RC Chalamila alikosea na alipaswa kuomba msamaha sio kujieleza

RC Chalamila alikosea na alipaswa kuomba msamaha sio kujieleza

Error 404

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2022
Posts
2,151
Reaction score
3,493
Habari JF , leo katika pitapita zangu nimekutana na kauli iliyozua maswali mengi sana kutoka kwa RC Chalamila , kwa ataeshindwa kununua gloves akajifungulie nyumbani .

Kimsingi inawezekana ni kauli sahihi katika mambo mengine ya afya lakini katika suala la uzazi ambalo lina faida kwa Serikali na familia inaweza isiwe sahihi kwa sababu :-

1.Kiafya ,Kijamii na kisiasa Mama mjamzito ni mtu anayehitaji mahitaji na huduma maalumu .

>>Kiafya kutokana na mabadiliko yanayotokana na ujauzito Changamoto nyingi sana zinaweza mkuta huyu mama ikiwemo kupoteza mtoto , mama mwenyewe au wote au kumuachia mama kilema/ugonjwa maishani .Hivyo kuna umuhimu Serikali kuweka mkono wake kwa kusaidiana na familia.

>>Kwenye jamii mama mjamzito amepewa hadhi ya peke yake ukiwa mahospitalini ,maofisoni hata kwenye vyombo vya usafiri utaliona hili , Hivyo kutoa kauli ya kutojali ya kujifungulia Nyumbani ukikosa gloves ni kugombana na Jamii .

>>Kisiasa Mama mjamzito ni Mali ya Serikali na taarifa zake zote lazima zihifadhiwe na kufuatiliwa kwa upekee ,Hapa Nguvu kazi inatengenezwa watu wakipunguza kuzaliana itakuwa shida ndio maana hata Serikali suala la uzazi limepewa kipaumbele.

2.Elfu hamsini sio hela ndogo , Watanzania wengi sana wanafanya kazi wanapata hela ambayo inaishia mahitaji ya kula , Mavazi na kulala ukiwa muajiriwa unaweza usiliewe hili lakini ndiyo hali halisi ya mtaani. Hata watu wanaotumia Bima ukiwastukiza walipe hata 2500 kwa Ajili ya kipimo au dawa katika 100 watakao mudu ni kama 10 tu

3.Afya ya Uzazi Msingi wa Uchumi na Maendeleo ya Nchi yoyote ile ,Nchi nyingi sana sasa hivi zinapambana kuongeza Raia , hivyo ni suala la kiserikali kwa asilimia kubwa . Katika hili suala Serikali inaweza fanya yafuatayo
>Kuhakikisha huduma za uzazi zinapatikana muda wote bure au kwa bei nafuu , kuwepo na taarifa maalumu ni vitu gani vitachangiwa na Serikali na vipi Mama mjamzito au

>Kuwepo Bima ya Uzazi ambayo itakuwa ya bei ya chini sana na itatumika kipindi cha ujauzito/uzazi .

Mwisho Kauli na maelezo ya RC Chalamila iamshe jamii kujipanga vizuri pindi inapopata mama mjamzito.
 
Habari JF , leo katika pitapita zangu nimekutana na kauli iliyozua maswali mengi sana kutoka kwa RC Chalamila , kwa ataeshindwa kununua gloves akajifungulie nyumbani .

Kimsingi inawezekana ni kauli sahihi katika mambo mengine ya afya lakini katika suala la uzazi ambalo lina faida kwa Serikali na familia inaweza isiwe sahihi kwa sababu :-

1.Kiafya ,Kijamii na kisiasa Mama mjamzito ni mtu anayehitaji mahitaji na huduma maalumu .







