu bila nafasi ya rufani. Haki ya rufani ndiyo moja ya misingi ya kutoa haki sasa ukiiondoa haki hiyo mlalamikaji ataona kweli katendewa haki pale anapokuwa hakubaliani na maamuzi?

10) Muda wa kuwasilisha malalamiko dhidi ya uraisi umeaachiwa sheria za kawaida lakini muda wa kusoma sababu za uamuzi na kuitisha uchaguzi mwingine umetamkwa. Swali hapo kwanini iwe hivyo kama siyo kujenga mazingira magumu ya anayetaka kulalamika kwa kutegemea sheria za bunge badla ya katiba yenyewe na hivyo kutoa mianya ya mahakama hizi zetu zinazoendeshwa kisiasa kutuchagulia viongozi kwa kudai muda umekwisha wa kulalamika? Walalamikaji wangelipewa muda wa wiki mbili tangia matokeo kutangazwa kudai haki yao mbele ya sheria.

11) Viongozi wa kimahakama kwa maana ya majaji wakuu wamepewa nyadhifa nyingi za kiutendaji kama za kuchunguza malalamiko dhidi ya Raisi kazi ambayo siyo yao ikiwemo ya kuteua viongozi wa ngazi za juu wa Tume huru ya uchaguzi kazi ambayo nayo ni ya kiutendaji kwenye Rasimu ambayo inakataza miingiliano ya dola tatu yaani mahakama, serikali na Bunge. Huu mkorogano unalenga kuhakikisha mahakama zinatumika kutuchagulia viongozi ambao watalindana nao. Ikumbukwe chini ya Rasimu hii Raisi ambaye anawateua nao majaji wakuu wamepewa nafasi ya kumpima utendaji wake kazi ambayo ni ya wabunge na hivyo kudhoofisha uwajibikaji wa Raisi kwa wananchi kupitia Bunge lao.

12) Teuzi za Raisi alizowekewa ndani ya Rasimu hii hazina ushiriki wa wananchi wa kutosha na hivyo kumpa mwanya wa kuteua watu awatakao hata kama hawana sifa bila ya ushiriki wa Raia kupitia Bunge lao!

13) Wakati kuondolewa Raisi madarakani kunatokana na ridhaa ya malalamiko ya wabunge inapokuja kuondolewa Makamu wa Raisi Bunge limeporwa hiyo ridhaa na kukasimiwa kwa Raisin a hivyo makamu wa Raisi kutowajibika Bungeni. Kwa lugha nyingie ni kuwa kama Raisi hamtaki Makamu wa Raisi basi anamshitaki Bungeni lakini kama anamtaka hata kama anatuhuma kibao Bunge ni marufuku kuwajibisha. Swali hilo ni Bunge la kuidhibiti serikali au Bunge jina tu?

14) Ukiondoa uteuzi wa Waziri Mwandamizi, teuzi za Raisi za mawaziri namanaibu wao hawahitaji kuthibitishwa na Bunge. Hili Bunge kama haliwezi kuwathibitisha wabunge linawezaje kuwathibiti utendaji wao? Rasimu hii imefanyakzai ya ziada kuhakikisha Bunge lijalo ni Bunge butu ambalo ukiondoa malipo yao halina meno ya kuithibiti serikali.

15) La ajabu mwanasheria Mkuu atathibitishwa na Bunge lakini mawaziri na manaibu wao hapana. Hii imekaaje maana mwanasheria mkuu aliyethibitishwa na Bunge anakuwa na uhalali mkubwa kuliko hata mawaziri na manaibu wao ambao hawajapitia kwenye tanuru la Bunge kwa kupigiwa kura ya maoni.

