Ratiba ya bunge la katiba leo tarehe 18-3-2014.

Ratiba ya bunge la katiba leo tarehe 18-3-2014.

Simiyu Yetu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2013
Posts
18,949
Reaction score
4,639
Baada ya jana jioni bunge la katiba kuingia katika hali ya sintofahamu iliyochangiwa pia na wabunge wa chadema,cuf na nccr- mageuzi leo asubuhi bunge litaendelea na shughuri zake kama inavyoonesha hapa chini.

1. Kuanzia saa tatu asubuhi mwenyekiti wa bunge maalumu mh samweli sitta ataweza kuwaapisha wabunge waliosalia kuapa ambao idadi yao yapata kama thelathini hivi.

2. Baada ya wabunge hao kumaliza kuapa jaji warioba ataweza kuwasilisha rasimu ya pili ya katiba ambapo imepangwa kuanza saa tatu na nusu au na dakika arobaini na tano mpaka saa saba kamili mchana.

3. Baada ya warioba kumaliza kuwasilisha rasimu mwenyekiti atalieleza bunge nini kitafuata baada ya zoezi hilo kukamilika.

Hivyo ndivyo utaratibu utakavyokuwa kwa leo karibu sana tuendelee kufuatilia katiba yetu inavyotungwa.

Samahani wakuu hiyo tarehe ni 18-3-2014 mkono uliteleza kidogo.
 
Kanuni haziruhusu warioba kuwasilisha kabla ya dhaifu hajafungua bunge
 
Kanuni haziruhusu warioba kuwasilisha kabla ya dhaifu hajafungua bunge
Unabisha ambacho hukijui au unabisha unachokijua any way ngoja saa tatu ifike uone nini kitafanyika make huu ubishi mwingine hauna maana hata chembe.
 
Mbona umeanzisha wewe badala ya Chabruma?....anyway kuna maridhiano yoyote yalifanyika baina ya UKAWA (sina uhakika na kifupisho hiki) na 6....kama la nataraji mvutano uliotokea jana utaendelea na leo hii pia.
 
Mbona umeanzisha wewe badala ya Chabruma?....anyway kuna maridhiano yoyote yalifanyika baina ya UKAWA na 6....kama la nataraji mvutano uliotokea jana utaendela na leo hii pia.
Yalikwisha jana hiyo hiyo leo ratiba kama ilivyopangwa tunasonga mbele penye wengi hapaharibiki neno mkuu.
 
Umekurupuka wazo likiwa kumuwahi nduguyo Chabruma kuanzisha uzi mpaka ukakosea kuandika tarehe,

Leo ni tarehe 18/03/2014 na sio tarehe 8/03/2014


Hahaaaaahaa haya karibu
 
Last edited by a moderator:
Mbona umeanzisha wewe badala ya Chabruma?....anyway kuna maridhiano yoyote yalifanyika baina ya UKAWA (sina uhakika na kifupisho hiki) na 6....kama la nataraji mvutano uliotokea jana utaendelea na leo hii pia.
Mkuu, mara baada ya mkutano wa jana kuvunjika, Kikao cha Kamati ya Mashauriano kiliitishwa. Katika kikao hicho, viongozi wa UKAWA walikuwepo na maridhiano yaliyofikiwa walikuwa pamoja. Labda leo kwani ni hulka yao kugeuka
 
Hakuna kanuni ambayo hutungwa na bunge halafu isitenguliwe na bunge husika jaribu kujielimisha mkuu.

Hakuna kanuni inayotungwa na bunge zima ikatenguliwa kwa utashi wa mtu mmoja kwa maslahi ya kikundi chake akafumbiwa macho. UKAWA msilifumbie macho
 
Yalikwisha jana hiyo hiyo leo ratiba kama ilivyopangwa tunasonga mbele penye wengi hapaharibiki neno mkuu.

Yaliishaje mkuu, hoja zao ambazo zilikua zinalaani uvunjifu wa kanuni kwa makusudi na sitta umeridhiwa na UKAWA? au makubaliano yao yapoje???
 
kwa hiyo wale waliopiga kelele jana wamekubaliana na hilo. ila hawa wabunge wanifurahishi kabisa, yaani badala ya kupinga kitu kwa hoja wanatumia nguvu, na wengi wao ni wapinzani
 
kwa hiyo wale waliopiga kelele jana wamekubaliana na hilo. ila hawa wabunge wanifurahishi kabisa, yaani badala ya kupinga kitu kwa hoja wanatumia nguvu, na wengi wao ni wapinzani

Wanaccm hawawezi kupinga uvunjifu wowote kanuni maana wametoka ukoo ule ule usiopenda serikali 3. Alovunja kanuni analinda maslahi ya walewale wasiopenda serikal 3. UKAWA simamieni kanuni zilizotungwa na bunge hilo wiki tatu huku kila mbunge akiwa amevuta zaidi ya mil.6 za posho kwa kutunga hzo kanuni zinazovunjwa leo.
 
Wanatupotezea muda tuu...sasa tofauti ya masaa mawili au manne ambao wameridhiana leo ni nini ? Kwani siwangesubiri Warioba aongee waone kama huo muda aliopangiwa hautamtosha..? Mimi ndio maana mpaka sasa hv I doubt wapinzani kama wana hekima na busara ya kuongoza nchi.....
 
Wakuu sitta alitoa dk 60 kwa Warioba lkn sasa atawasilisha kwa muda mrefu mpaka akamilishe kwa uhuru mpana.
 
Wanatupotezea muda tuu...sasa tofauti ya masaa mawili au manne ambao wameridhiana leo ni nini ? Kwani siwangesubiri Warioba aongee waone kama huo muda aliopangiwa hautamtosha..? Mimi ndio maana mpaka sasa hv I doubt wapinzani kama wana hekima na busara ya kuongoza nchi.....

6 kavurugizwa, kwa upuuzi huu naomba hata ngumi zipigwe
 
Back
Top Bottom