2.Elfu hamsini sio hela ndogo , Watanzania wengi sana wanafanya kazi wanapata hela ambayo inaishia mahitaji ya kula , Mavazi na kulala ukiwa muajiriwa unaweza usiliewe hili lakini ndiyo hali halisi ya mtaani. Hata watu wanaotumia Bima ukiwastukiza walipe hata 2500 kwa Ajili ya kipimo au dawa katika 100 watakao mudu ni kama 10 tu

3.Afya ya Uzazi Msingi wa Uchumi na Maendeleo ya Nchi yoyote ile ,Nchi nyingi sana sasa hivi zinapambana kuongeza Raia , hivyo ni suala la kiserikali kwa asilimia kubwa . Katika hili suala Serikali inaweza fanya yafuatayo




Mwisho Kauli na maelezo ya RC Chalamila iamshe jamii kujipanga vizuri pindi inapopata mama mjamzito.
watu wenye mashavu kuvimba wanatatizo
 
BILA SHAKA RAIS SAMIA AKIMALIZA UGENI ALIONAO ATAMTENGUA.
Na naomba iwe hivyo kwani kitendo chake kina athari kubwa kwa jamii na kwa watumishi wa hospitali ile.
 
BILA SHAKA RAIS SAMIA AKIMALIZA UGENI ALIONAO ATAMTENGUA.
Na naomba iwe hivyo kwani kitendo chake kina athari kubwa kwa jamii na kwa watumishi wa hospitali ile.
Yeah, nasikia analetwa Makongoro na mimi napewa Rukwa! Wacha tuone mkeka utakaosoma wiki ijayo! Huyu jamaa wasimrudishe tena kwenye utumishi wa umma ana maneno ya kijinga sana. Haya ndiyo madhara ya kutodhibiti mdomo! Mwanza nako aliongeaga ujinga hivi hivi wakamtengua Bi. Mkora naye sijui kwa nini alimrudisha!
 
Huenda alikuwa anajua anachokifanya au ameagizwa, na amesema hivyo ili kuhamisha mijadala fulanifulani.
Wanasiasa siyo watu kabisa...
 
Habari JF , leo katika pitapita zangu nimekutana na kauli iliyozua maswali mengi sana kutoka kwa RC Chalamila , kwa ataeshindwa kununua gloves akajifungulie nyumbani .

Kimsingi inawezekana ni kauli sahihi katika mambo mengine ya afya lakini katika suala la uzazi ambalo lina faida kwa Serikali na familia inaweza isiwe sahihi kwa sababu :-

1.Kiafya ,Kijamii na kisiasa Mama mjamzito ni mtu anayehitaji mahitaji na huduma maalumu .







2.Elfu hamsini sio hela ndogo , Watanzania wengi sana wanafanya kazi wanapata hela ambayo inaishia mahitaji ya kula , Mavazi na kulala ukiwa muajiriwa unaweza usiliewe hili lakini ndiyo hali halisi ya mtaani. Hata watu wanaotumia Bima ukiwastukiza walipe hata 2500 kwa Ajili ya kipimo au dawa katika 100 watakao mudu ni kama 10 tu

3.Afya ya Uzazi Msingi wa Uchumi na Maendeleo ya Nchi yoyote ile ,Nchi nyingi sana sasa hivi zinapambana kuongeza Raia , hivyo ni suala la kiserikali kwa asilimia kubwa . Katika hili suala Serikali inaweza fanya yafuatayo




Mwisho Kauli na maelezo ya RC Chalamila iamshe jamii kujipanga vizuri pindi inapopata mama mjamzito.
Kwenye mataifa yanayojali utu wa mtu huyu ingekuwa tayari keshapigwa chini
Kilichonishangaza zaidi kuna baadhi ya watu wamekubaliana naye tena wengine tunao hapa JF
 
Habari JF , leo katika pitapita zangu nimekutana na kauli iliyozua maswali mengi sana kutoka kwa RC Chalamila , kwa ataeshindwa kununua gloves akajifungulie nyumbani .

Kimsingi inawezekana ni kauli sahihi katika mambo mengine ya afya lakini katika suala la uzazi ambalo lina faida kwa Serikali na familia inaweza isiwe sahihi kwa sababu :-

1.Kiafya ,Kijamii na kisiasa Mama mjamzito ni mtu anayehitaji mahitaji na huduma maalumu .







