RC Kunenge: Mvua zimesababisha vifo vya watu 12, nyumba 107 zimesombwa na maji na nyingine 800 zimezingirwa!

RC Kunenge: Mvua zimesababisha vifo vya watu 12, nyumba 107 zimesombwa na maji na nyingine 800 zimezingirwa!

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mvua yaacha vilio Dar

WATU 13 wamefariki dunia, wakiwamo wanane ambao vifo vyao vimetokana na mvua kubwa iliyonyesha juzi jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi, watu watano ambao ni wa familia moja wamefariki dunia baada ya nyumba waliyokuwa wakiishi kuungua moto.

dar.jpg

Akizungumza na Nipashe jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Janet Magomi, alisema vifo vilivyotokana na mvua vimetokea Mto Msimbazi.

Alisema kwamba, Mto Msimbazi eneo la Kariakoo kulikutwa miili ya watu watano ambayo imehifadhiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na kati yake, mitatu tayari imeshatambuliwa na ndugu zao.

“Maeneo ya Buguruni, kuna taarifa ya watu wengine wawili, mwanaume na mwanamke ambao miili yao iliokotwa kwenye mto na maeneo ya Ukonga ipo taarifa ya mtu mmoja aliyeokotwa Mto Mvule, miili yote ipo Muhimbili,” alisema.

Kamanda Magomi alisema kati ya watu hao waliofariki dunia kutokana na mvua hizo za juzi, watoto ni wawili.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, watoto hao walifariki dunia wakati wakisaidiana kuokoana kwenye Mto Msimbazi.

Kuhusu tukio la moto, Kamanda Magomi alisema lilitokea juzi saa nne usiku Kata ya Pugu, Tarafa ya Ukonga wilayani Ilala jijini.
“Kuna nyumba iliungua na wamefariki wanafamilia watano ambao ni mke, watoto watatu na wifi ambaye ni mdogo wa mume wa mke aliyefariki dunia,” alisema.

Kamanda Magomi alisema watu hao walifariki dunia baada ya kufikishwa hospitalini.

“Walikuwa hawana majeraha wakati wakipelekwa hospitali, lakini wakati wakitaka kupatiwa matibabu, walionekana wameshafariki dunia, chanzo cha moto huu tunaendelea kuchunguza ila mashuhuda wanasema ulianzia sebuleni," alisema.

Aliongeza kuwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lilifika eneo hilo la tukio na kuuzima ili usiendelee kuleta madhara zaidi.
 
Watoto walikuwa wanaokoana na watu wanawaangalia tu mpaka wakapoteza maisha wote wawili
 
... counter attack ya mvua ya juzi sio mchezo! Disaster preparedness nchi hii ni zero!
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge amesema jumla ya watu 12 wamekufa kufuatia mvua kubwa iliyonyesha juzi 13/10/2020.

Kadhalika nyumba 107 zimesombwa na maji na nyingine zaidi ya 800 bado zimezingirwa na maji.

Serikali inaendelea kufuatilia athari mbalimbali zilizojitokeza na kutolea suluhisho stahiki, amesema RC.

Chanzo: Ayo TV

Maendeleo hayana vyama!
 
Poleni sana wahanga wa mafuriko pamoja na yote kura zenu za hasira 28 sio mbali
Wapo miongoni mwa wahanga wameongeza tatizo kwa kwenda kujenga kwenye njia za maji na kupunguza mtiririko wa maji, upo pia uzembe wa serikali wenye wajibu wa kujenga miundombinu ya maji. Pia ipo nafasi ya janga la asili, Japan pamoja na uimara wake kwenye uchumi na teknolojia hawajawahi kupata muarubaini wa kudumu kwenye majanga yanayowakumba.
 
Halima Mdee ,ametuponza watu wa Dar,
Kaleta Hadi mvua za mafuliko na kusababisha maafa.
 
Hasira za airport ya kimataifa ya Chato wakati hizo fedha zingejenga mitaro
Mlisha laanika nyie
Hamna jema hovyo tu na chuki zenu
Nyie hamna jema Na Vi ID vyenu kumi kumi humu
 
Hasira za airport ya kimataifa ya Chato wakati hizo fedha zingejenga mitaro
... yap! Hiyo ndio maana halisi ya maendeleo ya watu; miradi inayogusa moja kwa moja the common wananchi badala ya kuonesha ufahari usio na maana kama kujenga international airport kijijini; kununua madege ya kifahari ambayo since then yako grounded; madaraja ya baharini ilhali watu wanakufa kwa mafuriko simply mitaro imeziba or the masses wanapata adha za ajabu mvua zinaponyesha!
 
Hivi wale matapeli wa hali ya hewa waliosema leo mvua itakuwa kubwa kuliko ya juzi wako wapi? Juzi nilikuambia hivi huwa kuna watu wanawasikilizaga hao matapeli wa hali bya hewa?
 
Back
Top Bottom