Hiki ni kimojawapo ya mambo makuu yanayonifanya kukataa kutumia tena jina La Tanganyika. Tanganyika limekaa katika mtindo wa kutugawa...
Zipo nyingi faida za kuwaendelea kutumia jina la Tanzania.
Mh! Hiyo si sababu ya msingi, jina la T/bara linaleta utata, na umoja wa Afrika unaotaka ww ilikuwa iitwe tu Africa bara na Africa Zanzibar ili kudumisha huo umoja wa Africa, namuunga mkono Jaji Bomani kwa 100%, kwani jina Tanzania ni Tanganyika na Zanzibar, mambo ya kuengeza bara na visiwani hizo ni mbwembwe tu. Labda useme tu Tanganyika ni jina BAYA!Na mheshimu sana Jaji Bomani...lakini kwa hili sikubaliani naye. Jina la Tanganyika tukilitumia ama tukiwa tumetengwa na Zanzibar ama la litatugawa. Na hii itakuwa ni ushindi kwa wale ambao na maadui wa uafrika na wanafurahi sana wakiona waafrika wakigawanyika. Tusikubali mgawanyiko wa Waafrika.
Na mheshimu sana Jaji Bomani...lakini kwa hili sikubaliani naye. Jina la Tanganyika tukilitumia ama tukiwa tumetengwa na Zanzibar ama la litatugawa. Na hii itakuwa ni ushindi kwa wale ambao na maadui wa uafrika na wanafurahi sana wakiona waafrika wakigawanyika. Tusikubali mgawanyiko wa Waafrika.
Hakuna ubaya kujiita Tanganyika....
Lakini napendekeza Tanzania litumike kwani ni jina ambala watanzania wenyewe Tulilibuni...
Tanganyika tulipewa na wakoloni...halikuwepo hapo mwanzo ...unaweza kutueleza ni nani alitoa ruhusa tuiitwe Tanganyika ?
Mimi napendekeza kila mkoa uwe nchi kivyake..tusiekeane usiku
Hiki ni kimojawapo ya mambo makuu yanayonifanya kukataa kutumia tena jina La Tanganyika. Tanganyika limekaa katika mtindo wa kutugawa...umeona mwenye unasema linalandana na ziwa Tanganyika...hiyo maaana yake nini...kwamba na Kilimanjaro watataka wasikie jina lenye uhusiano na walipo, Songea hivyo hivyo mto Ruvuma, Dodoma na Bwawa lao maarufu Mtera...nakadhalika nakadhalika.
Faida chache za kubaki na jina Tanzania
1. Jina hili litatufanya watanzania (ambao wewe unataka tuitwe watanganyika) tuendelea kushikamana bila kutofautishana kwa misingi mingine.
2. Jina hili litaweka kumbukumbu sawa kuwa tuliwahi kuunga na nchi nyingine.
3. Jina hili litakuwa fimbo nzuri ya kuwatandika wale wenzetu waliotutenga(God forbid)-kama Wazanzibar watakubaliana na viongozi wao wanaowashawishi na kuwalazimisha kutubagua sisi watu wata Tanzania.
4. Jina hili litaendelea kutupa faraja na kujenga uimara wetu katika kuendeleza nia njema ya kuunganishwa waafrika kama wasisi wetu walivyokuwa wamefikiria hapo awali.
5. Jina hili litaonyesha ukarimu wetu kwa waafrika wenzetu.
6....
7.....
8..
Zipo nyingi faida za kuwaendelea kutumia jina la Tanzania.
Nashindwa kuelewa, ni mimi ndo sijakuelewa? Kwa maelezo yako uneonekana umeelewa kwamba TANZANIA haitakiwi tena. Ukweli ni kwamba, jina TANZANIA litaendelea kuwepo ktk serikali ya Shirikisho (muungano). Kinachozungumzwa hapa ni serikali hizi mbili, ya Zanzibar na Tanganyika. Kumbuka kabla hizi nchi mbili hazijaungana ziliitwa hivyo, sasa basi tuwe katika majina hayo ktk serikali zetu za nchi washirika, hilo jina TANZANIA tukutane nalo katika MUUNGANO tu. Hii ndo maana ya serikali tatu inayozungumzwa, siyo kwamba jina Tanzania halitakuwepo. Wasiwasi wako nimeuona hapo ulipoanza kuelezea Faida zako za kubaki na jina Tanzania.
labda walihisi watakuwa wanamfagilia mtikila
hebu tushupalie hili jina libadilishwe wakuu! vinginevyo na zanzibar nayo isomeke tanzania visiwani ndo itakuwa imebalansi
....1. Ukweli ni kwamba, jina TANZANIA litaendelea kuwepo ktk serikali ya Shirikisho (muungano). Kinachozungumzwa hapa ni serikali hizi mbili, ya Zanzibar na Tanganyika. Kumbuka kabla hizi nchi mbili hazijaungana ziliitwa hivyo, 2.sasa basi tuwe katika majina hayo ktk serikali zetu za nchi washirika, hilo jina TANZANIA tukutane nalo katika MUUNGANO tu. Hii ndo maana ya serikali tatu inayozungumzwa, siyo kwamba jina Tanzania halitakuwepo. 3. Wasiwasi wako nimeuona hapo ulipoanza kuelezea Faida zako za kubaki na jina Tanzania.
Lakini jina la tanzania liwepo ktk shirikisho au muungano,nje ya muungano hakuna jina tanzania kuna jina tanganyika na zanzibar,kwanini wakwepe jina tanganyika na kutaka liwepo tanzania bara??huu ni wizi wa majina ya pamoja jina tz bara liondoke na tusiliogope tanganyika,hili ndio jina halisi
Safari hii watanganyika kaunganeni na kenya muitwe tankenyan.
1. Mpaka hapo tupo pamoja
2. & 3. Hapa tunaanza kupishan;kwanza msimamo wangu kama raia wa nchi hii ni kuwa ama ziwepo serikali mbili ama serikali moja. Sasa kama wazanzibar watatutenga (God forbid) wakawa na serikali yao sisi tuendelee kutumia jina hilo la Tanzania kwa sababu na faida nilizozitaja kwenye post za mwazo za uzi huu. Nia ni njema kabisa ya mimi kutetea tuendelee kutumia jina hili. Nakuhakikishieni tukiweza kuendelea kutumia jina hili tutaepuka mtego ambao wazanzibar wanataka kuingia vile vile tutaweza kukwepa matatizo ambayo Mwl. Nyerere aliwahi kututaadharisha. Lakini kama wazanzibar watakubali ku 'dissolve' serikali yao tukawa na serikali moja basi itakuwa "well and Good" kutumia jina Tanziania maana jambo lilokuwa limeasisiwa na wazalendo wa awali wa nchi hii itakuwa imetimia.
N.B
Kuna jambo moja ambalo nimeligudua kuna wanasiasa ambao wanaotoka eneo la bara la JMT ambao kwa udi na uvumba wanataka wazanzibar watutenge. Wanasiasa hawa utawajua kwa hila yao hii chafu kupitia kauli wanazozitoa... mfano utawasikia wakisema " mfumo wa kuwa na serikali moja hauwezekani kwa sababu wazanzibar hawatakubali ". Nashindwa kuelewa ina maana wanasiasa hawa ndio wanavipimo vya kujua mawazo ya wazanzibar wote ?
Sote kwa pamoja tuhimizane tuwe na serikali moja ....tuachane na mambo ya mashirikisho.