2.Elfu hamsini sio hela ndogo , Watanzania wengi sana wanafanya kazi wanapata hela ambayo inaishia mahitaji ya kula , Mavazi na kulala ukiwa muajiriwa unaweza usiliewe hili lakini ndiyo hali halisi ya mtaani. Hata watu wanaotumia Bima ukiwastukiza walipe hata 2500 kwa Ajili ya kipimo au dawa katika 100 watakao mudu ni kama 10 tu

3.Afya ya Uzazi Msingi wa Uchumi na Maendeleo ya Nchi yoyote ile ,Nchi nyingi sana sasa hivi zinapambana kuongeza Raia , hivyo ni suala la kiserikali kwa asilimia kubwa . Katika hili suala Serikali inaweza fanya yafuatayo




Mwisho Kauli na maelezo ya RC Chalamila iamshe jamii kujipanga vizuri pindi inapopata mama mjamzito.
Chalamila amekosea kusema kweli kweli, ingawa ameongea ukweli. Unajua jinsi ya kufikisha ujumbe kwenye adhira ya watu wa Leval tofauti na ni kazi sana. Alipaswa kutumia, Lugha ya kistarabu kulingana na cheo chake. Twaswira ya mkuu ya mkoa ni twaswira ya Rais. Kwahiyo chochote anacho sema mkuu wa mkoa watu wanatafsiri kuwa ndiyo Rais alivyo mtuma, kwahiyo watu hawamjaji Chalamila ila wanamjaji aliye muweka. Kama kiongozi mkubwa kama yeye anapaswa ajue jinsi ya kumuwakilisha Rais kwenye vikao kwani sauti yake ni sauti ya Raisi wa nchi. Raisi hata siku moja hawezi kuongea Lugha kama hiyo, Raisi angewza kusema Kuw kuna Mama alinipigia simu kutaka msaada ili ajifungue nikampatia. Kwa sababu hii nchi inaendeeshwa kwa kodi za Watanzania na fedha nyingi zinatumika vibaya na wananchi wanajua.
 
Na hilo hasa ndio nililitarajia atafanya. Badala yake kaendeleza kiburi cha madaraka kwa kutoa sababu zisizo na mashiko yeyote.

Raisi Samia, ni wakati sasa Chalamila akapumzika nyadhifa za uteuzi zinahusiana na kusimamia watu.
 
Kama huna HELA jitahidi ukiwa unafanya starehe zako UTIMIE CONDOM.Itakusaidia kupunguza makasiriko.

📌Hivi aliowaambia maskini kuwa wao wana haki kwasababu ya kuwa mafukara ni nani.Yaani unalikuta jitu haliwezi hata kujihudumia ila bado linajitwika majukumu mengine ya ziada.

Huko Japana watu hata hawataki kusikia mambo ya ndoa,kwakua mtu anajipigia hesabu anaona mambo ya ulezi hana msuli nayo anaopt kujihudumia yeye kwanza au anaoata watoto mmoja au wawili📌📌

#Maskini mfanye kazi acheni kuendekeza NGONO!!!
 
Na hilo hasa ndio nililitarajia atafanya. Badala yake kaendeleza kiburi cha madaraka kwa kutoa sababu zisizo na mashiko yeyote.

Raisi Samia, ni wakati sasa Chalamila akapumzika nyadhifa za uteuzi zinahusiana na kusimamia watu.
HAKUNA BURE HAPA DUNIANI,FANYENI KAZI.

NCHI MASKINI KAMA HII WATU MILLION 60 WOTE MNATAKA MPATE VITU BUREBURE ALAFU HIYO MIUNDOMBINU ITAJENGWAJE???
 
HAKUNA BURE HAPA DUNIANI,FANYENI KAZI.

NCHI MASKINI KAMA HII WATU MILLION 60 WOTE MNATAKA MPATE VITU BUREBURE ALAFU HIYO MIUNDOMBINU ITAJENGWAJE???
Na wao serikali wafute kauli zao zile za kusema huduma bure wananchi wajuwe kuwa hakuna huduma za bure kila kitu ni kulipaaa

Ova
 
HAKUNA BURE HAPA DUNIANI,FANYENI KAZI.

