Rasmi Tundu Lissu ajibu tuhuma za muda mrefu kuhusu wanachama wa CHADEMA kujiteka wenyewe

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Akiongea na BBC Swahili hivi karibuni, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu hatimaye amezizungumzia tetesi na tuhuma zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba CHADEMA wana hulka ya kujiteka wenyewe ili wapate huruma ya wananchi.

Kwenye mahojiano hayo, Lissu amegusia sakata la Chacha Wangwe ambaye kwa muda mrefu sasa, limekuwa ni gumzo kutokana na tetesi zilizosambaa kuwa kada huyo wa CHADEMA aliuliwa na chama chake.

Kuhusiana na sakata hilo Lisssu amedokeza kuwa tuhuma hizo si za kweli na kwamba kama ingekuwa ni kweli basi wangechunguzwa.


Tundu Lissu aliongeza kwa kusema:

"Haya maneno ni aidha ya wauaji wenyewe au wapambe wao. Hizi si maneno ambazo zinapaswa kutiliwa maanani na mtu yoyote mwenye akili"

Soma pia: Tundu Lissu: Vyombo vya Usalama haviwezi kujichunguza vyenyewe sakata la Mauaji na Utekaji nchini
 
hivi kweli hata lissu angekuwa amepata kichaa hawezi kusema kuwa wangwe walimuuwa wao lazima akatae
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…