Ratiba rasmi ya rais Magufuli 2018-2025 hii hapa.Usifungue kama una presha

JPM kwa miundombinu amewapiku maraisi woote waliowahi kuongoza TZ ila naye amefeli sana kwenye demokrasia kuliko maraisi wote

Democracy is not good for a developing country as preached by west (protests, gays, etc)

Democracy is easy to hijack so that it becomes a fake one like in many African countries.

To me democracy is about the right to chose what to eat for breakfast, super, among plentiful food.

Right to chose between many forms of career to be pursued by the youth and become employed/employees.

Choice to visit doctors when sick

Equitable share of natural resources etc
 
Hao wanaofungua nyuzi kulalamika wapo Duniani kote, Hata ungefanya Nini wangebaki kulalamika, kwani hujawaona wanaofungua nyuzi kila siku kupinga ununuzi wa Ndege??
 
Nizimungumzie upande wa afya
Kila kituo cha afya( health centres) kupewa tsh 500 M kwa ajili ya upanuzi wa majengo zaidi afya ya mama na mtoto kujenga maabara na theatre hii naona wamefanya kitu super kabisa, upande wa dawa na vifaa tiba nako ameongeza nguvu sana ,kupanua hosp za kanda Kwa kuongeza huduma as mionzi (imaging studies )CT scan,MRI pamoja na cancer institute nayo kaweza sana...
Kumwaga medical doctors katika vituo vya afya kupunguza vifo cha akina mama na watoto pamoja na ajira zaidi ya 10000 za afya hapa pia naona kaweza. ...
 
Unalinganisha Chuwi na Simba, Kikwete alikuwa zama zingine na Magufuli yuko zama tofauti. Linganisha Kikwete na Kibaki au Magufuli na Kenyatta kupata picha kili.

Inabidi tumliganishe JPM na Kikwete, mtaje kila mtakachosema mafanikio yake alikikuta vipi na sasa kiko vipi maana JPM bado hajafikia level ya kulinganishwa na rais yeyote Kenya, hata kwa Uhuru pekee yake hajafika robo ya mafanikio ya rais Uhuru. Hebu mnitajie mradi mmoja mkubwa ambao alianzisha na kukamilisha hadi unaonekana na kutumika, mojawapo wa taaluma zangu ni projects management na muulize PM yeyote, kama kuna kitu kigumu kwenye mradi wowote, ni kufikisha hatima ya mradi na kuona ulichokitengeneza kinatumika kabisa.

Ukiangalia rais Uhuru kwenye awamu ya kwanza pekee yake alikua amekamilisha bonge la reli ya SGR ambayo urefu wake wa kilomita 500 ni zaidi ya mara mbili ya hako kasafu ka JPM kanachomuuma akili ka umbali wa kilomita 200, ambako hadi leo hii ni mapicha mapicha tu ya kwenye mitandao, siku kakizinduliwa na kutumika na treni moja ndio mje kuongea.

Kuna mifano mingi sana ambayo naweza nikakutajia jinsi Uhuru alizipata na yeye akaongeza zikafikia level gani

Nikutajie tu chache, wakati anaingia madarakani alikuta shule 8,000 pekee ndio zilikua zimeunga kwenye umeme, alikamilisha hatamu ya kwanza kama zimefikia 20,450
Wakenya 2.3m walikua na umeme, wakati huo akafikisha 4.1m
Umeme ulikua 1,660 megawatts yeye kaongeza 600 megawatts
Kakuta 2,200km of transmission lines na kuongeza 700km

Hapo sijataja barabara, bandari na mengine makubwa....
 
Hope these are not cooked data. Wajuzi wa mambo leteni figures za bongo
 
Mk54 akikujibu nitag
 
Haha kila siku kuota Kenya. LMAO umecheki installed power capacity ya Kenya according to these ignoramuses? [emoji23][emoji23][emoji23]
Eti tunatoshana at 1350MW na vile dar generators zimejaa juu ya power outages/ rationing.
 