NCHI MASKINI KAMA HII WATU MILLION 60 WOTE MNATAKA MPATE VITU BUREBURE ALAFU HIYO MIUNDOMBINU ITAJENGWAJE???
Kwanini wanatangaza kuwa huduma bure?

Kwanini wao viongozi wakitaka kuzaa hawaendi Temeke na michango ya 50,000 badala yake wanaenda Aga Khan?

Kuna baadhi ya watu wanaishi kwa mshahara wa 50,000 kwa mwezi, unatarajia atamudu vipi kutoa hiyo pesa kwa ajili ya kununua vifaa?

Usiwe na kiburi cha shibe kwa vile tu umemudu kupata mlo wako kwa uhakika. Sio kila fukara ni mvivu wa kufanya kazi.
 
Kama huna HELA jitahidi ukiwa unafanya starehe zako UTIMIE CONDOM.Itakusaidia kupunguza makasiriko.

📌Hivi aliowaambia maskini kuwa wao wana haki kwasababu ya kuwa mafukara ni nani.Yaani unalikuta jitu haliwezi hata kujihudumia ila bado linajitwika majukumu mengine ya ziada.

Huko Japana watu hata hawataki kusikia mambo ya ndoa,kwakua mtu anajipigia hesabu anaona mambo ya ulezi hana msuli nayo anaopt kujihudumia yeye kwanza au anaoata watoto mmoja au wawili📌📌

#Maskini mfanye kazi acheni kuendekeza NGONO!!!
Waalimu mkipata vihela kidogo mnasumbua
 
Kwenye mataifa yanayojali utu wa mtu huyu ingekuwa tayari keshapigwa chini
Kilichonishangaza zaidi kuna baadhi ya watu wamekubaliana naye tena wengine tunao hapa JF
Mshana, kwani sela ya afya iko vipi kwa mama mjamzito Tanzania. Tusiweke mambo ya huruma kwenye sela. Kama umeshawahi kwenda hospital na mama mjamzito,utakubaliana na alichosema chalamila. Tatizo letu sisi ni ,mtu akitusanua kwa kusema ukweli, tunachonga ili bi mkubwa amtimue. Rejea kauli ya Nape kuhusu chaguzi zetu. Haya nini kilitokea serikali za mitaa. Hawa watu tunatakiwa kuwapongeza kwa kusema ukweli
 
Asimfukuze afanye tu reshuffle Makonda Dar, Chalamila aende kwa Yule aliyekuwaga Dodoma akahamishwa nimemsahau jina kisha yule aende Arusha.
 
Mshana, kwani sela ya afya iko vipi kwa mama mjamzito Tanzania. Tusiweke mambo ya huruma kwenye sela. Kama umeshawahi kwenda hospital na mama mjamzito,utakubaliana na alichosema chalamila. Tatizo letu sisi ni ,mtu akitusanua kwa kusema ukweli, tunachonga ili bi mkubwa amtimue. Rejea kauli ya Nape kuhusu chaguzi zetu. Haya nini kilitokea serikali za mitaa. Hawa watu tunatakiwa kuwapongeza kwa kusema ukweli
Sela ndio nini
 
Mshana, kwani sela ya afya iko vipi kwa mama mjamzito Tanzania. Tusiweke mambo ya huruma kwenye sela. Kama umeshawahi kwenda hospital na mama mjamzito,utakubaliana na alichosema chalamila. Tatizo letu sisi ni ,mtu akitusanua kwa kusema ukweli, tunachonga ili bi mkubwa amtimue. Rejea kauli ya Nape kuhusu chaguzi zetu. Haya nini kilitokea serikali za mitaa. Hawa watu tunatakiwa kuwapongeza kwa kusema ukweli
kwa iyo sera ya afya inasema mama mjamzito akikosa pesa akajifungulie nyumbani au? Ebu tuambie iyo sera inasemaje.
 
Back
Top Bottom