Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Godfrey Chongolo ameongoza Mkutano wa Nane wa Baraza la Biashara la Mkoa huo.
Mkutano huo umefanyika Jumanne Disemba 11, 2024 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Nselewa Wilayani Mbozi.
Katika Mkutano huo Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Songwe (Songwe, Mbozi, Ileje na Momba) wamewasilisha taarifa za kufanyika kwa Mabaraza ya Biashara katika Wilaya zao.
Aidha, katika Mkutano huo kumewasilishwa wasilisho juu ya namna sekta ya madini itakavyoweza kufungua Mkoa huo kiuchumi.
Pia, zimewasiloshwa Sheria na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha kwa wadau wa Mkutano huo.
Pamoja na mambo mengine, Mhe. Chongolo amefanya uzinduzi na ugawaji wa Vitambulisho vya Wafanyabiashara Ndogondogo katika Mkoa huo.
Mkutano huo umefanyika Jumanne Disemba 11, 2024 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Nselewa Wilayani Mbozi.
Aidha, katika Mkutano huo kumewasilishwa wasilisho juu ya namna sekta ya madini itakavyoweza kufungua Mkoa huo kiuchumi.
Pia, zimewasiloshwa Sheria na Kanuni za Huduma Ndogo za Fedha kwa wadau wa Mkutano huo.
Pamoja na mambo mengine, Mhe. Chongolo amefanya uzinduzi na ugawaji wa Vitambulisho vya Wafanyabiashara Ndogondogo katika Mkoa huo.