Rasmi, Nigeria yatangaza kuuza mafuta yake kwa kutumia sarafu yake ya Naira badala ya Dola Marekani

Made
Madeni ya benki ya dunia yanatakiwa yalipwe Kwa sarafu gani
 
Wakati wenzetu wakipiga hatua kwenda mbele.

Sisi watanzania tunapiga hatua kurudi nyuma.

Tunadalalia kila rasilimali tuliyonayo.
 
Hixo hatua wauziane wenyewe humo ndani na Naira zao, international trade zina masharti mengine.

Watamuuzia urusi na China hayo mafuta?

Wape muda utasikia.

Masikini huwa tukishiba tuna lala tunasahau njaa huwa ina rudi tena kwa kasi sana.
Sisi wenyewe sasa hivi pesa zote za kulipia huduma hata za kitalii hatutaki dollar tunataka pesa za Tanzania

Mtu akija na dollar anunue pesa za Tanzania alipie kwa hela za Tanzania
 
Nadhani siku Tanzania tukaamua na sisi inawezekana wazo ni kuwa ikiwa tutajiunga BRICKS hatuwezi kutumia pesa Yao kufanya biashara?
 
Ikiwa madeni ni kwa Dola , Nigeria inadaiwa zaidi ya Tsh trillion 69 ,je unafikiri yeye mwenyewe hataki dola
 
Sisi wenyewe sasa hivi pesa zote za kulipia huduma hata za kitalii hatutaki dollar tunataka pesa za Tanzania

Mtu akija na dollar anunue pesa za Tanzania alipie kwa hela za Tanzania
Hahaha sawa kumbuka shibe ni mpito, ila njaa ni endelevu.

Kwa sasa shilingi moja mnauza dollar ngapi?
 
Ikiwa madeni ni kwa Dola , Nigeria inadaiwa zaidi ya Tsh trillion 69 ,je unafikiri yeye mwenyewe hataki dola
Ndio maana huwa wanatulazimisha tukope ile pesa yao ibakie na nguvu.
 
Sio kujitekenya hiyo hatua itapandisha thamani ya Naira

Nenda hapo Afrika kusini tu dolla huwa hawataki wanataka ununue bidhaa zao kwa Rand

Ubanunua Rand kwa dola ndio ununue bidhaa zao kwa Rand
Hiyo rand bado iko chin sana ukilinganisha na dollar pia south Africa n ulaya ndogo Nigeria hiyo choka mbaya kama tanzagiza tu
 
Bravo! Hivyo ndivyo tunavyobidi kwenda ili kujikomboa kiuchumi. Nigeria ni mzalishaji mkubw wa mafuta duniani. Lakini uhaba wa mafuta kwenye vituo vya kuuzia mafuta ndani ya nchi ni mkubwa kuliko ilivyo nchini Tanzania, nchi ambayo haizalishi mafuta.
 
Wazo zuri sana kwao, ingawa sijui kama litatekelezeka kirahisi.
By the way kwa nini serikali yao inagoma kumuuzia mafuta ghafi Dangote? Wanahofia nini?
 
Hiyo rand bado iko chin sana ukilinganisha na dollar pia south Africa n ulaya ndogo Nigeria hiyo choka mbaya kama tanzagiza tu
Kwa mafuta waweza toka ni mzalishaji mkuu wa mafuta duniani akishika nafasi ya tisa duniani na ni member wa OPEC

Na mafuta ya Nigeria ni mazuri mno
 
Wakati wenzetu wakipiga hatua kwenda mbele.

Sisi watanzania tunapiga hatua kurudi nyuma.

Tunadalalia kila rasilimali tuliyonayo.
Inauma lakini
Wabongo tumeshindwa Hadi kuendesha miradi wa mabasi wenye wateja wa kutosha
 
Nadhani siku Tanzania tukaamua na sisi inawezekana wazo ni kuwa ikiwa tutajiunga BRICKS hatuwezi kutumia pesa Yao kufanya biashara?
Tatizo tunaishi kwa madeni na misaada ambayo yote ipo kwa dollar kwa sababu marekani ndio nchi inayotoa misaada mingi kwa tz , kutoka kwenye mfumo wa mabeberu maana yake unaweza kujitegemea, kwahiyo haiwezekani kutoka kwenye mfumo wa dollar kwa nchi kama tanzania
 
Bravo! Hivyo ndivyo tunavyobidi kwenda ili kujikomboa kiuchumi. Nigeria ni mzalishaji mkubw wa mafuta duniani. Lakini uhaba wa mafuta kwenye vituo vya kuuzia mafuta ndani ya nchi ni mkubwa kuliko ilivyo nchini Tanzania, nchi ambayo haizalishi mafuta.
Mafuta ya Nigeria yana quality ya juu mno yanagombaniwa hivyo yote huwa exported halafu wao hu import toka Malta sababu hawana refinery

Sasa hivi Dangote kajenga refinery kwa hiyo wanaanza kuuza mafuta yaliyosafushwa sio ghafi

Ndio maana sasa wataka Naira sio dollar ili waimarishe currency yao
 
Inawezekana Kwani haiwezekani kusema nchi yoyote inayotaka kununua kitu kutoka Tanzania I change pesa kutoka dollar kuja kwenye Tsh then ndy anunue anachotaka?, ikiwa inawezekana hili Kuna namna tunaweza kuipandisha pesa yetu na kuwa juu
 
Inawezekana Kwani haiwezekani kusema nchi yoyote inayotaka kununua kitu kutoka Tanzania I change pesa kutoka dollar kuja kwenye Tsh then ndy anunue anachotaka?, ikiwa inawezekana hili Kuna namna tunaweza kuipandisha pesa yetu na kuwa juu
Ubaya ni kwamba sisi kama nchi tuna high demand ya dollar ,yani tunaihitaji haswa kwahiyo hicho unachosema in practice hakiwezekani,
 
Hahaha ya Sisi hizo Naira tutazitoa wapi?
Waongo tu hao wanajazana upepo, hata Nigerians hawayaki Hizo Naira, wana zibadili kwa dollor na kutunza dollar.
Wanajidanganya kwa muda mfupi na kujipa matumaini tu.
Uchumi ni zero kichwani mwako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…