Bro ebu tumia akili nshasema ili umlinganishe JPM na kikwete inabidi usubiri magufuri amalize mpaka 2025 apo ndo utakuws fea ila kumlinganisha mtu aliyetawala mika 10 na wa miaka 2.6 sio sawa pia kumringanisha JPM na kenyata itabidi usubiri 2020 maana uliyoyataja kenyatta aliyafanya kwa miaka mitano(2013-2017)
 
Haha, nacheka kwasababu ni Uhuru Kenyatta mwenywe ndio anapanda majukwaani na kusema atafanya kazi kama JPM.

Uhuru miaka 6, JPM 2½ halafu unataka kiwalimgamisha. 43% ya watoto walio kuwa wana shindwa kwenda shule za msingi kwa kikosa ada, leo wanaenda shule. Upande wa sekondari hiyo ni 10%.

Umeme unakusudiwa kufika zaidi ya ya 3500MW ndani ya miaka miwili. Bandari inachimbuliwa hivi sasa, leo hii reli za meter gauge ambazo hazijatumika kwa takriban 30yrs zimefufuka na zingine zinakarabatiwa. Wafanyakazi hewa 19,000, wakurugenzi wa mashirika mishahara imepumguzwa, ufufuaji wa mashirika makuu ya usafiri na mawasliamo. Zowezi zima la rushwa, kubwa na ndogo, rada za ndege za abiria nchi nzima, mikoa 7 inajengewa wodi maalum ya watoto wachanga. Vituo 12 vya ukusanyaji damu nchini, vitanda mahospitalini, bado sijagusia hospitali za rufaa zinazo jengwa mpya. Upande wa mageuzi ya kimfumo, mabenki, mashirika ya umma, tawala za mikoa, kuhamia Dodoma, ukusanjaji wa kodi, hati za viwanja, mabadiliko ya sheria za madini, kukaa chini na kujadilia na wachimbaji wa madini wakubwa. Yote hii ni ndani ya miaka 2½, na wala sijaweka vitu ambayo JPM amerithi kutoka serikali ya Kikwete.
 

Mada imekushinda hadi umeamua kujitoa ufahamu kwa kutumia uwongo, hebu weka video hata kamoja ka Uhuru akisema atafanya kazi kama JPM, maana akithubutu kuiga JPM atarudisha nchi yetu miaka 20 iliyopita. Tutaanza kuishi kwa uwoga uwoga wa kikorea Kaskazini kama mnavyoishi.
Halafu mimi nimelinganisha mafanikio ya Uhuru ya hatamu yake ya mwanzo, ambapo na JPM yupo kwenye hatua za mwisho za hatamu ya kwanza.
Tuliambiwa siku 100 za kwanza za JPM mtakua mumetupita, sasa hadi leo sijaona chochote kikubwa mlichofanikisha na kikaonekana.
 
Tusisahau ratiba za uzinduzi za Makamu,PM na viongozi wengine ambazo zitakuwemo kusindikiza zinduzi za Mh Rais.

"watapata tabu sana "
 

Hutaona haya yakiongelewa na hao maroporopo wa ufipa of course wapo wachache sana hiyo 2020 hata wakiambulia jimbo moja wakatoe sadaka

Kujua uchache wao na nguvu yao ya mdomo ni yale maandamano yao ya kipindi kile, tulipata kila aina ya vitisho kwamba pasingekalika Tanzania hii lakini siku ya tukio hata kuku alikua hakatizi mitaani, kwa hiyo tunawajua hawatupi shida.
 
Mambo yameshaanza tarayari. Hii ilikuwa ratiba ya jana.

 
Nawaonea huruma wajukuu na vitukuu vyetukwa madeni watakayo achiwa na Magufuli
Huyu mtu anakopa kila mahali kama vile hana akili nzuri na mbaya zaidi kila mradi utakuwa umekufa wakati wa kulipa madeni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…