16) Inapokuja umiliki wa akaunti nje kwa watumishi wa umma, katiba inakataza lakini inatoa mwanya wa Bunge kuunda sheria za kuruhusu watumishi wa umma kuwa na akaunti nje. Tatizo hapa ni kuwa anayetuhumiwa kuwa na akaunti nene nje ya nchi ni rahisi na wasaidizi wake kutokana na misamaha ya kodi ambao haijaidhinishwa na Bunge sasa kuliruhusu Bunge kupitia katiba kuendeleza wizi na uporaji wa mali za taifa hili ni kubariki dhuluma dhidi ya raia. Nilitarajia kutokana na tuhuma za viongozi wengi kutajwa kuwa wanamiliki akaunti kule Uswizi basi Tume isingetelekeka kwenye hili kumbe ndiyo wamejenga mazingira mabaya ya kuisigina hata hii rasimu kupitia sheria ndogondgo za Bunge! Kiburi hiki kimeongezeka hasa baada ya tume kupewa kibali ya kuisigina katiba iliyopo kwa kutumia sheria za kawaida ambazo kupitishwa kwake kunahitaji koramu ya wabunge wasiopungua 30 tu!

17) Inapokuja uthibiti wa misamaha ya kodi ambayo hushinikizwa na Raisi na kupitishwa na baraza la mawaziri hii inayoitwa katiba mpya ipo kimya ikimaanisha ya kuwa “business as usual”! Yaani hakuna mabadiliko nah ii ni katiba mpya jina tu siyo kimantiki hata chembe.

18) Bunge na mahakama zimenyang’anywa haki ya kujua kama Raisi alishauriwa vyema na kupuuzilia mbali ushauri wa baraza la mawaziri lakini bunge hilohilo likisaidiwa na watendaji wakuu wa mahakama kwa maana ya majaji wakuu wamepewa mamlaka ya kumchunguza Raisi. Hivi watamchunguzaje Raisi ambaye ushauri aliopewa wanakatazwa kuuchunguza? Hicho ni kiini macho na bila ya Bunge kuwa na mamlaka ya kuzisoma nyaraka mbalimbali za maamuzi ya vikao vya baraza la mawaziri pale ambapo kuna malalamiko yanayohusu utendaji wa Raisi na mawaziri sasa Bunge litawezaji kutekeleza majukumu yake yta kikatiba kama siyo ubabaishaji tu huu?

19) Makosa ya jinai ambayo yamegundulika baada ya Raisi kustaafu Bunge au mahakama kamwe haziwezi kuyachunguza jambo ambalo linaashiria ni jitihada za kulinda maovu yoyote ambayo Raisi ameyatenda na kumpa kinga ya kijumla ambayo itampa kiburi cha kufanya anavyoona inafaa kwa kuwa yuko juu ya sheria. Hii ni karne ya 21 au tunarudi karne ya 19?

20) Raisi kuteua manaibu mawaziri ambayo majukumu yao yanagongana na ya katibu mkuu ni kupunguza idadi ya wizara bila ya kupunguza matumizi.

21) Kazi za Waziri mwandamizi zinaingiliana na za Makamu wa Raisin a mawziri na hana uhaja zaidi ya kuleta migongano ya kiutendaji. Tume hii ambayo tangia tupate uhuru wamezoea kuwa na Waziri Mkuu wameshindwa kuona na kuwa na uelewa ya kuwa Waziri mwandamizi ni mzigo tu ambao inabidi tuukatae. Waziri mwandamizi kama alivyo waziri mkuu kwenye mfumo uliopo kawekwa pale ili kumlina Raisi kwa kubeba lawama pale mambo yanapokwenda kombo na ndiyo maana zimewekwa ibara za kuthibitishwa na Bunge bila kuwekwa utaratibu wa kuwajibika Bungeni. Bunge halina mamlaka ya kumchunguza chini ya mapendekezo haya. Bunge ni kuthibitisha uteuzi khalafu hawana mamlaka ya kumchunguza utendaji wake!

22) Mawaziri na manaibu wao hawahitaji kuthibitishwa na Bunge lakini katibu mkuu kiongozi uteuzi wake kuthibitishwa na Bunge. Hapa uhalali wa kisiasa wa mawaziri na manaibu wao umefifilishwa na wa katibu mkuu kiongozi ambao anawajibika kwa mawaziri na manaibu wao umeimarishwa lengo haliko wazi hata chembe.



