Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
- #21
1) Ibara ya 205 (2) imethibitisha tatizo nililoliona ya kuwa tume ya uteuzi inaiingilia kazi za tume ya utumishi wa umma za kufanya mapendekezo ya uteuzi wa wajumbewa tume ya maadili. Inapokuja masuala ya kinidhamu tume ya utumishi wa umma inabebeshwa majukumu ya kuwathibiti wajumbe wa tume ya maadili wakati tume ya utumishi wa umma haikushirikishwa katika kuwateua. Ninarudia kamati maalumu ya uteuzi iliyofurika na majaji ifutwe na kazi zao zichukuliwe na tume ya utumishi wa umma.