RC Makalla atoa Wiki moja kukomeshwa biashara ya ngono, awataka Polisi kuvaa kiraia na kujifanya wateja


Nampongeza Mkuu wa Mkoa Amos Makalla. Pamoja na mapungufu ya hapa na pape, lakini serikali yetu bado ni sikivu na kiwango fulani cha hofu ya Mungu.
Hili ni jema na huleta ulinzi wa Mungu kwa taifa dhidi ya majanga, matememeko, mafuriko, vita, magaidi, magonjw ank.
 
Huyu Makala naye hajitambui! Sasa ndio kwanza anaishamirisha biashara kwa kuwapa gear ya kuingia rais wale polisi waliokuwa wanasitasita! Unamtumaje mtu mwenye njaa akatupe chakula kibovu kama siyo umekusudia akakile😃!? Hao polisi chondechonde wasiwabake tu kama wataamua kuonja tunda na wawalipe kwa huduma kama kawaida!
Makala, nenda kwa Kolomoje ukachukue desa la namna bora ya kupambana na biashara hiyo ambayo inawezekana hata waandamizi wako ni wateja wazuri😃😜!
 
Kwa namna hiyo biashara inavyoendeshwa kwa sasa kutokana na maendeleo ya teknolojia sidhani kama itakuwa rahisi hivyo....wanaweza kumalizana na wale wanaojipanga barabarani hovyo hovyo na kwenye madanguro..

Lakini hawa wanaokuwa ndani ya clubs na bars usiku na mchana hakuna namna maana wanaweza kuwa kama wateja wengine waliokuja kuburudika huku biashara inaendelea...wapo wale ambao ni online na wateja wao wako online ni mwendo wa simu, facebook na whatsap, wapo wale wenye maagent wao wakiwemo bodaboda wewe ni kuagiza tu anatoka home anakuja...

NINI KIFANYIKE KUPUNGUZA AU KUKOMESHA?
Serikali iwekeze sana kwenye mifumo ya maisha kitabia ya watu wake kuanzia wadogo kwa maana mashuleni, mitaani na majumbani....
Mfumo wa elimu huko mashuleni bado hauko sawa, kuanzia elimu yenyewe na maadili ili kushape kizazi na vizazi..
Viongozi wa dini washirikishwe sana kwenye mafundisho yao kwa watu hasa watoto.
Wizara ya Ustawi wa jamii ipewe nguvu sana kudeal na malezi ya watu huko mitaani na kutengenez uelekeo wa kimaadili.
Serikali ijitahidi kupunguza tatizo la ajira linalokuwa kwa kasi ili angalau raia waweze kuishi kama binadamu huko mitaani..
Mfumo wa elimu uboreshwe ili jamii iwe na watu wengi wenye uelewa mitaani na kujitengenezea ajira wenyewe.
 
this is funny to me..let wait see....his predecessor fails...i wonder what strategies he will use...
 
Imetajwa kwenye Biblia na Quran. Ipo siku zote. Hii sio mara ya kwanza kutaka kuomdolewa na ika survive!....kwa sababu ipo toka enzi za Quran na Biblia vinaandikwa !!!
 
Nilijua dar nzima aisee,kumbe hapo tu, vijiwe vingine nauli yake haifiki hata 400 kutokea hapo mabaharia kuliko kukamatwa inabidi tu mjiongeze.
 
Ulichokifanya hapo ndio umevifanyia promotion hivyo vituo, hizo sehemu kuna watu wataenda kujionea sababu walikua hawajahi kufika.
 
Hayo machimbo ni makongwe wala hayahitaji ufichuzi wowote..labda useme massage centers
 
Umalaya unafanyika hadi maofisini mpaka kwenye mabunge aache zake hizo hiyo mambo anataka watu wapone wapi sasa baadae watakuja kukamata wanywa pombe usiku...wewe kama hununui waache watu waburudike siku ukimkamata muhuni nyumbani kwako utajua kuwa haya machimbo ni ulinzi mzuri kwa wake na wanafunzi...jitu zima linapigwa mzigo wewe unaumia nini?
 
Acheni wivu aisee na kuingilia starehe za wenzenu, serikali ifanye tu utaratibu waanze kulipa kodi na wazingatie kanuni za afya na usafi.
 
Hiyo ndio changamoto kubwa ya maisha magumu ya Daresalama!?
 
Kiukweli kabisa kutoka kumoyo hii operation sijaipenda kabisaaaaa.

Waache kina dada wajiingizie kipato, mi nashauri waboreshe sio kuighasighasi namna hii. Wanataka sie madomo zege tukabake ama??

Mi nashauri tu kama hao wa uwanja wa fisi na m/nyamala walio karibu kabisa na makazi ya watu wahame, wapelekwe eneo ambalo halina makazi ya watu ili kuepusha watoto kuona kinachotendeka. Ama lah baadhi ya bar zirihusiwe kabisa na zilipe kodi kama kawa.

Au mnasemaje wakulungwa wa kusuuza rungu kwa buku jero.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…