RC Chalamila awataka wakazi wa DSM wajilinde Wao na familia zao dhidi ya matukio hatarishi badala ya kuwatupia Polisi lawama

watu watatu na smg unawazuiaje?
 
Una kichwa kigumu wewe cha kuelewa kama tofali za Mbozi. Ndio maana CHADEMA hainaga mawazo mapya miaka nenda rudi.
Nyie mngekuwa na mawazo mapya, miaka 60 kwenye uongozi nchi ingekuwa nyuma kiasi hiki?!
 
Mkuu wa mkoa wa DSM Albert Chalamila amewataka wananchi wa DSM kujilinda wao na familia zao dhidi ya matukio yoyote yanayoweza kuhatarisha Amani na Usalama wao

kwahiyo ulinzi wa kwanza ni wewe mwenyewe Raia”
Naunga mkono hoja ya RC Chalamila, tena nashauri kila kaya, kila familia ijengewe uwezo interms of capacity building, kila familia iweze kujilinda kama RC Chalamila alivyo jilinda kama alivyoeleza hapa This man is either a sadist or alimuua kibaka, akanywa bia kusherehekea?
View: https://youtu.be/DU2KYclh1l8?si=75ZpspiMj0XVDSbNP
 
Kwa kauli hii CCM rasmi mmefungua milango ya kufanya uangalizi upya wa namna raia wanaweza pata mafunzo ya kujilinda bila kusahau kumiliki Silaha 😂
 
Mafwele weeh.
Msanii wa kuvamia na kupotea, kazi zako njema Sana machoni pa Mtawala wa Urithi toka nchi za Kisultani.
mawachukua misukule mnasingizia mambo mengineyo, si sawa.

acheni ramli chonganishi na ushirikina mara moja sawa gentleman na wenzako?🐒

ramli ndio satellites zenu sio?
 
Chalamila apimwe ngoma huwenda imepanda kichwani
 
Ameongea vizuri tofauti na kichwa cha habari
 
Mnaweza kumlaumu ila kwa Mara ya kwanza ameongea point. Jukumu la usalama wetu ni letu wenyewe kuwa kuanzia halafu ndio hao vyombo vya kipolisi. Sema wangepunguza masharti kule kwenye umiliki wa silaha
 
Unafiki ndio tatzo
 

Kauli aliyotoa huyo RC wa huko Dsm Bw. Chalamila unaweza ukaichukulia kuwa ni kauli nyepesi Sana, lakini ukiichambua kwa kina Sana ni Kauli nzito Sana, hii ni kutokana na Mazingira halisi ya kiusalama ambayo ni tete Sana yaliyopo hivi Sasa hapa nchini. Hii kauli unaweza ukaiita kuwa ni Declaration of a full scale war between the Innocent Civilians against the Police/Tiss Officials who are allegedly to be involved in the activities of Abducting Civilians. Hiyo kauli yake ni ya hatari Sana kwa mustakabali mwema wa usalama wa watu na mali zao. Sina uhakika kuwa kabla ya huyo RC kutoa kauli hii hadharani alijaribu kutafakari kwanza juu ya mapokeo ya wananchi kuhusu hoja yake hiyo. I' not sure.
Kauli Kama hiyo ya huyo RC wa Dsm iliwahi kutolewa na baadhi ya Watawala wa nchini Afrika ya Kusini enzi za utawala wa ubaguzi wa rangi, hali iliyosababisha reaction mbaya Sana kutoka kwa raia wa nchi hiyo (hususani watu weusi) ambao nao waliamua kujibu mapigo kwa kuanzisha kampeni ya kujihami, kampeni hiyo ilikuwa kali na ya hatari zaidi ambayo waliyoiita kwa jina la 'We are Fighting Back,' Hiyo kampeni ndio iliyoilazimisha Utawala wa Makaburu enzi hizo kuamua kutoa tangazo la Hali ya Hatari (The State of Emergency) kwa nchi nzima, tangazo hilo lilidumu kwa miaka mingi Sana na kugharimu maisha ya Watu wengi Sana katika nchi hiyo.
Nafikiri watawala wetu waliopo hapa nchini wanapaswa wajifunze historia ya mambo kama haya kutoka kwa wenzetu katika nchi zingine ambako nao pia waliwahi kupitia hali Kama hii tunayopitia Sasa hivi hapa Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…