Pre GE2025 RC Kunenge awataka TANROADS na TARURA kumaliza miradi ya barabara iliyoahidiwa na CCM 2020

Pre GE2025 RC Kunenge awataka TANROADS na TARURA kumaliza miradi ya barabara iliyoahidiwa na CCM 2020

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2018
Posts
882
Reaction score
3,337
Kunenge alitoa agizo hilo katika mkutano wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Pwani uliofanyika Kibaha, ukiwahusisha wadau wa maendeleo na wataalamu wa sekta hiyo.

Alisisitiza umuhimu wa kuwa na mpango wa utekelezaji wa ujenzi wa barabara, hasa zile zilizokuwa sehemu ya ahadi za uchaguzi. Pia, alihimiza tathmini ya barabara zilizokamilika, zinazoendelea, na zile ambazo hazijaanza, huku kipaumbele kikiwekwa kwenye barabara muhimu zaidi.

"Tunapaswa kutambua ni barabara zipi zimekamilika, zipi bado na zipi hazijaanza. Waheshimiwa wabunge wanapaswa kutueleza barabara chache zenye umuhimu wa kipekee ili zipewe kipaumbele, hata kama ni tano au kumi, ni lazima tujue zipi tunapaswa kuzitekeleza haraka ili kuepuka msukosuko kwa serikali na chama.

Aliendelea kueleza kuwa utekelezaji wa miradi hiyo unapaswa kuzingatia maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Alisisitiza kuwa barabara zenye mchango mkubwa kwa uchumi zinapaswa kupewa kipaumbele, huku serikali ikiepuka miradi inayoweza kuwa mzigo mkubwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti, alieleza kuwa miundombinu ya barabara ni changamoto kubwa Kisarawe kutokana na milima mingi na bajeti ndogo. Alisema wananchi wanalia kuhusu hali mbaya ya barabara, jambo linalohatarisha nafasi za viongozi katika uchaguzi ujao.

"Tunaelekea kipindi cha mvua na pia kampeni zinakaribia. Kila mkutano ninaofanya, asilimia kubwa ya maswali ni malalamiko ya wananchi kuhusu barabara. Wilaya yetu ina historia ya zaidi ya miaka themanini, lakini tuna kilomita saba pekee za lami. Hali hii inafanya kuwa changamoto kubwa kwa wabunge na madiwani wetu katika uchaguzi ujao,"

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Watu waishio pembezoni mwa barabara ya mzenga-mlandizi-bagamoyo wamefanyiwa tathmini zaidi ya miaka kumi sasa kwa ajili ya kulipwa ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami lakini mpaka sasa hakuna malipo yoyote yaliyofanyika, wananchi wamezuiwa kuendeleza ardhi yao kwa namna yoyote
 
Watu waishio pembezoni mwa barabara ya mzenga-mlandizi-bagamoyo wamefanyiwa tathmini zaidi ya miaka kumi sasa kwa ajili ya kulipwa ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami lakini mpaka sasa hakuna malipo yoyote yaliyofanyika, wananchi wamezuiwa kuendeleza ardhi yao kwa namna yoyote
Hiyo sawa na utapeli tu

Ova
 
Kunenge alitoa agizo hilo katika mkutano wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Pwani uliofanyika Kibaha, ukiwahusisha wadau wa maendeleo na wataalamu wa sekta hiyo.

Alisisitiza umuhimu wa kuwa na mpango wa utekelezaji wa ujenzi wa barabara, hasa zile zilizokuwa sehemu ya ahadi za uchaguzi. Pia, alihimiza tathmini ya barabara zilizokamilika, zinazoendelea, na zile ambazo hazijaanza, huku kipaumbele kikiwekwa kwenye barabara muhimu zaidi.

"Tunapaswa kutambua ni barabara zipi zimekamilika, zipi bado na zipi hazijaanza. Waheshimiwa wabunge wanapaswa kutueleza barabara chache zenye umuhimu wa kipekee ili zipewe kipaumbele, hata kama ni tano au kumi, ni lazima tujue zipi tunapaswa kuzitekeleza haraka ili kuepuka msukosuko kwa serikali na chama.

Aliendelea kueleza kuwa utekelezaji wa miradi hiyo unapaswa kuzingatia maagizo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Alisisitiza kuwa barabara zenye mchango mkubwa kwa uchumi zinapaswa kupewa kipaumbele, huku serikali ikiepuka miradi inayoweza kuwa mzigo mkubwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti, alieleza kuwa miundombinu ya barabara ni changamoto kubwa Kisarawe kutokana na milima mingi na bajeti ndogo. Alisema wananchi wanalia kuhusu hali mbaya ya barabara, jambo linalohatarisha nafasi za viongozi katika uchaguzi ujao.

"Tunaelekea kipindi cha mvua na pia kampeni zinakaribia. Kila mkutano ninaofanya, asilimia kubwa ya maswali ni malalamiko ya wananchi kuhusu barabara. Wilaya yetu ina historia ya zaidi ya miaka themanini, lakini tuna kilomita saba pekee za lami. Hali hii inafanya kuwa changamoto kubwa kwa wabunge na madiwani wetu katika uchaguzi ujao,"

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kwenye swala la barabara za lami kwenye mitaa ya mkoa wa pwani mnatia aibu sana,li mkoa lina viwanda karibu kila uchochoro lakini sijui hizo hela mnazokusanya kodi mnapeleka wapi,halafu hakuna eneo linalonipa kero kama hilo li pori la Tumbi hapo kuanzia TAMCO mpaka Picha ya ndege,miaka nenda rudi liko vilevile hakuna cha maana kinachofanyika hapo.....
 
Mkuu wa mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge amezitaka Wakala wa barabara Tanzania TANROADS na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini TARURA, kushughulikia barabara ambazo waliahidiwa Wananchi katika kampeni za CCM katika Uchaguzi Mkuu uliopita mwaka 2020 ili zisije kuleta msuko suko mkubwa kwa CCM kwenye uchaguzi mkuu ujao kwasababu wananchi watapima serikali kwa namna ilivyotekeleza ahadi zake.

Amesema hayo katika mkutano wa bodi ya barabara ya mkoa iliyofanyika mjini Kibaha mkoani Pwani na kuhusisha wadau mbalimbali wa Maendeleo na wataalamu.

Pia soma: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Kunenge amesema ni lazima kuwe na mipango ya utengenezaji wa barabara kwa maendeleo katika mkoa kwa kuanzia kwanza barabara ambazo waliahidi Wananchi kwamba zipi zimekamilika na zipi bado zipo katika utekelezaji na zipo kwenye hatua gani.

“Na tuone na zile barabara ambazo hatujaanza kabisa na tujue kipaumbele ni barabara zipi na zitakamilishwa kutokana na fedha zipi na waheshimiwa Wabunge watueleze ni barabara zipi zipewe kipaumbele hata kama ni tano hata kumi zipi hizo zipewe kipaumbele zitatupa msukosuko mkubwa” alisema RC Kunenge.

“Hata akija Kiongozi mkubwa zitaleta msukosuko mkubwa yaani lazima tuzijue na tuziwekee mkakati kulingana na maagizo ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan” alisema Kunenge.

“Angalieni zipi mmezitekeleza na zipi bado hamjazitekeleza na tutoe sababu kwanini hatujazitekeleza na tuone kama tutaenda nazo kwani tunafahamu tuna majukumu mengi lakini hizi barabara tukiziangalia zinaweza kutupa unafuu”-RC Kunenge.
1741331564930.jpeg
 
Back
Top Bottom