RC Chongolo akabidhi gari la Wagonjwa, apongeza maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Momba

RC Chongolo akabidhi gari la Wagonjwa, apongeza maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Momba

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Screenshot 2025-01-29 151124.png

Screenshot 2025-01-29 151136.png
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe.Daniel Chongolo, amepongeza maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Momba iliyopo katika Kata ya Chitete, akibainisha kuwa licha ya kasoro ndogo zilizojitokeza, majengo yaliyojengwa ni mazuri na yanaonesha matumizi mazuri ya rasilimali. Alisema hayo wakati wa ziara yake ya siku moja kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Momba.

"Tumekuja hapa kukagua na kujiridhisha kuhusu matumizi ya fedha ambazo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amezishusha kwa ajili ya miradi ya maendeleo ili kuboresha huduma za jamii," alisema Mhe. Chongolo.
Screenshot 2025-01-29 151200.png

Screenshot 2025-01-29 151147.png
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mganga Mfawidhi (MOI) wa Hospitali ya Wilaya hiyo, Dkt. Faraja Mwinuka, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Fabian Manoza, ujenzi wa hospitali huo ulianza Aprili 2024 kwa gharama ya shilingi milioni 796 na unatarajiwa kukamilika Januari 2025.

Mkandarasi alipata nyongeza ya muda kutokana na changamoto ya kusafirisha vifaa vya ujenzi. Dkt. Mwinuka alisema kuwa ujenzi huo unahusisha majengo manne, yakiwemo jengo la maabara, jengo la mionzi, jengo la kufulia, na stoo ya dawa. Hadi sasa, jumla ya shilingi milioni 583 zimetumika, na hatua za mwisho zikiendelea, ikiwa ni pamoja na uwekaji wa marumaru na kufunga milango. Kukamilika kwa hospitali hiyo kutasaidia wananchi wa maeneo ya Kata za Chitete na Msangano, na kupunguza changamoto ya kusafiri umbali mrefu kwa ajili ya huduma za afya.
Screenshot 2025-01-29 151616.png

Screenshot 2025-01-29 151616.png
 
Huenda Leo chongolo ndo angekuwa makamu wa Rais
 
Kweli hii ni Afrika sasa nimeamini, hapo gloves ndani ya hospital hakuna ila gari limenunuliwa na linalala kwa dereva wa hilo gari sio hospital na dereva analitumia hilo gari km lake sio km la hospital, naakubari nakubari mama mjamzito akifika hapo akatoe 50,000/- ya gloves?
 
Back
Top Bottom