23) Makatibu wakuu hawahitaji kuthibitishwa na Bunge kwa hiy0o matatizo ya kimfumo ya watendaji waandamizi serikalini kutowajibika bungeni rasimu hii inahimiza uendelee!

 
1) Nafasi za Ukatibu mkuu na ukatibu mkuu kiongozi zimetengewa maafisa waandamizi serikalini na kuleta ubaguzi kwa raia wenye sifa ambao wako nje ya utumishi wa umma ambao wangeweza kuleta chahcu ya mabadiliko. Rasimu hii inakataza ubaguzi wa aina zote lakini hapa umebarikiwa! Hii ni migongao ambayo haina ulkazima bali kuondolewa.
 

1) Ibara ya 120 (4) ya rasimu ambayo inahitaji kura za utungwaji wa sheria zizidi two thirds ya wabunge wa bara na two thirds ya wabunge wa visiwani unalenga kuhakikisha hilo bunge halifanyi kazi. Ni vigumu kupata hayo maridhiano kwenye sheria za kawaida. Zaidi ya nusu ya wabunge wa kila sehemu ya Muungao inatosha kuifanya hiyo kuwa sheria kwa kuzingatia koramu ya siku hiyo jambo ambalo halikubaiishwa kwenye ibara hii.

 
1)

2) Ibara ya 120 (4) ya rasimu ambayo inahitaji kura za utungwaji wa sheria zizidi two thirds ya wabunge wa bara na two thirds ya wabunge wa visiwani unalenga kuhakikisha hilo bunge halifanyi kazi. Ni vigumu kupata hayo maridhiano kwenye sheria za kawaida. Zaidi ya nusu ya wabunge wa kila sehemu ya Muungao inatosha kuifanya hiyo kuwa sheria kwa kuzingatia koramu ya siku hiyo jambo ambalo halikubaiishwa kwenye ibara hii.

3) Ibara ya 121 (1) inalizuia Bunge lisitunge sheria za masuala ya fedha lakini lipo kimya juu ya suala la misamaha ya kodi. Ibara tajwa imezungumzia kiujumla kuwa wanaweza kupunguza tozo za ushuru bila ya kuweka wazi ya kuwa misamaha ya kodi imekatazwa. Misamaha ya kodi ndiyo inaoongoza katika kulifukarish hili taifa lakini rasimu hii inasema hilo siyo tatizo!

4) Haki ya kupiga kura na haki ya uraia wa kuzaliwa siyo haki zinazoweza kunyang'anywa na sheria yoyote hivyo hazipaswi kuwekewa utata kama zilivyowekewa utata na hii rasimu ya katiba.

5) Kero nyingine iliyopo ambayo rasimu hii imeibariki ni kuwa vyama vya siasa vinaweza kutengua ridhaa ya wapigakura kwa kuwafukuza uanachama wabunge ambao iliwadhamini. Inavyotakiwa iwe ni kuwa wabunge aendelee na kazi ya kuwatumikia wananchi kama wabunge huru badala ya haki ya wapigakura kukasimiwa kwa vyama vya siasa.

6) Haki ya wapigakura kup[inga matokeo ya Ubunge kama ya uraisi yalipaswa kuainishwa na rasimu hii badala ya kuliachia bunge ambalo lina masilahi mazito ya kuwakataza wapigakura wasifungue mashauri ya kupinga matokeo endapo wanaona uchaguzi haukuwa huru na haki. Hii rasimi imetamka dola ipo mikononi mwa raia sasa hiki kigugumizi kinatoka wapi?

7) Rasimu hii imeiondoa Dodoma kama eneo na mahali pa vikao vya Bunge la sasa itategemeana na utashi wa Spika. Haya makao makuu kweli yatajengwa kwa utatani wa aina hii? Labda lengo ni kuweka utaratibu wa mzungukoi kati ya bara na visiwani.

