RC Chalamila avunja mkataba wa Serikali na JWTZ wa ujenzi wa ofisi za halmashauri za Busokelo

RC Chalamila avunja mkataba wa Serikali na JWTZ wa ujenzi wa ofisi za halmashauri za Busokelo

Hii wanajaribu kuwaonyesha wanajeshi kwamba wao wanasiasa ndo wataalam (ndo kila kitu), ili ile fikra ya wajeda ya kwamba wao ndo wenye nchi waifute kabisa vichwan mwao. Hii hata jiwe itamfurahisha sana.
 
Kwa mara ya kwanza jeshi letu limeshindwa kazi, mkuu wa mkoa ametudhibitishia

Meja general mbuge alisema jeshi halijawahi shindwa sasa hapa mbona mkuu wa mkoa analizalilisha jeshi letu imara?
 
Chalamila ni kiumbe mjanja mjanja sana! Isije ikawa ameshatafuta mzabuni mwingine ili ale 10% ya faster faster! Maana huu ni mwaka wa uchaguzi.

Maamuzi yanaonekana ni ya kukurupuka kabisa. Yaani Msimamizi ameeleza wazi ya kwamba Halmashauri imekua ikitoa fedha za ujenzi kwa kusua sua! Badala ya kumkomalia DED atoe hela za ujenzi kwa wakati, yeye anaamua kuwadhalilisha Wanajeshi wetu!!
Huyo RC, amekuwa mkweli, tofauti na wengine ambao miradi mingi inayotekelezwa na taasisi za majeshi, kusua sua, na viongozi kuogopa kuwatimua kwenye kazi tofauti na wakandarasi wengine. Tatizo liko hapa ofisi nyingi za halimashauri zinajengwa chini ya tamisemi, hawatoi pesa kulingana na awamu za ujenzi, hivyo mkandarasi anashindwa kuendelea na kazi, na kama ingekuwa ni kampuni binafsi wanatishwa wanakopa pesa sehemu nyingine ili mradi uende tu, ila kama ni jwtz, pesa watatoa wapi?!! Mala ngapi jiwe ametoa maelekezo kwwnye taasisi ya TBA, kuwa wanakwamisha miradi kuisha kwa wakati?? Tatizo jingine kwenye gharama za ujenzi, wanatoa gharama ndogo kutafuta sifa, ila kazi ikianza tu ndio balaa, pesa hazitoshi kulingana na gharama halisi za ujenzi!! Yale maghorofa ya magomeni toka wapewe muda wa mwisho magereza, umefikia wapi?? Ma RC, DED, DC, wana kazi sana kwenye miradi inayosimamiwa na taasisi hizi, bora hata huyu amethubutu. Kwa mfumo wa sasa hakuna pesa ya kujenga jengo la halimashauri inayotoka halimashauri.
 
01 Julai 2020
Mbeya, Tanzania

HUU NI UPUUZI, HATUWEZI KUVUMILIA, NAVUNJA MKATABA, HATUWEZI KUBEMBELEZANA" - RC MBEYA MKUU



Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, amevunja mkataba wa ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Busokelo lenye kugharimu Bilion 5.2 baada ya kampuni ya Mzinga Holding Company kushindwa kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.

Source : Global TV online
16 Jun 2015 · Mzinga Corporation is a Government Institution under the Ministry of Defence. The Corporation's Head Office is in Mzinga, Pwani.
 
June 2, 2020
Busekelo, Mbeya
Tanzania

RC CHALAMILA ASOMEWA HISTORI YA MRADI
Historia ya ujenzi wa jengo la utawala Halmashauri ya Busekelo mkoa wa Mbeya toka mwaka 2013/ 14 ambao ulianza na kutokana kutopatiwa fedha 2015/ 2016 ulifikia phase ya kwanza kuweka msingi na mradi kusimama.

Pia 2017 pesa kidogo zililetwa hivyo mkandarasi wa kwanza akashindwa kuendelea na kazi. Mzinga Corp. mwaka 2018 wakapewa kazi lakini kasi ndogo ya fedha kuletwa ktk mradi imewapa changamoto kubwa Mzinga Corporation ktk kujaribu......2020


Source : HAROUB TV
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya hapa amepotoka kuwakoromea JWTZ wakati historia ya mradi huo ulioanza 2013 unaonesha pesa kidogo kupelekwa ktk mradi.

Serikali tajiri tangu 2017 imeshindwa kupeleka fedha ktk mradi huo hivyo kulidhalilisha shirika la Mzinga Coro.huku fedha haziwasilishi kwa wakati na hata zikifika ni kiduchu huku ni kutafuta kiki za kisiasa kuwalaumu Mzinga Corp.
 
Back
Top Bottom