RASMI - UEFA yaondoa sheria ya goli la ugenini

RASMI - UEFA yaondoa sheria ya goli la ugenini

denooJ

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2020
Posts
18,509
Reaction score
68,228
Habari ndio hiyo, sasa kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake.

Sheria hiyo iliyoanzishwa mwaka 1965 itaondolewa kuanzia msimu ujao kwenye mashindano ya UEFA ikiwemo Champions League.

Sheria hiyo iliyokuwa inaibeba timu iliyofunga magoli mengi ugenini imekuwa ikitumiwa kwenye mashindano yote ya UEFA ngazi za vilabu kuanzia Europa League na Champions League.

Rais wa UEFA Alexander Ceferin amenukukiwa akisema; sio sahihi tena kwa goli la ugenini kuwa na uzito wa ziada.

Natumai Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) nalo litafuata mfano wa UEFA kuondoa hiyo sheria iliyopitwa na wakati.

- Ushindi mechi tano wakukumbukwa zaidi wa sheria ya goli la ugenini, ligi ya mabingwa Ulaya.

1. May 2019: Ajax 2 - Tottenham 3 (Agg. 3-3), Tottenham wakapita kwa goli la ugenini.

2. Apr. 2019: Man City 4 - Tottenham 3 (Agg. 4-4), Tottenham wakapita kwa goli la ugenini.

3. March 2019: PSG 1- Man Utd 3 (Agg. 3-3) Man utd wakapita kwa goli la ugenini.

4. April 2018: Roma 3- Barca 0 (Agg. 4-4) Roma wakapita kwa goli la ugenini.

5. May 2009: Chelsea 1 - Barca 1 (Agg. 1-1) Barca wakapita kwa goli la ugenini.
 
Lile goli lilikuwa tamu na lilikuwa chungu pia...ngoja tuone sheria mpya kama nayo itanoga!
Nilikuwa silipendi mara nyingi niliona linazibeba timu zenye uwezo mdogo, wanakubahatisha kimoja cha maana then ni kupaki basi mwanzo mwisho, utahangaika utafute pa kupita mpaka dakika 90 zinaisha hujapiga hata one shot on target.
 
Hahaha kama vile presha imeshuka upande A na kwenda upande B.

Yale mambo ya kupaki basi kwa vile una goli la ugenini ndiyo yanaelekea ukingoni.

Stori za tumekufa kiume ndiyo zimeisha.
Kabisaa, sasa kila mbuzi ale kwa urefu wa kamba yake.
 
Nilikuwa silipendi mara nyingi niliona linazibeba timu zenye uwezo mdogo, wanakubahatisha kimoja cha maana then ni kupaki basi mwanzo mwisho, utahangaika utafute pa kupita mpaka dakika 90 zinaisha hujapiga hata one shot on target.
Lkn unausahau haka kautamu...timu yako imefungwa 3-1 away ukaja home ukafunga 2-0 kwa sheria ya zamani si inakuwa imeisha iyo?
 
Hahaha kama vile presha imeshuka upande A na kwenda upande B.

Yale mambo ya kupaki basi kwa vile una goli la ugenini ndiyo yanaelekea ukingoni.

Stori za tumekufa kiume ndiyo zimeisha.
😂😂😂😂😂😂
 
Hata sheria ya offside nayo ya kifala kwa sasa watu wanapima eti mtu kzidi kisigino.
Iwe kama mpira kuingia golini lazima mtu mwili wote uwe kweli offside.
 
Lkn unausahau haka kautamu...timu yako imefungwa 3-1 away ukaja home ukafunga 2-0 kwa sheria ya zamani si inakuwa imeisha iyo?
Hapa ndio utafurahi sasa, utaruka ruka kama ndama!.
 
Hata sheria ya offside nayo ya kifala kwa sasa watu wanapima eti mtu kzidi kisigino.
Iwe kama mpira kuingia golini lazima mtu mwili wote uwe kweli offside.
VAR miyeyusho nakubaliana nawe, siku hizi wachezaji kabla ya kushangilia goli kwanza wanaangalia VAR.
 
Hii sijaipata fresh,

Ina maanisha Simba akienda Zambia kucheza na Nkana, tukapigwa 2-1

Inatakiwa ashinde goli ngapi kwa mkapa ili asonge mbele?
 
Huu ndio ulikuwa utamu wa mpira sasa
Nilikuwa silipendi mara nyingi niliona linazibeba timu zenye uwezo mdogo, wanakubahatisha kimoja cha maana then ni kupaki basi mwanzo mwisho, utahangaika utafute pa kupita mpaka dakika 90 zinaisha hujapiga hata one shot on target.
 
Hii sijaipata fresh,

Ina maanisha Simba akienda Zambia kucheza na Nkana, tukapigwa 2-1

Inatakiwa ashinde goli ngapi kwa mkapa ili asonge mbele?
Hii ni kwa mashindano ya shirikisho la mpira barani ulaya (UEFA), huku kwetu kwa CAF mambo bado yapo kama zamani, sheria ya goli la ugenini bado inatumika, hapo Simba lazima ashinde 1-0 kwa Mkapa ili asonge mbele
 
Hii sijaipata fresh,

Ina maanisha Simba akienda Zambia kucheza na Nkana, tukapigwa 2-1

Inatakiwa ashinde goli ngapi kwa mkapa ili asonge mbele?

Ashinde goli moja ili muende ule muda wa nyongeza dk 30.kwa sababu matokeo yatakuwa 2-2 hakuna tena goli la ugenini.dk hizo zikiisha kwa matokeo hayo wataenda penati.

Ama kiurahisi zaidi simba ashinde goli mbili kwa sifuri tu hapo bila kuruhusu goli.kwa kila namna Simba anatakiwa ashinde ushindi wa kumzidi mpinzani wake goli 2, kama atamfunga 3 kwa 1 matokeo ya kwenda yatakuwa(simba 4 Nkana 2).

Hii ni kama sheria ya goli la ugenini kwa club bingwa Africa likifutwa.
 
Ashinde goli moja ili muende ule muda wa nyongeza dk 30.kwa sababu matokeo yatakuwa 2-2 hakuna tena goli la ugenini.dk hizo zikiisha kwa matokeo hayo wataenda penati.ama kiurahisi zaidi simba ashinde goli mbili kwa sifuri tu hapo bila kuruhusu goli.kwa kila namna Simba anatakiwa ashinde ushindi wa kumzidi mpinzani wake goli 2, kama atamfunga 3 kwa 1 matokeo ya kwenda yatakuwa(simba 4 Nkana 2).hii ni kama sheria ya goli la ugenini kwa club bingwa africa likifutwa.
No. Hiyo sheria imeondolewa mashindano ngazi ya vilabu Ulaya sio Afrika.
 
Back
Top Bottom