8) Ushiriki wa mwanasheria wa serikali kwenye ajira za watumishi wa Bunge kunaashiria nini? Hana sababu ya kuwepo huko!

9) Jaji Mkuu umri unaanzia miaka 45 wakati umri wa Raisi unaanzia miaka 40. Hizi tofauti zaashiria nini?

10) Majaji wa mahakama ya juu hawahitaji kuapishwa na Bunge wakati Jaji Mkuu na Naibu wake kuapishwa na Bunge. Maana halisi ya uwajibikaji Bungeni imefifilishwa. Bunge kupitia raia ndiyo wanajua utendaji wa majaji husika sasa katiba inapowazuia kutoa michango yao juu ya teuzi za namna hii basi ni kubariki ufisadi na dhuluma nyingi ambazo zimezagaa katika mfumo uliopo.

 
1)

2) Ibara ya 120 (4) ya rasimu ambayo inahitaji kura za utungwaji wa sheria zizidi two thirds ya wabunge wa bara na two thirds ya wabunge wa visiwani unalenga kuhakikisha hilo bunge halifanyi kazi. Ni vigumu kupata hayo maridhiano kwenye sheria za kawaida. Zaidi ya nusu ya wabunge wa kila sehemu ya Muungao inatosha kuifanya hiyo kuwa sheria kwa kuzingatia koramu ya siku hiyo jambo ambalo halikubaiishwa kwenye ibara hii.

3) Ibara ya 121 (1) inalizuia Bunge lisitunge sheria za masuala ya fedha lakini lipo kimya juu ya suala la misamaha ya kodi. Ibara tajwa imezungumzia kiujumla kuwa wanaweza kupunguza tozo za ushuru bila ya kuweka wazi ya kuwa misamaha ya kodi imekatazwa. Misamaha ya kodi ndiyo inaoongoza katika kulifukarish hili taifa lakini rasimu hii inasema hilo siyo tatizo!

4) Haki ya kupiga kura na haki ya uraia wa kuzaliwa siyo haki zinazoweza kunyang’anywa na sheria yoyote hivyo hazipaswi kuwekewa utata kama zilivyowekewa utata na hii rasimu ya katiba.

5) Kero nyingine iliyopo ambayo rasimu hii imeibariki ni kuwa vyama vya siasa vinaweza kutengua ridhaa ya wapigakura kwa kuwafukuza uanachama wabunge ambao iliwadhamini. Inavyotakiwa iwe ni kuwa wabunge aendelee na kazi ya kuwatumikia wananchi kama wabunge huru badala ya haki ya wapigakura kukasimiwa kwa vyama vya siasa.

6) Haki ya wapigakura kup[inga matokeo ya Ubunge kama ya uraisi yalipaswa kuainishwa na rasimu hii badala ya kuliachia bunge ambalo lina masilahi mazito ya kuwakataza wapigakura wasifungue mashauri ya kupinga matokeo endapo wanaona uchaguzi haukuwa huru na haki. Hii rasimi imetamka dola ipo mikononi mwa raia sasa hiki kigugumizi kinatoka wapi?

7) Rasimu hii imeiondoa Dodoma kama eneo na mahali pa vikao vya Bunge la sasa itategemeana na utashi wa Spika. Haya makao makuu kweli yatajengwa kwa utatani wa aina hii? Labda lengo ni kuweka utaratibu wa mzungukoi kati ya bara na visiwani.

8) Ushiriki wa mwanasheria wa serikali kwenye ajira za watumishi wa Bunge kunaashiria nini? Hana sababu ya kuwepo huko!

9) Jaji Mkuu umri unaanzia miaka 45 wakati umri wa Raisi unaanzia miaka 40. Hizi tofauti zaashiria nini?

