Ushauri wangu chadema siku ya kufunga kampeni Dar es salaam, ikiwezekana fanyieni jangwani, pia wilaya zote za dar ziwepo hapo, pia mkutano au hotuba ya mh.lissu iandikwe rasmi, pia apewe muda wa kutosha kuhutubia kama masaa matatu hivi, pia ikiwezekana irushwe live na radio na TV, bila kusahau mitandao ya kijamii.Ombeni TV moja au mbili irushe mkutano huo, hoja zote zilizotolewa na jpm akiwa dar zijibiwe ipasavyo.Siku hyo mh.lissu ashauliwe kushusha jazba atulie hasa.pia hotuba hiyo ionyeshe mahali tulikotoka,tulipo, tunakoelekea na tulipokwama na namna ya kutoka iwapo chadema ikichaguliwa.pia wabunge wa dar wanadiwe ipasavyo kwa kuonyesha kwa nn wao wachaguliwe na sio wa ccm.Pia nashauri wafuatao wawepo, ponda, prof.baregu,sheikh Katimba,mwamakula, ikiwezekana na askofu bagonza waalikwe.Pia wajitaidi mkutano uishe saa kumi na mbili jioni bila kuzidisha muda