RC Chalamila: Hajatekwa, amejipoteza mwenyewe

RC Chalamila: Hajatekwa, amejipoteza mwenyewe

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akizungumza kwenye sherehe za kuweka Wakfu jengo la Ibada la Kanisa la Waadventista wa Sabato Magomeni, leo Disemba 15, 2024.

"Mkoa wa Dar es Salaam uko salama, hizo habari zinazosambaa za mtu kutekwa sio za kweli na hivi karibuni mtasikia wenyewe nini kilisababisha apotee"

Pia, Soma: Mke wa Ulomi asimulia sakata la kupotea kwa mumewe

Kufuatia taarifa zinazozagaa mitandaoni, Jeshi la Polisi limetoa ufafanuzi kwa mujibu wa ushahidi uliokusanywa.

Vincent Peter Massawe, ambaye taarifa za kupotea kwake ziliripotiwa tarehe 19.11.2024, alithibitishwa kuwa na harusi tarehe 16.11.2024. Baada ya harusi, aliazima gari aina ya Toyota Ractis (T.642 EGU) kwa shughuli hizo lakini hakulirejesha. Badala yake, tarehe 18.11.2024, aliuza gari hilo kwa shilingi milioni tisa, akalipwa milioni nane, na kiasi kingine alituma kwa mke wake kulipia madeni ya harusi.

Gari hilo limekamatwa, na ushahidi unaonyesha Massawe pia anadaiwa na watu wengine jumla ya shilingi milioni 69. Uchunguzi unaendelea kubaini ukweli wa tukio hili, na taarifa rasmi zitatolewa baada ya mahojiano zaidi, hasa na mke wake, ambaye inaaminika ana taarifa muhimu.
IMG_1630.jpeg
 
Sasa mtu dalali wa magari serikali ikuteke kwa lipi,wakati wewe siyo mwanaharakati wala hujishugulishi na siasa
Kipindi cha nyuma na huwa napenda sana kusema humu kuna watu wanapita na huu upepo,wa kutekana
Watu wamedhulumiana,watu wanadaiana hata kuna watu wakijuwa fulani ana hela wanakuja kukuteka !
Na ukiona mpaka imefika watu wanatekana basi watu hawana imani na mamlaka za kusimamia haki na sheria

Ova
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akizungumza kwenye sherehe za kuweka Wakfu jengo la Ibada la Kanisa la Waadventista wa Sabato Magomeni, leo Disemba 15, 2024.

"Mkoa wa Dar es Salaam uko salama, hizo habari zinazosambaa za mtu kutekwa sio za kweli na hivi karibuni mtasikia wenyewe nini kilisababisha apotee"
View attachment 3177258

Kufuatia taarifa zinazozagaa mitandaoni, Jeshi la Polisi limetoa ufafanuzi kwa mujibu wa ushahidi uliokusanywa.

Vincent Peter Massawe, ambaye taarifa za kupotea kwake ziliripotiwa tarehe 19.11.2024, alithibitishwa kuwa na harusi tarehe 16.11.2024. Baada ya harusi, aliazima gari aina ya Toyota Ractis (T.642 EGU) kwa shughuli hizo lakini hakulirejesha. Badala yake, tarehe 18.11.2024, aliuza gari hilo kwa shilingi milioni tisa, akalipwa milioni nane, na kiasi kingine alituma kwa mke wake kulipia madeni ya harusi.

Gari hilo limekamatwa, na ushahidi unaonyesha Massawe pia anadaiwa na watu wengine jumla ya shilingi milioni 69. Uchunguzi unaendelea kubaini ukweli wa tukio hili, na taarifa rasmi zitatolewa baada ya mahojiano zaidi, hasa na mke wake, ambaye inaaminika ana taarifa muhimu.
View attachment 3177269
Kuuza gari, kulipa madeni hakuthibitishi kuwa kajiteka mpaka atakapopatikana na kugundulika labda alikimbia nchi au amejificha.
 
Sasa mtu dalali wa magari serikali ikuteke kwa lipi,wakati wewe siyo mwanaharakati wala hujishugulishi na siasa
Kipindi cha nyuma na huwa napenda sana kusema humu kuna watu wanapita na huu upepo,wa kutekana
Watu wamedhulumiana,watu wanadaiana hata kuna watu wakijuwa fulani ana hela wanakuja kukuteka !
Na ukiona mpaka imefika watu wanatekana basi watu hawana imani na mamlaka za kusimamia haki na sheria

Ova
Kwenye msafara wa mamba na kenge wamo. Wale wanaoteka kwa mrengo wa kisiasa, aliyetekwa hupotezwa(Huuawa). Lakini aliyetekwa kwa mrengo wa kibiashara; watekaji hudai kiasi fulani cha fedha (mortigage/ransom) fidia ili huyo aliyetekwa aachiwe ( kumkomboa)au arudishwe. Hivyo ni vitu viwili tofauti.
 
Naona huu mchezo wa kutekwa ndiyo unaingia Tanzania. Ulianzia Marekani, mara zote waliotekwa au kutekwa walikuwa na majina ya Kabila moja, Italians. Kwa TZ tunaona wanaotekwa wana majina ya Kabila moja, tangu Soka, Mlay, Mbowe, Massawe, Urassa, wengi wana CHADEMA? Hii ni bahati mbaya, au ni elimu? Wamesoma mbinu za Marekani kwa ujasiriamali?
 
Back
Top Bottom