10) Majaji wa mahakama ya juu hawahitaji kuapishwa na Bunge wakati Jaji Mkuu na Naibu wake kuapishwa na Bunge. Maana halisi ya uwajibikaji Bungeni imefifilishwa. Bunge kupitia raia ndiyo wanajua utendaji wa majaji husika sasa katiba inapowazuia kutoa michango yao juu ya teuzi za namna hii basi ni kubariki ufisadi na dhuluma nyingi ambazo zimezagaa katika mfumo uliopo.

 
1) Rasimu hii inapendekeza kustaafu kwa jaji Mkuu na Naibu wake ni miaka 70. Hiv hawa vijana kweli lini watapata nafasi ya kufanyakazi za umma kama wazee ndiyo ving’anganizi?


2) Umri wa kustaafu majaji wa kawaida wa Mahakama ya juu haukuanishwa sasa sijui ni miaka 70 au 60? Rasimu imefanya hiyo kuwa ni siri!
 
1) Kwenye teuzi za majaji, bunge limetupiwa virago vyake. Halina ubavu wa kuhoji ajira hizi na hivyo kugeuzwa simba asiye na meno hata ya kubweka hawezi. Ipo kazi na hii rasimu watunzi wanaona ina hadhi ya kuitwa katiba mpya!
 
1) Umri wa kustaafu wa majaji wa mahakama ya rufaa kama ulke wa Mahakama ya juu umefichwa kama ni hivyo kwanini ule wa Jaji Mkuu na Naibu wake umeainishwa? Inanikumbusha kitabu cha “Animal Farm”……………wanyama wote ni sawa lakini wengineo ni sawa zaidi……….

2) Utenganishwaji wa Msajili wa Mahakama na Mtendaji Mkuu wa mahakama hiyo ni kuleta migongano isiyo ya lazima na kuwatafutia watu ajira. Kazi zote za msajili ni za mtendaji mkuu wa mahakama sasa kuzitenganisha na kuwatafutia watu ugali ni matumizi mabaya ya madaraka. Msajili anasemekana ana majukumu ya kuratibu shughuli za kimahakama bila ya kuusimamia mfuko wa mahakama hili lawezekana? Kazi ya kusimamia mfuko lipo kwa mtendaji mkuu ambaye haratibu shughuli za mahakama. Mtendaji mkuu majukumu yake ni ya kiuhasibu zaidi na ya Msajili ni ya kiutawala zaidi. Ili Msajili atekeleze majukumu yake ni lazima awe mtendaji mkuu na huyo mtendaji mkuu awe Mhasibu tu hapo migongano itakuwa haipo vinginevyo rasimu inatuandaa kwa mivutano isiyo na tija.

3) Wajumbe wa Tume ya kimahakama haina uwakilishi wa raia wa kawaida ambao ndiyo waathirika na maamuzi ya majaji sasa hii Tume itafanyaje kazi kama hakuna uwakilishi wa watu ambao ndiyo wahimili wa mwisho wa maamuzi ya kimahakama. Hivi hii kweli ni katiba mpya au katiba ya zamani ambayo imebandikwa viraka?

4) Ibara ya 185 ilikuwa ni nafasi ya kuanisha vigezo vya uteuzi wa utumishi wa umma kujumuisha ushindani na uwazi lakini nafasi hiyo haikutumika. Tume inaweza kupendekeza uteuzi wa viongozi bila ya kuzitangaza nafasi hizo na kudai waliopendekezwa wanao uweledi!
 
1)

2) Bodi ya Tume huru ya uchaguzi itakayoteuliwa na Raisi hahitaji kuthibitishwa na Bunge. Matatizo ya kimfumo yapo palepale. Bila ya kuthibitishwa na Bunge hiyo Tume ni huru kwa maana ya jina tu bali siyo shirikishi na wajibikaji kwa wananchi kupitia Bunge lao ambalo ndilo kazi yake kuhakiki maamuzi ya watendaji serikalini kama ufanyaji wa teuzi hizi.

3) Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi inayojiita ni huru nafasi za uenyekiti na unaibu uenyekiti zimehifadhiwa kwa majaji kama vile raia wengineo hawana sifa za kuzishika nafasi hizo ambazo ni kusimamia wataalamu waliochini yao. Majukumu haya siyo ya jaji ila ni ya raia yeyote mwenye sifa za kiutawala.

4) Ibara ya 190 (7) (b) ni tata kwa sababu kuwakataza watumishi wa umma kuwa wajumbe wa tume wakati tume yenyewe ni ya umma ni kutupotosha. Tatizo hapo ni lugha ya kuwa kama mteuliwa ni mtumishi wa umma kabla hajaanza majukumu mapya ya tume itabidi aachie ngazi ya shughuli nyiningineo ya umma aliyokuwa nayo.

 
1) Ibara ya 191 (1) inaleta migongano mikubwa ya mihimili ya dola ya mahakama na bunge na serikali. Majaji wakuu wanakatazwa na rasimu hii kufanya kazi za kiutendaji. Pili inawezekana kabisa tume ionekane machoni pa raia kuwa siyo huru kwa sababu kamati ya uteuzi inaundwa na mgombea uraisi wa chama tawala. Kamati ya Bunge inayoshughulikia ajira na nidhamu ndiyo ipewe majukumu haya na hii kamati ya uteuzi ivunjiliwe mbali kwa maana itaondoa uhalali wa matokeo ya chaguzi zetu hususani za Uraisi. Kero iliyopo leo ni mfumo ambao mgombea Uraisi anayo sauti ya kuteua tume aitakayo na hii inayojiita katiba mpya haijatatua hilo tatizo! Sasa hii ni katiba mpya au change la machoni tu? Maspika wa bara na visiwani wanatoka wapi kwani wao hawana ubavu kwenye shughuli za muungano. Mkurugenzi wa Tume anatoka wapi kwenye ajira hizi? Yeye mwenyewe inabidi aajiriwe na kama husika ya Bunge kuondoa hisia teuzi za tume zimefanywa na chama kimoja.

 

1) Ibara 191 (5) ni utapeli usio na kifani baada ya kuchakachua uteuzi wa wajumbe wa tume sasa bunge litapelekewa kuthibitisha kwanini lithibitishe kazi ya mgombea mtarajiwa wa uraisi kama siyo mgongano wa masilahi binafsi ambao umekatazwa na Ibara za 14-18?

 
1) Ibara ya 192 (5) imeweka utaratibu wa kumchunguza mjumbe wa tume lakini wapigakura hawana lao. Ni majaji na mawakili na kamishina wa tume ya haki za binadamu na mjumbe wa tume ya maadili ndiyo wamepewa kazi hizo na wapigakura wao ni kuangalia huo mchezo wa kuigiza unavyochezwa! Tutafika kweli kwa kuwakwepa wananchi na huku tukidai katiba hii ni yao tu lakini haiwashirikishi katika kufikia maamuzi?

2) Ibara ya 193 imekwepa kuweka kipengele cha kusema kutakuwepo na sheria ya uchaguzi ambayo tume itabidi iizingatie katika kusimamia, kuratibu na kutangaza matokeo ya uchaguzi. Hiki kipengele kimo kwenye katiba ya sasa lakini inavyoonekana hapa tume itajifanyia kazi inavyoona inafaa jambo ambalo ni hatari sana maana katiba siyo sheria ya uchaguzi ambayo kazi yake ni kufafanua kwa undani jinsi tume itakavyofanyakazi zake.

 
1) Mkurugenzi wa uchaguzi chini ya mapendekezo hayo ni jukumu la Raisi na Bunge halishirikishwi kuthibitisha uteuzi huu na Raisi wala hahitaji kushauriwa na chombo chochote kile! Yaani uteuzi huu ni suala binafsi la Raisi. Hivi uhuru wa hii tume uko wapi? Hata nafasi haitangazwi, wala hakuna ushindani wala Bunge halina mwanya wa kuhakiki uteuzi husika lengo la usiri huu ni nini kama siyo kuweka mtu ambaye atachakachua matokeo ya uraisi?

2) Ibara ya 197 (2) (b) inalazimisha vyama vya siasa kutopinga muungano sasa haki zao za kikatiba za kutoa maoni yao ziko wapi kama zinaona muungano hauna tija? Muungano ni mktaba wa hiari sasa unapolindwa na sheria badala ya ridhaa ya wahusika huo muungano ni feki.

 
1) Mkurugenzi wa uchaguzi chini ya mapendekezo hayo ni jukumu la Raisi na Bunge halishirikishwi kuthibitisha uteuzi huu na Raisi wala hahitaji kushauriwa na chombo chochote kile! Yaani uteuzi huu ni suala binafsi la Raisi. Hivi uhuru wa hii tume uko wapi? Hata nafasi haitangazwi, wala hakuna ushindani wala Bunge halina mwanya wa kuhakiki uteuzi husika lengo la usiri huu ni nini kama siyo kuweka mtu ambaye atachakachua matokeo ya uraisi?

2) Ibara ya 197 (2) (b) inalazimisha vyama vya siasa kutopinga muungano sasa haki zao za kikatiba za kutoa maoni yao ziko wapi kama zinaona muungano hauna tija? Muungano ni mktaba wa hiari sasa unapolindwa na sheria badala ya ridhaa ya wahusika huo muungano ni feki.

 
1) Ibara ya 198 inasema Msajili wa vyama vya siasa atateuliwa na Raisi kwa utaratibu ambao hauko wazi kupitia mapendekezo ya Tume ya utumishi wa umma na kuthibitishwa na Bunge sasa yawaje Mkurugenzi wa uchaguzi asithibitishwe na Bunge wala kupendekezwa na Tume ya utumishi wa umma kabla ya Raisi kumteua? Mazingira ya kuchakachua chaguzi zijazo yameandaliwa kwa uangalifu mkubwa sana.


2) Ibara ya 199 inapaswa Msajili aongezewe majukumu ya kutoa adhabu kwa vyama vya siasa ambavyo havifuati wajibu waliopewa na katiba na sheria za vyama vya siasa zitakazotungwa.

3) Ibara ya 200 (2) iondoe suala la kamati maalumu ya uteuzi kazi hizi zifanywe na tume ya utumishi wa umma maana inaingiliwa kazi zake.

4) Ibara 202 irekebishwe kwa sababu inaleta migongano kati ya mahakama na bunge na serikali. Kazi hizi zifanywe na kamati husika ya bunge.

 
1) Ibara 203 (2) (m) inatoa mwanya kwa tume ya maadili kufanya kazi bila ya uwazi kwa kuruhusiwa kutotoa taarifa zake kwa umma juu ya uchunguzi wake na kuwa na hiari ya kuzitoa au la na vigezo vya kufanya maamuzi ya namna hii havikuwekwa wazi! Kufanya kazi kwa usiri ndiyo nafasi inapewa taasisi ya umma kuuchakachua ukweli au kutumia mamlaka haya vibaya ikiwemo kukomoana. Taarifa za uchunguzi za Yule ambaye hakubaliki kujulishwa umma na za yule ambaye anakubalika kutiwa kapuni kwa minajili ya kumlinda.

 
1) Ibara 203 (2) (m) inatoa mwanya kwa tume ya maadili kufanya kazi bila ya uwazi kwa kuruhusiwa kutotoa taarifa zake kwa umma juu ya uchunguzi wake na kuwa na hiari ya kuzitoa au la na vigezo vya kufanya maamuzi ya namna hii havikuwekwa wazi! Kufanya kazi kwa usiri ndiyo nafasi inapewa taasisi ya umma kuuchakachua ukweli au kutumia mamlaka haya vibaya ikiwemo kukomoana. Taarifa za uchunguzi za Yule ambaye hakubaliki kujulishwa umma na za yule ambaye anakubalika kutiwa kapuni kwa minajili ya kumlinda.

 
Back
Top Bottom